Uzima Tele
JF-Expert Member
- Jan 20, 2023
- 1,103
- 2,352
Nimefuatilia kwenye Online TVs za YouTube mikutano ya CHADEMA leo J'tano ya kuimarisha chama chao waliyoipa jina la Operesheni +255 - Katiba mpya na Okoa bandari zetu..
Leo Freeman Mbowe, Mwenyekiti Taifa (CHADEMA) amehitimishia mikutano yake mji mdogo wa Nyehunge Jimbo la Buchosa Wilaya ya Sengerema. Makamu Mwenyekiti- CHADEMA Taifa, ndugu Tundu Lissu yeye kahitimishia mikutano yake jioni hii mjini Chato, Jimbo la Chato Wilaya ya Chato Kwa hayati Rais John P. Magufuli
Kilichonifanya niposti uzi huu ni kuelezea kwa ufupi juu ya ujumbe unaotumwa kwa viongozi wa serikali hii ovu chini ya CCM na umati wa watu/wananchi wanaojitokeza kwenda kuwasikiliza viongozi wa CHADEMA..
1. MOSI, watu hawa wanakuja wenyewe kwa hiari yao kwenye mikutano hii. Hili ni moja na la muhimu sana kuliko yote..
2. MBILI, tofauti na mikutano ya viongozi wa CCM ambayo huwa na misururu mirefu ya magari ya umma, wasanii waimbaji, fedha na sound systems za kufa mtu, CHADEMA ni kinyume chake kabisa. Ukiondoa msafara wa FM ambaye anatumia helkopita, Tundu Lissu yenye msafara wake hauzidi gari nne au tano, na maeneo mengine hata sound systems ni duni sana lakini wananchi hawajali kabisa hayo. Wao wanachotaka ni kusikia CHADEMA wana ujumbe gani wa matumaini ya kesho yao kwao..
3. TATU, ukiwatazama wananchi hawa wanapokuwa kwenye mikutano hii, wanakuwa watulivu sana wakisikiliza kwa makini hatua kwa hatua kinachosemwa na viongozi. Hili ni la muhimu zaidi kuliko yote maana umakini wa mtu katika kusikiliza huleta uelewa na ufahamu ndani yake. Na mtu akielewa, anakuwa amekomboka huyo..!!
4. NNE, Ujumbe ninaoupata mimi kupitia mikutano hii ni huu...
Kwamba, lipo jambo linatokota na linaweza kulipuka wakati wowote. Pia kuna kila dalili kuwa wananchi tumechochwa na namna CCM wanavyoindesha nchi hii na watu wako tayari kufanya lolote kwa njia yoyote kufanya mabadiliko ili mradi waambiwe nini cha kufanya nje kabisa ya utaratibu wa sanduku la kura kwa mtindo na mfumo wa chaguzi za sasa..
5. TANO na mwisho, nafurahishwa sana na uwezo na ufundi wa Freeman Mbowe na Tundu Lissu wa kujenga hoja na kuwasilisha ujumbe wao kwa watu..
Kwa kweli kwa hili, kiboko yao ni Tundu Lissu. Huyu jamaa ni maridadi sana ktk kuelezea jambo gumu kwa hadhira (audience) yoyote kwa lugha rahisi na ya kueleweka kwa kila mtu hata kwa wanakijiji..
Mfano leo kule Chato na jana kule Mbogwe, alieleza kwa ufasaha usiomithilika uhusiano wa mfumo mbovu wa kisheria na kiutawala (kikatiba) na matatizo ya ukosefu wa huduma bora za kijamii kama maji, elimu, barabara nk pamoja ubovu wa mikataba mbalimbali ambayo CCM inaingia na wageni ukiwemo wa bandari unaowapa waarabu wa Dubai bandari zetu zote kupitia kampuni yao ya DP World..
Baada ya hapo akahusianisha na umuhimu wa kuandika katiba mpya bora yenye CHECKS & BALANCES OF POWERS kwa taasisi zetu za kiserikali yaani executive, parliament & judiciary..
Alipomaliza kufundisha somo hilo, na ukiangalia sura na nyuso za wananchi waliokuwa wanasikiliza, unaona wazi na bila shaka kuwa, wananchi walielewa vyema somo lile..
