Kaizer
Platinum Member
- Sep 16, 2008
- 25,320
- 17,823
mimi kuna mzee aliniambia all women are sycopath.....
dawa ni wewe mwanaume kudharau tu.
akikuudhi sana ongeza mke...
ewaaaa
mimi kuna mzee aliniambia all women are sycopath.....
dawa ni wewe mwanaume kudharau tu.
akikuudhi sana ongeza mke...
yan hiyo si suluhu ni kujiongezea matatizo tu
Rafiki wangu wa karibu sana amenieleza tatizo lake nikaona si vyema kulileta hapa kwa wahenga kwani palipo na wengi hapaharibiki jambo.
Anasema ameona na mkewe ndoa ya Kikristo miaka 10 iliyopita na kipindi chote cha uchumba aliamua kuto onja chochote hadi ile siku ya ndoa yao ili heshima, uaminifu na adabu iwepo. Baada ya kuona kila mmoja alimweleza mwenzake tabia ambazo hazipendi kama kufokeana hadharani, kupigana n.k. na wakakubaliana kwamba kila mmoja atajitahidi asimwudhi mwenziwe. Miaka 5 ya ndoa ilikuwa mizuri na waliishi kwa kuzingatia misingi waliyoiweka. Baada ya miaka mitano mkewe akaanza zile tabia ambazo ni kero kwa mumewe huku mume akimkumbusha kuwa anakiuka maagano lakini mkewe anaziacha wiki then anarudia tena.
Mbaya zaidi kuna kipindi mume alisafiri na katika kumpigia mkewe simu kumtakia hali na kumweleza habari za safari mkewe akashindwa kuwa seriuos kuhusu ule ujumbe kwani inaonyesha alikuwa ametingwa labda na TV au na kitu kingine. Hii hali ikawa imemuudhi mumewe na wakawa wanajibizana ki ugomvi ugomvi na hata aliporudi akawa amerudi na uso wa chuki.
Ilipofika usiku kitandani kana kwamba haelewi kilichomuudhi mumewe mkewe akaamuuliza mbona huongei na mimi kwa furaha? nini kimekuudhi?
Maswali haya yalimuudhi sana yule mume kwani hakujua mkewe haelewi nini wakati wamegombana jana kwenye simu na hawajasuluhisha.
Naomba mawazo yenu wana JF je mwanamke kama huyu utamwelewaje? amekupuuza? ameku ignore? au ana matatizo gani?. Na nini cha kumfanya ili awe na approach sahihi?
Hii ndio maana huyu rafiki yangu amesema hamuelewi mkewe hata baada ya kuwa kwenye ndoa kwa miaka 10 sasa. Naomba msaada wenu,
Pole sana ndugu yangu kwa maswaiba yanayo kukuta
Ndoa kama taasisi ina changamoto nyingi sana, jipo moyo, na jitahidi kutafuta chanzo cha mfarakano, tatua tatizo kisha maisha yatasonga.
Kwa mfano, kuna wanandoa walipata kuwa na mfarakano uliotishia ndoa yao kuvunjika, kwani mwanamke alikuwa ni kiguu na njia nyumbani hatulii, mara atakwambia nakwenda kusuka nyele za kimasai, hiyo inamchukua jumamosi na jumapili kuanzia asubuhi mpaka jioni, mara anaaga kwenda kwenye 'kitchen party' mara kwa shoga yake mtaa wa pili kunashuguli...... mume na mke kila siku ugomvi... na mara nyingi mke akitoka kwenye matembezi anakuwa amechoka na ikawa mara nyingi anageukia upande wa pili wa kitanda au anaangalia tamthilia kuvizia mume alale asiumbe tunda.
Huyu bwana uvumilivu ukamshinda, akatafuta ushauri kwa rafiki yake wa karibu, kabla ajachukua maamizi ya kuachana na mkwe, baada ya maongezi marefu, rafiki wa yule jamaa akamguzia kibao rafiki yake na kumueleza kuwa yeye ndio mwenye matatizo, alimpa ushauri kuwa siku amboyo mkewe atamuaga anataka kwenda matembezi ajitahidi kumpa mkewe mahaba ya kikweli kweli, [kwa kifupi jamaa alipewa desa ya jinsi ya kumtosheleza mkewe kimahaba]
Siku ya siku ikafika, ijumaa jioni wakekaa sebuleni, mke akamtaarifu mume kuwa anampango wa kwenda saloon kusuka nywele, jamaa alifurahi, na kuahidi kumuachia ufunguao wa gari na kisha jamaa akavuta wallet na kumkabidhi wekundu wa msimbazi watano, mke akaduwaa, wakiwa kitandani jamaa akakumbukia desa lake na taratibu akaanza kupractice, ndani ya saa 1 mke alikuwa hoi kwa mahaba aliyopewa.
Jumamosi ikafika, jamaa akaaga subuhi, akaondoka na kumuacha mkewe akiwa bado nyumbani, ilipofika mida ya mchana, mume akampigia simu mkewe kutaka kujua anaendeleaje na ususi, mke alisema bado yuko nyumbani anafanya usafi, jamaa aliporudi nyumbani jioni anakuta mkewe hajatoka yuko busy na shughuli za nyumbani, na maandalizi ya chakula cha familia, safari ya salooni ikafa.
