lukindo
JF-Expert Member
- Mar 20, 2010
- 8,466
- 9,028
hapo kwenye red mkuu wajuzi wa mambo wameanza kuhoji na hasa huku Afrika juu ya ELIMU na VYETI. Wengi walidhani haya maswali yangeishia kwenye level za certificates lakini ni bahati mbaya sasa inaenda mpaka level ya PhD na Profs kielelezo kuwa rushwa ina nguvu ya kutisha hapa kwetu kuzidi elimu zote. Angalia wote wanaoharibu, hakuna hata mmoja darasa la saba! Ndio maana wakenya walishikilia mzee Kivuitu ajihudhuru baada ya kuvuruga uchaguzi nza si hivyo tu bali degree yake ya UDSM ifutwe.Sijui hawa watu wanawaza kwa kutumia akili gani, na cha kushangaza eti mkuruguenzi ni Profesa!!!
Wanaposema kwamba wanaanzisha utaratibu wa mtu kuweza kuhama na namba yake ya simu kutoka kampuni moja kwenda nyingine, nadhani ni upuuzi wa mwaka...
Yaani mathalani mtu ana namba 0754096210 ya voda, alafu anaamua kuhamia airtel, akitumia namba hiyo hiyo... Hawa watu wamesahau kwamba Gharama za kupiga simu ndani ya mtandao mmoja ni tofauti na gharama za kupiga simu kutoka mtandao mmoja kwenda mwingine?!. Kwa hiyo mi ambaye nilijua ndugu au rafiki yangu yupo voda, siku nikitaka kumpigia natumia line yangu ya voda ili kubana matumizi, kumbe mtu huyo alishahamia airtel na namba hiyo hiyo, so inakula kwangu!!!
Au TCRA wamejisahau kwa kuwa wao wana mihela na hawaangalii wanatumia line gani kupiga mtandao gani? Au wamesahau majority ya watanzania siku hizi wana line zaidi ya moja ili kubana matumizi?
Mi nadhani wawe wabunifu wa kweli, sio kukopi na kupesti tu kila wanachosikia huko nje...
Hata mimi nilimsikia akiongea na sikuelewa alichokuwa akimaanisha na nikadhani labda nilikuwa pekee