Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga

MBUZI MWENYE BUSARA

Senior Member
Nov 24, 2019
143
151
Habari wadau wa jukwaa hili pendwa,

Naomba nienda moja kwa moja kwenye mada.

Mimi nimeoa na Mungu amenijalia watoto wawili. Nafanya kazi sekta binafsi na mke wangu sasa ni mama wa nyumbani. Mke wangu kabla sijamuoa alikuwa amenunua kiwanja chake makao makuu ya wilaya na mimi pia nilikuwa nimenunua kiwanja changu katika wilaya hiyo hiyo ila kwenye tarafa mojawapo.

Tulipooana tuliamua kuishi wilayani, kipindi hicho mimi nilikuwa sina kazi ila yeye alikuwa na kazi japo si mshahara mkubwa na alikuwa kwenye kata mojawapo katika wilaya hiyo nami nilikuwa nimepanga makao makuu ya wilaya, ambapo yeye ndiyo alinunua kiwanja.

Mwaka mmoja baada ya ndoa nikaajiriwa mkoa mwingine hivyo nikamuacha yeye na mtoto, yeye akiwa bado anafanya kazi.
Nikaanza kujenga msingi kwenye kiwanja changu na sikuendeleza nikaachia kwenye msingi. Baadaye nikapiga msingi kwenye kiwanja chake.

Mwaka moja baadaye yeye akaachishwa kazi pale alipokuwa anafanya kazi, ikabidi niwachukue nikae nao mjini. Lakini nikaona ni gharama sana kupanga mjini na mshahara ni mdogo, nikaamua kuchukua mkono nikaendeleza msingi katika kiwanja chake kwa maamuzi kwamba, niendeleze hata vyumba kadhaa halafu niirudishe familia wilaya wakakae huko, mimi nichukue chumba kimoja kupunguza gharama.

Hili pia lilichangia na mgogoro, nikaona siku moja nitapoteza kazi halafu sina pakukimbilia wakati natafuta kazi nyingine. Nikaanza ujenzi na taratibu zote halmashauri nilifanya kwa jina langu. Nikajenga vyumba viwili nikaweka na umeme nikahamisha familia. Kwa sasa wana miezi kadhaa nakuwa nawatembelea walau kila mwisho wa mwezi.

Kilichonifanya niandike uzi huu ni kwamba mke analeta jeuri kwenye hiyo nyumba, kwa kiasi fulani amebadilika, maana juzi kati tulitofautiana jambo fulani dogo nikagundua kiburi kimempanda sana.

Pili, sasa hivi anapambana hati iwe kwa jina lake. Kwa sasa tuna harakati za kuweka maji anajitahidi ajaze fomu yeye kwa jina lake na pia juzi nililipia hela B con na imewekwa sasa yeye anataka kujiandika kama mwenye nyumba.

Ebu naomba ushauri wenu nimuache ajiandike? Nia yangu mimi ni kulinda ndoa yetu, maana naona yeye kama akipata umiliki atanisumbua na tutasababisha mgogoro utakao wasumbua watoto wetu.

Ebu naombeni ushauri kulingana na uelewa na uzoefu, maana mimi kama baba mwenye nyumba ni wajibu wangu kulinda familia yangu, wakina mama wanadanganyika haraka sana. Natarajia kumpiga marufuku harakati zote kwa mamlaka niliyonayo ila nasubiri ushauri wenu.

Asanteni.

Soma mrejesho wa kisa hiki: Mrejesho: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga
 
Mkeo anatazama sana mali kuliko ndoa na future yenu pamoja na watoto.

Kimsingi tayari ulisha fanya makosa kujenga kwenye kiwanja cha mkeo kabla ya kujadili kibadilike na kua kiwanja chenu (nadhani ulimuamini kama mke na mama wa watoto wako).

Haya uliyo yaeleza tayari ni dalili mbaya kwa afya ya ndoa yenu.
Nakushauri uishie hapo ulipo komea, usionyeshe tofauti, kuchukizwa wala kung'ang'ania nyumba uliojenga kwenye kiwanja cha mkeo na upatazame kama kituo cha kuwalelea watoto wenu.

Ongeza bidii kwenye kazi/tafuta kazi, na anza kuendeleza kiwanja ulicho kinunua ili nawewe uwe na kwako.

Pole sana mkuu
 
Mkeo anatazama sana mali kuliko ndoa na future yenu pamoja na watoto.
Kimsingi tayari ulisha fanya makosa kujenga kwenye kiwanja cha mkeo kabla ya kujadili kibadilike na kua kiwanja chenu (nadhani ulimuamini kama mke na mama wa watoto wako).
Haya uliyo yaeleza tayari ni dalili mbaya kwa afya ya ndoa yenu.
Nakushauri uishie hapo ulipo komea, usionyeshe tofauti, kuchukizwa wala kung'ang'ania nyumba uliojenga kwenyw kiwanja cha mkeo na uoatazame kama kituo cha kuwalelea watoto wenu.
Ongeza bidii kwenye kazi/tafuta kazi, na anza kuendeleza kiwanja ulicho kinunua ili nawewe uwe na kwako.
Pole sana mkuu
Kwa huu ushauri umemaliza kila kitu mkuu
 
Wanawake wengi siku hizi wamekua hawana hisia za mapenzi ya kweli (real love from within), hii hupelekea kutoishi katika ile misingi halisi ya ndoa na kuheshimu mamlaka ya baba kua kichwa cha familia na msimamizi wa mali.

