Mpiga Debe anapoongea Kiingereza: Baada ya kudhalilishwa kuwa hajasoma..

Una sema kweli lakini tuludi nyuma, Daradara ni biashara sidhani kama utapenda ufanye biashara kila siku upate hasara. Kwa ustaarabu wa huyo konda wa kuchukua wanafunzi sita alionyesha utu kabisa, kuliko wale ambao huwa wanawagomea wanafunzi kabisa. Kama utakuwa unafanya biashara utanielewa nina maana gani. Jioni huyo konda atatakiwa apeleke marejesho ili atetee kibarua chake. Lakini kuna watu mjini huwa wanadhani hizo daradara zinatolewa rudhuku na serikali. Akipakia wanafunzi wachache basi na daradara nyingine nayo ije ichukuwe wengine kuliko wote kulundikana kwenye gari moja kama vile imegeuzwa school bus.

Sijasema huyo konda ana makosa wala kuibeza hiyo kazi yake,coz sina hiyo style ya kudharau watu, simdharau ninayemjua na nisiyemjua pia.
ninachosema mimi hapa watanzania kumuona huyo konda eti educated kisa tu ameongea kiingereza, jamani,mpo dunia ya ngapi? kiingereza ni lugha tu kama lugha nyengine.
 
Sishauri watu wajifunze kiingereza/lugha za mataifa yenye nguvu kiuchumi na wala sisemi wasijifunze...somo tunalopata hapa ni kutodharau wengine so far mara nyingi stress za maisha zinapeloekea mtu kufikia asipotaka kufika in actual sense! Tanmo kitufe cha thanks sikioni ningekugongea kwa kutushirikisha somo la maisha!
 
Na mbaya zaidi wasio jua ki2 hujifanya ndio wajuaji zaizi na wajuwaji hawawi na wenge ...
lakini imeandikwa ajikwezae atashushwa na ajishushae atakwezwa. asema Bwn.
NB:_sio ndoto lakini hahahahaahaaa!!...
 
Sijasema huyo konda ana makosa wala kuibeza hiyo kazi yake,coz sina hiyo style ya kudharau watu, simdharau ninayemjua na nisiyemjua pia.
ninachosema mimi hapa watanzania kumuona huyo konda eti educated kisa tu ameongea kiingereza, jamani,mpo dunia ya ngapi? kiingereza ni lugha tu kama lugha nyengine.
Ndo maana kule bungeni wanaikoroga ehh?Bongo watu hawaongei kingereza mitaani useme kwamba kajifunza tu...mpe konda wa watu credit!Amejifunza/isoma ndo maana anajua!
 
Kuna siku nilikua naongea na muosha magari mmoja akaniambia kitu kilichonishangaza sana. Yeye kwa siku anaweza kuosha kati ya gari 15 na siku nzuri hadi gari 20 au 25 kwa sh. 2000 kila moja. Kupiga mahesabu nikagundua huyu jamaa kwa siku anaingiza kati ya 40,000 - 50,000! Hata ukitoa garama zote bado income yake ni kubwa kuliko baadhi yetu tunaosubiri tarehe 60, ukizingatia yeye hana PAYE wala nini. Wengi wa makondakta na madereva, mafundi gereji tunawadharau lakini kimapato wametuacha mbali. Kwanza wengi wana magari yao ya kutembelea, wengine wanamiliki daladala, teksi, nyumba n.k. Usimdharau mtu!
 
Mijitu mingine bana.........kwa kujipa matumaini ya kiajabu ajabu......kufanikiwa au kutofanikiwa kimaisha ni jambo moja na kuongea lugha iwe kifaransa/kiingereza/kispanish etc etc ni jambo jingine...........mwanangu aliyeko junior high school anaogea vizuri kiingereza + kispanish na sasa yuko mid-level kwenye kifaransa...........i mean...whats a big deal na lugha ya kiingereza............assume yule abiria naye angeongea kiingereza ......then what!!!

Namkumbuka rafiki yangu January.........na msemo wake........ni sawa kabisa kwa million flies kufurahia/kung'ang'ania kidonda...........