Mume akaendelea kutumia shule aliyopewa, kwa uadilifu, kadri siku zilizidi kwenda mke akarudisha heshama na safari za mara kwa mara zikakoma.
Kwa kiasi kikubwa ufanisi mdogo wa mume mara nyingi ndio inakuwa chanzo kikubwa cha migogoro ndani ya nyumba
mwambia jamaa ani pm anipe story kikamilifu tuweze kusaidiana
Mpe pole huyo rafikiyo,inaelekea bado hajajua jinsi ya kuishi na mkewe.
Jana nilikuwa nasikiliza radio sijui ni ipi ila walikuwa wanaongelea maisha ya mume na mke ndani ya ndoa
yule mchungaji alikuwa akielekeza yale maongezi haswa kwa wanaume
na kuwaambia kuwa,ninanukuu "mke wako ni mtoto wako, yakupasa umlee, umsikilize, umdekeze, umliwaze
ingawaje huyo mtoto atakuwa anakuudhi, anafanya mambo ya ajabu ajabu lakini ye anaona kawaida, atakuwa haelewi unachosema ingawa ye anaona anaelewa..hivyo basi wewe mwanaume unapoishi na huyo mkeo yani mtoto wako,yakupasa umtreat kama mtoto wako wa kumzaa na umchukulie kama mtoto..si mnayajua maudhi ya watoto lakini?".mwisho wa kunukuu
Basi nikirudi kwenye mada, na kwa huyo rafiki yako hapaswi kununa.we wamnunia mtoto ye anakuona we ndo wa ajabu tena anakuona chizi
anapaswa akae nae chini amueleze kinachomkera kwani akikuna mwenzake hatajua kinachomsibu.
Wamezaa watoto wangapi? Je mke wake ameongeza kipato zaidi kabla ya hiyo miaka 10 ya ndoa? Alishawahi kumfumania mumewe kisha jamaa akaomba radhi? Amfuatilie kwa umakini ili ajue source ya kiburi chake. Wanawake wengi japo si wote hujikita katika kutafuta ndoa lakini wakizipata husahau juhudi kubwa waliyotumia katika kujishape ili waonekane wake bora.
Rafiki wangu wa karibu sana amenieleza tatizo lake nikaona si vyema kulileta hapa kwa wahenga kwani palipo na wengi hapaharibiki jambo.
Anasema ameona na mkewe ndoa ya Kikristo miaka 10 iliyopita na kipindi chote cha uchumba aliamua kuto onja chochote hadi ile siku ya ndoa yao ili heshima, uaminifu na adabu iwepo. Baada ya kuona kila mmoja alimweleza mwenzake tabia ambazo hazipendi kama kufokeana hadharani, kupigana n.k. na wakakubaliana kwamba kila mmoja atajitahidi asimwudhi mwenziwe. Miaka 5 ya ndoa ilikuwa mizuri na waliishi kwa kuzingatia misingi waliyoiweka. Baada ya miaka mitano mkewe akaanza zile tabia ambazo ni kero kwa mumewe huku mume akimkumbusha kuwa anakiuka maagano lakini mkewe anaziacha wiki then anarudia tena.
Mbaya zaidi kuna kipindi mume alisafiri na katika kumpigia mkewe simu kumtakia hali na kumweleza habari za safari mkewe akashindwa kuwa seriuos kuhusu ule ujumbe kwani inaonyesha alikuwa ametingwa labda na TV au na kitu kingine. Hii hali ikawa imemuudhi mumewe na wakawa wanajibizana ki ugomvi ugomvi na hata aliporudi akawa amerudi na uso wa chuki.
Ilipofika usiku kitandani kana kwamba haelewi kilichomuudhi mumewe mkewe akaamuuliza mbona huongei na mimi kwa furaha? nini kimekuudhi?
Maswali haya yalimuudhi sana yule mume kwani hakujua mkewe haelewi nini wakati wamegombana jana kwenye simu na hawajasuluhisha.
Naomba mawazo yenu wana JF je mwanamke kama huyu utamwelewaje? amekupuuza? ameku ignore? au ana matatizo gani?. Na nini cha kumfanya ili awe na approach sahihi?
Hii ndio maana huyu rafiki yangu amesema hamuelewi mkewe hata baada ya kuwa kwenye ndoa kwa miaka 10 sasa. Naomba msaada wenu,
huy jamaa f*l* kabisa vitu vidogo kama hivi anataka ushauri wa rafiki yake ? akikuta sms ya mapenzi kwenye simu ya wife si anaweza ua ?
Mume ur the problem, acha kununa mzee
Mkuu nina wasiwasi na mtoa mada. Itakuwa yeye ndo mhusika na anazuga. Hi sio jitu ya kuomba ushauri, tatua mwenyewe. Mbona watu wazima wanadeka sana?
Wamezaa watoto wangapi? Je mke wake ameongeza kipato zaidi kabla ya hiyo miaka 10 ya ndoa? Alishawahi kumfumania mumewe kisha jamaa akaomba radhi? Amfuatilie kwa umakini ili ajue source ya kiburi chake. Wanawake wengi japo si wote hujikita katika kutafuta ndoa lakini wakizipata husahau juhudi kubwa waliyotumia katika kujishape ili waonekane wake bora.
haaah haaah duh hii imetulia!mwambie ampeleke kw babu akapate kkombe atamwelewa! Icjekuwa ni wewe then wajfnya ni rafk yko?