mwita ke mwita
JF-Expert Member
- Aug 13, 2010
- 7,848
- 3,483
Samehe nawe utasamehewa, ucpige pool
Acha kabisa chalie yangu, kuna siku nilikipa ofa kidemu kimoja kikaagiza chips mishikaki 10 ya ng'ombe, 10 ya mbuzi, samaki, kuku na juisi mbili na bado kalisema naomba nauli ya daladala kama change imebakiha ha ha,basi una uzoefu sana aisee
kama nawe ulikuwa unacheat poaMoyo wangu umeruka nikawaza mengine....................!
hapo red hakuna asiye umiaga Kimbeka na hakuna usaliti usioumiza ama unaotia tabasamu usoni,
mm huwa nasema daima siwez kumchukia mtu ila naweza kuchukia kosa la mtu, na huwa naamini mwanadamu ambaye ni sawa na yuko at cross roads ni subject to change at any time so hata kama anabadilika still anaweza kubadilika kuwa mwema ama kuwa mmbaya.
ni kiasi cha kuona kosa kwa jicho la tofauti na nimpaka umeweaza kuteganisha mambo haya mawili yaani uweze kutengenisha makosa na mtu mwenyewe ndipo utakapoona urahisi wa kusamehe
Dah.......ninavyodhani....... kama angekuthamini asingemfunulia mwanaume mwingine.......tena kulala huko huko...... Huyo ni changudoa........
Nashukuru kwa ushauri wenu wana JF wote! Nimeongea na yule mama na binti mwenyewe, nimeamua kumsamehe kwa kosa la kunisaliti, lakini swala la yeye kuendelea na mimi kama wachumba nimemwambia anipe muda, hadi mwezi wa tano nitampa jibu! Japo anaendelea kunitumia sms za kuniomba msamaha na kuomba tuendelee na uchumba wetu kama mwanzo! Ahsanteni wote kwa ushauri wenu!
Nashukuru kwa ushauri wenu wana JF wote! Nimeongea na yule mama na binti mwenyewe, nimeamua kumsamehe kwa kosa la kunisaliti, lakini swala la yeye kuendelea na mimi kama wachumba nimemwambia anipe muda, hadi mwezi wa tano nitampa jibu! Japo anaendelea kunitumia sms za kuniomba msamaha na kuomba tuendelee na uchumba wetu kama mwanzo! Ahsanteni wote kwa ushauri wenu!
i love that sense of humorHahaha mwanaume kazini hata kama una maumivu unajikaza ili hata ukifa the world will know that a single man stood against many and before the sun sets i will mend my broken heart
Wadau, jana niliwaombeni ushauri juu ya binti ambaye alikuwa mchumba wangu, lakini hakuwa mwaminifu, alilala kwa mwanaume mwingine toka ijumaa hadi jumapili na baadae kuja kuomba msamaha!
Leo, nataka kuwapa feedback-kwanza ile jana dada wa binti alijitahidi mpaka akaonana na mimi japo nilijitahidi sana kujenga mazingira ya mimi kuto kukutana na yeye, alipo fika tukaongea kwa kirefu juu ya mdogo wake, na yeye alikiri kwamba mdogo wake hakuwa mwaminifu, lakini wamekwisha mweka chini na wamemsema sana! Nikamwambia nashukuru kwa kulitambua hilo kwani hata mimi nilienda pale hostel bila taarifa kwani nilisha pata hizo habari za yeye kutoka kila ijumaa, hivyo nikamwambia mimi basi tena! Akajitahidi sana kunishawishi nibadili msimamo, lakini nikamgomea!
Leo hii, binti amewahi ofisini kwangu kuliko hata mfagia ofisi, nakuja nimemkuta amekaa nje ananisubiri, alipo niona tu akaanza kulia na kunishika miguu eti nimsamehe, nikamtimulia mbali, akaenda kwa bosi wangu (ni mama) kumwelezea kila kitu, amemwomba eti amsaidie kunisii mimi nimsamehe, eti ni marafiki zake walimdanganya, hata kaa arudie tena! Na ameomba sana hili swala mama yake asijue, eti anapressure anaweza kupata matatizo! Sasa huyu mama amesema niende ofisini kwake saa 8, na anaonekana anataka kunishawishi nisamehe, na mimi sipo tayari kusamehe, wadau ushauri wenu please!
Binti bado yupo hapa around, yupo kama amechanganyikiwa tena sana, kiukweli nimemsaidia sana yeye na familia yake kiuchumi, tangu akiwa kidato cha tano hadi sita, then first year hadi sasa yupo third year!