Yaani tunawafundisha nini wale wanafunzi/watoto wetu.......yaani ukijua kiingereza wewe ndio umeula?....maskini hata wanafunzi wale wakasahau kuwa wanatakiwa kuwahi shule.......na kuanza kumshangilia konda........hivi tunajenga jamii gani wandugu.......

Hivi nyie baadhi yenu hapa JF mnaomshangilia yule konda......mnaona ni sahihi wanafunzi kugombania basi na kuning'inia...........sitashangaa kuambiwa/kusikia nyie (mnaomtetea konda hapa JF) ndio mnaoshangilia yale mabasi yanayoenda speed za ajabu safari za mikoani......kisa kuwahi biashara ili kutimiza lengo la tajiri...........

Notwithstanding jamaa (mpiga debe) ana responsibility ya kutimiza malengo kwa tajiri yake.......however, twende mbele turudi nyuma.....wanafunzi wanatakiwa waende shule........na sio kwenda tu.......inabidi wawahi.......

Yule abiria aliamua kuwatetea wanafunzi ili wapande basi/daladala waweze kuwahi shule..........poor him......"slave mentalities" wakamgeuzia kibao......kisa eti konda anaongea kiingereza.....damn!....halafu mijitu mingine humu JF inashangilia!!!!!

Huyo konda has a lot to be desired...........i.e. alifukuzwa kazi.........ana frustrations zake.............na inaelekea wengi wenu mnaomshangilia huyo konda mnahitaji break na kuangalia hiki kipande cha Robert (Bob) Marley

http://www.youtube.com/watch?v=QrY9eHkXTa4&feature=related
 
Kuna somo hapo la kutokumdharau mtu kwa muonekano wake..

Don't judge a book by its cover.

ulikuwa wewe nini? Teh teh pole.
Me nimeachwa hoi na jinsi wanafunzi waliokuwa wanatetewa walivyomgeuka jamaaa

Tusidanganyane. Wala tusijidanganye wenyewe. Kiingereza pekee si usomi. Hivi niulize swali, ni kitu gani ambacho humfanya binadamu a-judge the book by its cover? Ina-sound vizuri mtu akisema "Don't judge the book by its cover" kwa sababu watu wana-assume yuko humble ((again wanajudge the book by its cover" )(Paradox)!) Dunia na watu huwa na natural trend ya mambo. Mfano maji kwa kawaida hutiririka kuelekea sehemu iliyo chini ki-mwinuko, Watu waliosoma huwa na maendeleo zaidi ya waliosoma (generally), watu wa mjini huwa wamechangamka kuliko watu wa vijijini. Hata hivyo nakubali exceptions huwa zipo ila ni rare sana that is why judging the book by its cover itaendelea ku-exist hata kwa wale wanoonekana kuwa wanaiponda.

Nachozungumza hapa ni kuwa hakuna mtu, narudia, hakuna mtu awe jakaya, Dr Slaa, Papa Benedict XVI, Osama na wewe ambaye ha-judge kwa mazoea. Wanaoweza kuwa exceptional ni watoto wadogo sana (sana) kwa umri ambao hawana experience yoyote ambao wako tayari kutafuna wembe na kushika moto kwa kuwa hawajui wala kukumbuka moto unaunguza na wembe unakata.

Kwa thread hii, kujua kiingereza inaweza isiwe sababu, suala tu ni kuwa konda amepata "sympathy" na hasira za watu dhidi ya judgements zinazowaudhi, lakini konda hajaonesha usomi wowote (hajaonesha kutokuwa msomi pia) ambao ungestahili "kushabikiwa" kiwango hiki. NI kawaida yetu kuongea mambo yanayopendeza lakini tunaziachia saikolojia zetu ziamue zenyewe. Kuna wadada na wakaka humu wanafurahia maneno ya "Don't judge the book by its cover" sasa nenda umevaa vibaya uone kama utapata consideration. Nenda kajaribu.........

Hata hivyo ni vizuri tuangalie kauli zetu.
 