Wamekua na mapenzi ya kuigiza hasa hawa tunaowaoa wakiwa wameshavuka 25+ maana wanakua tayari wana past experiences zao nyingi na ma-ex zinawafanya wawe na mixed feelings.

Kwa kifupi ktk kipindi cha uchumba wana uwezo mkubwa sana wa kuficha makucha yao hasa wakiona kuna fursa huko mbele. Watajitahidi kukuonyesha upendo wa hali ya juu ili mradi ujichanganye utangaze ndoa.

Kimbembe kinaanza mkishakua ktk ndoa focus yao kubwa huanza kua kwenye mali na watoto tu (ambao anaweza akawa amekubambikia pia). Wengi wanaamini wanaume hua tunakufa mapema, hivyo mali zikiwa kwa jina lake basi itakua nafuu kwake kuzilinda endapo ndugu zako wenye tamaa wataingilia kati (hawa mara nyingi hua hawana nongwa sana, ingawa ni rahisi kurubuniwa na ndugu zao wenye tamaa za mali muachane ili wanufaike wao).

Lakini wengine wameenda mbali zaidi ambapo mali zikiwa kwa majina yao hupandwa na viburi na kujiona wao ndio "wakuu wa kaya" na kumdharau moja kwa moja mwanaume ambae alipambana kuifikisha familia ilipo. Kundi hili ni lile linalorubuniwa na ma-ex au majamaa yanayowatongoza tongoza ovyo kila siku na kauli zao mbiu hua "kama vipi tuachane tu!". Yani muachane ili umuachie mali aendelee kudanga na mabwana zake au mwanaume wa ndoto zake ambae alishindwa kua nae wakati mpo kwenye ndoa.

USHAURI: Kijana jipange, hakikisha kabla haujaoa una mali zako ambazo kimsingi atakuja kuzikuta mkiwa mmeshaoana. Haya mambo ya kuchuma pamoja ktk ndoa yamekua ya kiduwanzi siku hizi. Otherwise KATAA NDOA! THESE H*** AIN'T LOYAL ANYMORE!!! Nakaribisha povu
 
Mkuu umesahau kuwa chako mwanaume ni cha familia ila cha mwanamke ni chake...jenga kwako ikibid tena bila yy kujua, na kama haitaleta mgogoro umiliki uwe wenu wote sio wew pekeako ili kumuondolea sumu inayofukuta ndani yake kwa manufaa ya watoto.
 
Mkeo ni aina ya wanawake walio wengi. Anajaribu kusort interest zake binafsi ndani ya ndoa jambo ambalo ni hatari. Kwa mtazamo wangu,hujawekeza sana hapo kwenye kiwanja chake. Mueleze bayana ubaya wa hiyo tabia na mtazamo wake kisha jitoe ktk kupaendeleza hapo!

Pambana kufa na kupona kutafuta hela kama mwanaume ( kwa sababu inavyoonekana bado huna hela). Jitume sana. Anza kujenga nyumba zako mjini (sio wilayani) kwa document zako. Hakikisha weww ndiye utakayekua na hela na utakayecontrol uchumi wa familia
 
Hiyo nyumba ya vyumba 2 si kitu, bado una energy ya kutosha kufanya mambo makubwa zaidi.

Mkeo inaonekana yuko short minded, anadhani hako kanyumba ndiyo kafika, kwamba kujenga ndiyo kila kitu kumbe sio. Ndani ya miaka kadhaa hako kanyumba katakuwa obsolete.

Kwa sasa ndio muda mzuri wa kuijua tabia halisi ya huyo mke wako. Kaa naye chini mchane wazi kwa nini amebadilika, na kwa nini anataka aandikwe yeye, anahofia nini ukiandikwa wewe kama baba mwenye familia?

Baada ya kumjua then utajua hapo una mke mke, ama mke mke wao.
 
Habari wadau wa jukwaa hili pendwa,

Naomba nienda moja kwa moja kwenye mada.

Mimi nimeoa na Mungu amenijalia watoto wawili. Nafanya kazi sekta binafsi na mke wangu sasa ni mama wa nyumbani. Mke . Kwa sasa tuna harakati za kuweka maji anajitahidi ajaze fomu yeye kwa jina lake na pia juzi nililipia hela B con na imewekwa sasa yeye anataka kujiandika kama mwenye nyumba.
.

Asanteni.
Kiwanja ni cha mke ila kosa ni kusaidia kujenga hapo hivyo acha kelele kwenye nyumba ya mke wako.
 
Wanawake wengi siku hizi wamekua hawana hisia za mapenzi ya kweli (real love from within), hii hupelekea kutoishi katika ile misingi halisi ya ndoa na kuheshimu mamlaka ya baba kua kichwa cha familia na msimamizi wa mali.

Mwishon hapo umemaliza kibabe sana
 
Kama ulivyo sema Nia yako ni kulinda ndoa yako lakini mwenzio pengine nia yake ni kuivunja ndoa yenu hapo tuta hesabu maumivu ...
 
Back
Top Bottom