Mabaki ya mabomu 2 yalipuka na kuua watoto wawili walio kuwa wakicheza kwenye migomba na kuwaacha 4 wakiwa wamejeruhiwa vibaya.
More news stay tuned.
Mabaki ya mabomu 2 yalipuka na kuua watoto wawili walio kuwa wakicheza kwenye migomba na kuwaacha 4 wakiwa wamejeruhiwa vibaya.
More news stay tuned.
Jamani hivi hii serikali yetu inatupeleka wapi? We Mrisho una tupeleka wapi watanzania wako? Yao wapi maisha bora kw akila mtanzania? mbona tunashuhudia vifo vya kizembe namna hii nawe umekaa kimya tu? Au kwa vile Ikulu haiko Mbagala? Kumbuka wananchi hao hao wa Mbagala ndio walokupa wewe kura za kukuwezesha kula.
Uliruhusuje wananchi wa Mbagala kuruhusiwa kurudi majumbani mwao (Mbagala) tena na fidia zikatolewa wakati wewe na serikali yako hamkuwa na uhakika kuwa mahali pale ni salama? Hebu jeshi liwajibike katika vifo hivi ni aje wawe hawakumaliza mabomu yote? Hivi ni lini tutafikia mahali pa kuwawajibisha wewe na serikali yako kwa uzembe huu wa serikali yako?
Nasikitika sana kuwa hamu na uaminifu wangu kwako na serikali yako imefikia tamati sina uhakika kama mwakani nitakupa kura yangu tena.
Aksante.
Poleni wafiwa na majeruhi MUNGU awape nafuu