We Ogah kwani wanafunzi kuwahi shule ni jukumu la konda?Huyo abiria aliyekua anawatetea kama aliwapenda sana angewalipia nauli ya mtu mzima ili wote wapate sawa yao...konda afikishe mahesabu na watoto wawahi shule!Nashangaa unapomgeuzia huyo konda kibao utadhani yeye daladala ni yake!Ile ni kazi kama unayofanya wewe na lazima akamilishe alichotumwa na bosi ili na yeye watoto wake waende shule.Kama unataka kumkasirikia mtu kwa hali iliyopo nenda wizara ya elimu au kwenye ofisi ya mkuu wa magamba!
 
We Ogah kwani wanafunzi kuwahi shule ni jukumu la konda?Huyo abiria aliyekua anawatetea kama aliwapenda sana angewalipia nauli ya mtu mzima ili wote wapate sawa yao...konda afikishe mahesabu na watoto wawahi shule!Nashangaa unapomgeuzia huyo konda kibao utadhani yeye daladala ni yake!Ile ni kazi kama unayofanya wewe na lazima akamilishe alichotumwa na bosi ili na yeye watoto wake waende shule.Kama unataka kumkasirikia mtu kwa hali iliyopo nenda wizara ya elimu au kwenye ofisi ya mkuu wa magamba!

Lizzy mambo hayaendi hivyo. Kama huna uchungu na wenzako hilo ni suala lako mwenyewe. Kutetea wanafunzi haimaanishi ni lazima uwalipie nauli. Wapo makonda ukiwaambia watu wameshajaa kwny daladala wanakwambia ungepanda Taxi, sidhani hivi ndivyo mambo yanavyotakiwa kwenda. Ni kweli konda ana haki yake na wanafunzi wengi huwa wasumbufu lakini ni lazima mambo yaende kwa utaratibu, kama tajiri wa konda ni mkorofi hili si tatizo la abiria mtetezi.

Sidhani pia kama ni sawa kumsema Ogah aende ofisi ya Mzee wa Kaya, kwa sababu unajua hili ni jambo lisilotekelezeka. Ah, haya bwana.
 
3D yeye anapodai konda angewapandisha wanafunzi wote wakati wakuwakilisha mahesabu nani atakua pale kumweleza tajiri kwanini mahesabu hayajakamilika??Hapo unatakiwa umfikirie konda!Kuhusu kuwafikiria wanafunzi..kuna utaratibu na ndio maana alipakiza 6 akataka waliobaki wapande daladala nyingine.Nyie mnataka kusema tu wanafunzi wapandishwe bila kufikiria matokeo yake yatakuaje kwa konda!Mimi nataka konda aendelee kua na kazi na wanafunzi waende shule kwa utaratibu walioweka wenye magari yao.
 
3D yeye anapodai konda angewapandisha wanafunzi wote wakati wakuwakilisha mahesabu nani atakua pale kumweleza tajiri kwanini mahesabu hayajakamilika??Hapo unatakiwa umfikirie konda!Kuhusu kuwafikiria wanafunzi..kuna utaratibu na ndio maana alipakiza 6 akataka waliobaki wapande daladala nyingine.Nyie mnataka kusema tu wanafunzi wapandishwe bila kufikiria matokeo yake yatakuaje kwa konda!Mimi nataka konda aendelee kua na kazi na wanafunzi waende shule kwa utaratibu walioweka wenye magari yao.

Kwa lugha hii sasa nakuelewa, maana ukiniambia niende kwa Mkuu wa Magamba, virungu ntavikwepaje? Otherwise, naunga mkono hoja yako ya idadi, nilikuwa nafahamu wanne kwa kipanya na sita (wanafunzi fulani waliniambia 10) kwa Coaster/DCMs. Wanafunzi wengine wakorofi sana, juzi kati hapa ilibidi nijiunge na jeshi la konda kumshusha mwanafunzi mkorofi, not physically lakini.
 
Serikali ya Tz bwana huku ng'ambo kuanzia mtu wa miaka 4 analipa nauli complete,awe mwanafunzi/askari wote bei moja hakuna cha nauli nusu wala bure.hakuna mambo hayo.
 
