Masokotz
JF-Expert Member
- Nov 26, 2018
- 3,495
- 5,532
Ilikuwa April 2017,
Niliamka Asubuhi nikiwa na mawazo mengi sana,Haikuwa mara ya kwanza mm kuamka asubuhi ila siku hii ilikuwa tofauti.Wawili kati ya watu niliokuwa nafanya nao kazi ambao walikuwa na uzoefu waliamua kuacha kazi na kwenda katika kampuni nyingine na nilibaki na timu ndogo ya watu wa chache sana ambao sijui kama na wao walikuwa na mpango wa kuondoka au la.
Hatukuwa na Pesa benki hata ya kuweza kulipia Bills za kawaida na tayari tulikuwa na madeni kadhaa ambayo yalikuwa yanaumiza vichwa vyetu.Vile vile tayari nilishaanza kuchoka hasa baada ya kuona kwamuda kwamba Biashara niliyokuwa nafanya bado ilikuwa haijawez kutengeneza mapato ya uhakika ya kuweza kugharamikia shughuli za kuendesha ofisi.Kwa ufupi hakukuwa na Mauzo kabisa.
Wenzangu ambao nilikuwa nafanya nao kazi hasa ambao niliwaajiri walikuwa wanajua tuna shida ila hawakujua ukubwa wa shida zetu na kwa kweli wazo al kuwaambia kwamba sasa tumeamua kufunga kampuni na kila mmoja aangalie ustaarabu mwingine ni wazo ambalo liliumiza sana moyo wangu.
Nilshajaribu kufikiri zaidi kuhusu namna bora ya kuweza kuhakikisha biashara inaendelea kuwepo ila jitihada nyingi zilikuwa hazina matokeo.Ulikuwa ni wakati wa maamuzi magumu.
Nilijianda kwa unyonge na kuelekea Ofisini ambapo nilikuta wafanyakazi wote wameshawasili.NIliitisha kikao cha wafanyakazi wote nikawaweleza hali halisi ya kampuni na kuwaambi sina namna zaidi ya kuachana na biashara niliyokuwa naifanya.Kwa kweli walipata mshtuko hasa ukizingatia kwamba wengi walikuwa ndio ajira yao ya kwanza na pia walishazoe mazingira ya kazi na tulishakuwa kama ndugu pale ofisini.Hivyo baada ya kuwaambia kwamba tunafunga kampuni moja kwa moja walijaribu kutoa maoni mbalimbali lakini mm nilishafanya maamuzi na ulikuwa ni wakati wa kwenda kufanya jambo jingine.
Baada ya kuwaeleza niliwaomba wote waandika barua ya kuomba kuacha kazi na kisha nitawaapa nyaraka zote za muhimu ikiwa cheti cha huduma bora,barua nzuri ya recommendation na msaada wowote ule ambao watahitaji katika kutafuta ajira mpya.
Baada ya kuwaeleza yote na kunielewa niliwapa nafsi ya kuuliza maswali.Mmoja wao aliniuliza swali ambalo lillinishangaza sana.Aliniuliza WHAT ABOUT YOU.Sasa itakuaje kuhusu WEWE?Kwanza sikutarajia swali kama hilo hivyo nilianza kwa kujaribu kudownplay kisha nikawaambia kwa kiingereza.
"I will have to hold the fort,I am a startup creature and I will move to the next Idea and hopeful the money will come" Kabla ya kuanzisha biashara hii nilishaanza biashara nyingine kadhaa na hata baada ya biasharahi nitaanzisha biashara nyingine.Katika ulimwengu wa biashara na hasa biashara zinazoanza kuna changamoto nyingi hata hivyo changamoto kubwa kuliko zote ni kupata wateja hasa wateja wanaoweza kulipa vizuri.
Ndio maana mara nyingi unapoanzisha biashara unashauriwa sana kuzingatio masoko/wateja kawani unapokuwa na uhakika wa soko basi kutengeneza bidhaa au huduma ni jambo rahisi sana.
Je, umewahi kulazimikakufunga biashara yako iwe ndogo au kubwa? Je, ulijisikiaje? Je kufunga biashara kulikufanya uvunjike moyo wa kuanzisha biashar nyingine? Je, uliendelea kuanzisha biashara mpya?Je umeshakutana na biashara ambayo imekutoa kifedha na kimaisha?Karibu tujadili zaidia.
