Mnyika, Zitto, Januari, Kafulila, Nape kuanzisha Jukwaa la viongozi vijana?

Hongereni sana cdm kwa kujikomba sana kwa ccm. Slaa asalimiana na kikweta, lema wafanya sherehe na mkuu wa mkoa, shibuda ahudhuria kuapishwa jk, mbowe atumia busara kukubaliana na ccm kuhusu wakuu wa wilaya, leo hii mnyika zito mnatafuta nini kwa nape. Safi sana mrema alianza kidogokidogo ,maalimu sefu kidogokidogo, kama ukombozi unakuja kwa urafiki safi sana. Hamjifunzi toka kwa mandera endeleeni kuunga mkono ujinga
 
nape?
uungane na nape ili iwe nini?
huyu ni mtetezi wa mafisadi na ufisadi,ni jasiri wa kifisaadi hajawahi kushinda kwa anayoyasimamia.

nape akikuambia hii ni rangi nyekundu ukitulia na kuichunguza vizuri unakuta ni njano.
sijui ni hana msimamo au hajijui?


wewe umeacha kumuona January kuwa ni kibaraka wa mafisadi unamsema Nape anayewindwa na mafisadi kwa hali na mali au una chuki binfsi au na wewe unafaidika na huu mfumo wa kifisadi na mafisadi wake huku ukijitia ni CDM
 
... Mhe Mnyika, ondoka hapo kwenye kundi hilo haraka kwa kuwa hadhi yako hailingani nalo hata kidogo. Take special NOTE now!!
 
..nadhani ni mbinu ya CCM kudhoofisha upinzani.

..vijana toka vyama vya upinzani lazima wakati wote wajitofautishe na wale walioko CCM.
 
Alhamisi Kwenye saa saba na robo pale Southern Sun, Iliypkuwa Holiday inn karibu na Ocean Road Zitto alikuwa na Mwamvita Makamba Zainabu Kawawa,na mwanaume mwingine sikuona sura yake labda ndio huo mtandao
 
HEBU WEWE mnyika achana na mambo ya kunusana nusana na hawa jamaa hawaaaminiki hta kidogo wasipokuibia wanakuwekea sumu wasipokuwekea sumu wanakutafutia kashfa wasipokutafutia kashfa wanakuuwa CCM sio watu jukwaa la vijana nini hawajui nini kuhusu vijana achana kupoteza muda wako wa kupangia mikakati ya mabadiliko ukaenda kusahaulishwa huko kuwa ni jukwaa
 
Umoja ni nguvu, utengano udhaifu. I recomend and support anytype of union in taking Tanzania to the next level..
 
Wadau nimeinasa mahali kuwa kuna mazungumzo yanaendelea baina ya baadhi ya Viongozi vijana kuacha tofauti zao za kiitikadi (Kivyama) na kuanzisha jukwaa la Viongozi vijana kwa lengo la kujadili mstakabari wa Tanzania sasa na baadae kiuchumi, kisiasa, kimichezo na kiutamaduni.
Kama mjadala na mazungumzo haya yapo, naomba kuyaunga mkono, kwani ndiyo yatakayofanikisha kuleta tija kwa mstakabari wa taifa hili. Sasa hivi kinacholitesa taifa hili ni tatizo la mvutano wa kiitikadi na kivyama badala ya mvutano wa kimtazamo wenye lengo la kusukuma maendeleo ya taifa hili mbele kwa haraka.
Hivi Kafulila ni Kiongozi??! Anamwongoza nani???
 
Alhamisi Kwenye saa saba na robo pale Southern Sun, Iliypkuwa Holiday inn karibu na Ocean Road Zitto alikuwa na Mwamvita Makamba Zainabu Kawawa,na mwanaume mwingine sikuona sura yake labda ndio huo mtandao
Sidhani, mi nahisi kuna mmoja hapo analikuwa anamkopa mwenzake
 
Hivi nape naye ni wakuitwa kiongozi? au ndio kiongozi asiye na meno ? mbona mtatiro hayupo kwenye hiyo list? kama Nape ni kiongozi wa chama chake tu na si Taifa
 
Back
Top Bottom