People are already pushed on the walls. Bila shaka maombi yetu tukiongozwa na mtumishi wa Bwana Yesu Kristo, Mch. Mbarikiwa Mwakipesile yamesikika na kumfikia Mungu kwenye kiti chake cha enzi. Amina🙏🙏🙏🙏
Leo Freeman Mbowe, Mwenyekiti Taifa (CHADEMA) amehitimishia mikutano yake mji mdogo wa Nyehunge Jimbo la Buchosa Wilaya ya Sengerema. Makamu Mwenyekiti- CHADEMA Taifa, ndugu Tundu Lissu yeye kahitimishia mikutano yake jioni hii mjini Chato, Jimbo la Chato Wilaya ya Chato Kwa hayati Rais John P. Magufuli
Kilichonifanya niposti uzi huu ni kuelezea kwa ufupi juu ya ujumbe unaotumwa kwa viongozi wa serikali hii ovu chini ya CCM na umati wa watu/wananchi wanaojitokeza kwenda kuwasikiliza viongozi wa CHADEMA..
1. MOSI, watu hawa wanakuja wenyewe kwa hiari yao kwenye mikutano hii. Hili ni moja na la muhimu sana kuliko yote..
2. MBILI, tofauti na mikutano ya viongozi wa CCM ambayo huwa na misururu mirefu ya magari ya umma, wasanii waimbaji, fedha na sound systems za kufa mtu, CHADEMA ni kinyume chake kabisa. Ukiondoa msafara wa FM ambaye anatumia helkopita, Tundu Lissu yenye msafara wake hauzidi gari nne au tano, na maeneo mengine hata sound systems ni duni sana lakini wananchi hawajali kabisa hayo. Wao wanachotaka ni kusikia CHADEMA wana ujumbe gani wa matumaini ya kesho yao kwao..
3. TATU, ukiwatazama wananchi hawa wanapokuwa kwenye mikutano hii, wanakuwa watulivu sana wakisikiliza kwa makini hatua kwa hatua kinachosemwa na viongozi. Hili ni la muhimu zaidi kuliko yote maana umakini wa mtu katika kusikiliza huleta uelewa na ufahamu ndani yake. Na mtu akielewa, anakuwa amekomboka huyo..!!
4. NNE, Ujumbe ninaoupata mimi kupitia mikutano hii ni huu...
Kwamba, lipo jambo linatokota na linaweza kulipuka wakati wowote. Pia kuna kila dalili kuwa wananchi tumechochwa na namna CCM wanavyoindesha nchi hii na watu wako tayari kufanya lolote kwa njia yoyote kufanya mabadiliko ili mradi waambiwe nini cha kufanya nje kabisa ya utaratibu wa sanduku la kura kwa mtindo na mfumo wa chaguzi za sasa..
5. TANO na mwisho, nafurahishwa sana na uwezo na ufundi wa Freeman Mbowe na Tundu Lissu wa kujenga hoja na kuwasilisha ujumbe wao kwa watu..
Kwa kweli kwa hili, kiboko yao ni Tundu Lissu. Huyu jamaa ni maridadi sana ktk kuelezea jambo gumu kwa hadhira (audience) yoyote kwa lugha rahisi na ya kueleweka kwa kila mtu hata kwa wanakijiji..
Mfano leo kule Chato na jana kule Mbogwe, alieleza kwa ufasaha usiomithilika uhusiano wa mfumo mbovu wa kisheria na kiutawala (kikatiba) na matatizo ya ukosefu wa huduma bora za kijamii kama maji, elimu, barabara nk pamoja ubovu wa mikataba mbalimbali ambayo CCM inaingia na wageni ukiwemo wa bandari unaowapa waarabu wa Dubai bandari zetu zote kupitia kampuni yao ya DP World..
Baada ya hapo akahusianisha na umuhimu wa kuandika katiba mpya bora yenye CHECKS & BALANCES OF POWERS kwa taasisi zetu za kiserikali yaani executive, parliament & judiciary..
Alipomaliza kufundisha somo hilo, na ukiangalia sura na nyuso za wananchi waliokuwa wanasikiliza, unaona wazi na bila shaka kuwa, wananchi walielewa vyema somo lile..
People are already pushed on the walls. Bila shaka maombi yetu tukiongozwa na mtumishi wa Bwana Yesu Kristo, Mch. Mbarikiwa Mwakipesile yamesikika na kumfikia Mungu kwenye kiti chake cha enzi. Amina🙏🙏🙏🙏