Iwapo una kampuni ambayo ni Dormant au biashara ambayo unataka kuifunga na unahitaji kupata uzoefu wetu na ushauri tafadhali wasiliana nasi kwa email masokotz@yahoo.com
Niliamka Asubuhi nikiwa na mawazo mengi sana,Haikuwa mara ya kwanza mm kuamka asubuhi ila siku hii ilikuwa tofauti.Wawili kati ya watu niliokuwa nafanya nao kazi ambao walikuwa na uzoefu waliamua kuacha kazi na kwenda katika kampuni nyingine na nilibaki na timu ndogo ya watu wa chache sana ambao sijui kama na wao walikuwa na mpango wa kuondoka au la.
Hatukuwa na Pesa benki hata ya kuweza kulipia Bills za kawaida na tayari tulikuwa na madeni kadhaa ambayo yalikuwa yanaumiza vichwa vyetu.Vile vile tayari nilishaanza kuchoka hasa baada ya kuona kwamuda kwamba Biashara niliyokuwa nafanya bado ilikuwa haijawez kutengeneza mapato ya uhakika ya kuweza kugharamikia shughuli za kuendesha ofisi.Kwa ufupi hakukuwa na Mauzo kabisa.
Wenzangu ambao nilikuwa nafanya nao kazi hasa ambao niliwaajiri walikuwa wanajua tuna shida ila hawakujua ukubwa wa shida zetu na kwa kweli wazo al kuwaambia kwamba sasa tumeamua kufunga kampuni na kila mmoja aangalie ustaarabu mwingine ni wazo ambalo liliumiza sana moyo wangu.
Nilshajaribu kufikiri zaidi kuhusu namna bora ya kuweza kuhakikisha biashara inaendelea kuwepo ila jitihada nyingi zilikuwa hazina matokeo.Ulikuwa ni wakati wa maamuzi magumu.
Nilijianda kwa unyonge na kuelekea Ofisini ambapo nilikuta wafanyakazi wote wameshawasili.NIliitisha kikao cha wafanyakazi wote nikawaweleza hali halisi ya kampuni na kuwaambi sina namna zaidi ya kuachana na biashara niliyokuwa naifanya.Kwa kweli walipata mshtuko hasa ukizingatia kwamba wengi walikuwa ndio ajira yao ya kwanza na pia walishazoe mazingira ya kazi na tulishakuwa kama ndugu pale ofisini.Hivyo baada ya kuwaambia kwamba tunafunga kampuni moja kwa moja walijaribu kutoa maoni mbalimbali lakini mm nilishafanya maamuzi na ulikuwa ni wakati wa kwenda kufanya jambo jingine.
Baada ya kuwaeleza niliwaomba wote waandika barua ya kuomba kuacha kazi na kisha nitawaapa nyaraka zote za muhimu ikiwa cheti cha huduma bora,barua nzuri ya recommendation na msaada wowote ule ambao watahitaji katika kutafuta ajira mpya.
Baada ya kuwaeleza yote na kunielewa niliwapa nafsi ya kuuliza maswali.Mmoja wao aliniuliza swali ambalo lillinishangaza sana.Aliniuliza WHAT ABOUT YOU.Sasa itakuaje kuhusu WEWE?Kwanza sikutarajia swali kama hilo hivyo nilianza kwa kujaribu kudownplay kisha nikawaambia kwa kiingereza.
"I will have to hold the fort,I am a startup creature and I will move to the next Idea and hopeful the money will come" Kabla ya kuanzisha biashara hii nilishaanza biashara nyingine kadhaa na hata baada ya biasharahi nitaanzisha biashara nyingine.Katika ulimwengu wa biashara na hasa biashara zinazoanza kuna changamoto nyingi hata hivyo changamoto kubwa kuliko zote ni kupata wateja hasa wateja wanaoweza kulipa vizuri.
Ndio maana mara nyingi unapoanzisha biashara unashauriwa sana kuzingatio masoko/wateja kawani unapokuwa na uhakika wa soko basi kutengeneza bidhaa au huduma ni jambo rahisi sana.
Je, umewahi kulazimikakufunga biashara yako iwe ndogo au kubwa? Je, ulijisikiaje? Je kufunga biashara kulikufanya uvunjike moyo wa kuanzisha biashar nyingine? Je, uliendelea kuanzisha biashara mpya?Je umeshakutana na biashara ambayo imekutoa kifedha na kimaisha?Karibu tujadili zaidia.
Iwapo una kampuni ambayo ni Dormant au biashara ambayo unataka kuifunga na unahitaji kupata uzoefu wetu na ushauri tafadhali wasiliana nasi kwa email masokotz@yahoo.com