Kwa lugha hii sasa nakuelewa, maana ukiniambia niende kwa Mkuu wa Magamba, virungu ntavikwepaje? Otherwise, naunga mkono hoja yako ya idadi, nilikuwa nafahamu wanne kwa kipanya na sita (wanafunzi fulani waliniambia 10) kwa Coaster/DCMs. Wanafunzi wengine wakorofi sana, juzi kati hapa ilibidi nijiunge na jeshi la konda kumshusha mwanafunzi mkorofi, not physically lakini.

Hehehe unamwogopa rais wako?We ndo umemwajiri ujue..yani ye ndo konda na wewe mmiliki!
 
Serikali ya Tz bwana huku ng'ambo kuanzia mtu wa miaka 4 analipa nauli complete,awe mwanafunzi/askari wote bei moja hakuna cha nauli nusu wala bure.hakuna mambo hayo.
Hiyo system ni nzuri kwasababu inampa kila mtu nafasi ya kukwea chombo cha usafiri bila kukabana mashati maana ukilipa nauli nzima unakua na haki "nzima".
 
Tatizo la Watz ni kushindwa kutofautisha mambo , sasa kwa konda kuongea kiingereza amegeuka msomi kwa hiyo hata mtoto wangu wa 5 yrs anazungumza kiingereza basi naye ataitwa msomi , kuna watu wengi wasomi Wazuri tu lakini kiingereza mgogoro , anakiandika vizuri lakini si kuongea
 
Hehehe unamwogopa rais wako?We ndo umemwajiri ujue..yani ye ndo konda na wewe mmiliki!

Lizzy hili suala la kumwajiri Rais linakuwa sahihi kwa fikra za ki-Nyerere tu. Hivi vizazi vya akina Gbagbo na Wazee wa Magamba huwezi kuviajiri, vinajiajirisha vyenyewe. Ukitaka kuuliza iweje wakupuuze wewe mwajiri watajibu, "Kutokana na taarifa za kiintelijensia..........." au kama anavyosema Mjomba Mpoto, "Ririkuwa rinapambana na porisi tukarishinda."
 
Hadithi imekaa kama ya kutunga ili ku make a point kwamba tusidharau wenzetu na kazi zao. Lakini, ni dhahiri, hadithi ni ya kutunga.
 
We Ogah kwani wanafunzi kuwahi shule ni jukumu la konda?Huyo abiria aliyekua anawatetea kama aliwapenda sana angewalipia nauli ya mtu mzima ili wote wapate sawa yao...konda afikishe mahesabu na watoto wawahi shule!Nashangaa unapomgeuzia huyo konda kibao utadhani yeye daladala ni yake!Ile ni kazi kama unayofanya wewe na lazima akamilishe alichotumwa na bosi ili na yeye watoto wake waende shule.Kama unataka kumkasirikia mtu kwa hali iliyopo nenda wizara ya elimu au kwenye ofisi ya mkuu wa magamba!

kwa hiyo hiyo ndio iliyokufanya umshangilie (eti apewe credit) konda kuongea kiingereza?............Pure bongo style of thinking.........
 
sijasema huyo konda ana makosa wala kuibeza hiyo kazi yake,coz sina hiyo style ya kudharau watu, simdharau ninayemjua na nisiyemjua pia.
Ninachosema mimi hapa watanzania kumuona huyo konda eti educated kisa tu ameongea kiingereza, jamani,mpo dunia ya ngapi? Kiingereza ni lugha tu kama lugha nyengine.

mi naona watu walimshabikia kwakua watz wengi either hatujui au hatujiamini kuongea kingereza. Si kila anayezungumza kingereza ni msomi. Hapa home tuna mtoto wa 3 years anaongea fluent kingereza ila hajui hata kuandika jina lake,
konda aliwaimpress watu ndani ya daladala maana hawakutegemea kama nae anaweza kuongea kimombo.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
hadithi imekaa kama ya kutunga ili ku make a point kwamba tusidharau wenzetu na kazi zao. Lakini, ni dhahiri, hadithi ni ya kutunga.

inawezekana ni kweli kabisa.ila kikubwa ni kuwa usimdharau mtu hata kama umem rate very low kwenye scale yako.
 
Back
Top Bottom