LIKUD
JF-Expert Member
- Dec 26, 2012
- 15,115
- 27,104
Hii nimesimuliwa na ndugu yangu, hebu msikilize mwenyewe :
...Mimi kama LIKUD nilimpa ushauri wangu, but na nyinyi wana JF mnaweza toa mawazo yenu, nitakayo ona yanamfaa jamaa ninaweza yaongeza kwa ajili ya kumshauri zaidi.Nilifahamiana na mke wangu tangu tulipokuwa tunasoma chuo kikuu, tulianza kama marafiki baadaye tukafunga baada ya kumaliza chuo na kupata kazi. Sasa kuna huyu jamaa ambaye ni rafiki yangu tangu tupo chuo na anafahamu uhusiano wangu na mke wangu tangu tunasoma, na infact yeye ndiye aliyekuwa bestman wangu.
Mwaka mmoja baada ya mimi kufunga ndoa , best man wangu nayeye akafunga ndoa, halafu akaja kuishi jirani kabisa na nilpokuwa naishi mimi, yeye alikuwa amejiajiri mwenyewe.. Mpaka wakati wote huo sikushtukia kama mke wangu na yule rafiki yangu walikuwa wanatoka....
Miaka miwili baadaye nikapangiwa Iringa kikazi, yule rafiki yangu na mke wake nao wakahamia Iringa tena palepale tulipokuwa tunaishi sisi, ( Rafiki yangu a likuwa anatoa kisingizio cha urafiki wetu mimi na yeye ambao kwa kweli tulikuwa kama ndugu ), tukaa pale Iringa kwa mwaka mmoja, nikapewa transfer na kuhamia Tabora, muda mfupi baadaye rafiki yangu na yeye akahamia Tabora, Sikukaa sana tabora miezi tisa baadaye nikarejeshwa makao makuu Dar es salaam, rafiki yangu na yeye akahamia tena Dar es salaam. ( Kwa muda wote huo sikuwa nimehisi chochote kati ya mke wangu na huyo rafiki yangu ) hadi wiki mbili zilizo pita shemeji yangu ( yani mke wa rafiki yangu ) aliponikalisha chini na kuniambia mchezo mzima, akaniambia yeye alishtukia tangu muda mrefu na muda wote huo alikuwa anamvumilia mumewe mpaka uvumlivu ulipo mshinda, so kwa kuwa imemuuma sana, kaamua kuja kunifuata ili na sisi tufanye kweli ili kulipa kisasi ) .
Maneno ya shemeji yangu yaliniumiza sana moyo na ni kama yalinizindua kutoka usingizini coz mambo mengi nilikuwa siyaoni kwa sababu nilikuwa namuamini sana mke wangu na nisingetegemea kama angefanya uchafu kama huo. Shemeji yangu aliniambia mambo mengi sana ambayo nikiya connect napata picha kamili, hapa nilipo nimechanganyikiwa sijui nimfanye nini huyu mke wangu ama nichukue uamuzi gani?...