Mkumbavana
Member
- Jan 24, 2012
- 79
- 22
Asalam aleikum, mimi ni mwanaume rijali mwenye mke 1 na watoto 2,kwa muda mrefu mke wangu amekua haelewani na mama yangu mzazi, na kila ninayeongea naye ili kujua tatizo anamlaumu mwenzie, nikaonelea nikate mawasiliano ya chakula cha usiku/ndoa na mke na niwe nachelewa home ili kumshikisha mke adabu kama mnavyojua hakuna kama mama,matokeo yake nikiwa kazini nimepokea ujumbe toka kwa wife kuwa nanukuu "nakupenda sana mume wangu,kama umeamua hivyo basi nakuomba unitaftie mtu wa kuniliwaza maana mm sijui pa kuanzia na siwezi kuvumilia upweke tena" nimeshindwa kujua nimzibue au nimfukuze,mpaka sasahivi niko bar nagonga maji na nina mawazo tele,msaada jamani nifanyaje