Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
22nd October 2009
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete, amejikuta akikumbana na mauzauza ya aina yake katika ziara yake ndani ya wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro baada ya wananchi kibao kuzomea mfululizo, kisa kikiwa ni kumpinga mbunge wa jimbo lao la Ulanga Magharibi, Dk. Juma Ngasongwa.
Mauzauza hayo ya zomeazomea kwa mbunge (Ngasongwa), mbele ya mke wa Rais, yalitokea jana wilayani humo, ikiwa ni mara tu baada ya wananchi kutajiwa jina la Dk. Ngasongwa.
Kwa ujumla, sakata lenyewe ambalo aibu yake ilizidi maradufu baada ya wanafunzi kibao wa shule za sekondari kuungana na watu wazima katika kuzomea lilikuwa hivi:
Kwanza, Mama Salma na msafara wake waliwasili katika Tarafa ya Malinyi kwa ajili ya kuendelea na ziara yake ya kukagua na kuhamasisha shughuli mbalimbali za maendeleo ya wanawake wilayani Ulanga.
Kama kawaida yake, Mama Salma alipokewa kwa furaha, chereko na na watu kibao waliofurika kumshuhudia wakati akiendelea na shughuli zake, ikiwa ni pamoja na kugawa misaada ya vifaa vya afya katika kituo cha Afya cha Mtimbira ambacho hutoa huduma kwa wajawazito.
Wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa hivyo vya afya kwa kituo cha Mtimbira, ndipo mauzauza yalipotokea, mara tu baada ya Mkuu wa Wilaya ya Ulanga,
Dk. Rajabu Rutengwe kumtambulisha Ngasongwa.
Mkuu wa Wilaya alipolitaja tu jina la Ngasongwa, umati wa watu uliokuwepo ukalipuka ghafla kwa kelele za kuzomea bila kukoma, huku wengine wakipiga miluzi ya kebehi.
Hata hivyo, mbunge huyo hakuwepo kwenye hafla hiyo huku taarifa nyingine zikidai kuwa machale yalishamcheza kitambo, kwani awali alionekana akishiriki mapokezi ya Mama Salma na kuongozana naye hadi katika tarafa hiyo.
Baadaye tena, wakati Mkuu wa Wilaya akisoma taarifa ya maendeleo wilayani humo na kumtaja Ngasongwa, wananchi walilipuka tena na kuzomea kwa jazba, huku wakipinga hatua ya kutajwa tajwa kwa mbunge huyo waliyedai hana msaada wowote kwao.
Hali hiyo ilielekea kuvuruga utaratibu na kumfanya Mama Salma aingilie kati na kumfanya Mkuu wa Wilaya aseme 'Mtimbila oyeee...!'.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Issa Machibya, pia alishangazwa na wananchi hao ambao walizomea kwa nguvu pale naye alipolitaja jina la Ngasongwa.
"Hana msaada kwetu... hayupo pamoja nasi na siku zote hujitokeza pale viongozi mbalimbali wanapofanya ziara zao huku, wakiondoka naye haonekani... nadhani ndio maana watu wanazomea kila wanaposikia jina lake," akasema mmoja wa wananchi waliokuwepo kwenye hafla hiyo.
Kama hiyo haitoshi, tukio kama hilo pia lilijitokeza tena katika Shule ya Sekondari Kipingo wakati Mama Salma alipotembela na kugawa zawadi ya jezi kwa moja kati ya shule nane ambazo wanafunzi wake walikusanyika hapo (Sekondari ya Kipingu) kwa ajili yake.
Mama Salma alikutana na mauzauza hayo pale alipowaambia wanafunzi wa shule zote nane ambao walikusanyika kwa ajili yake kuwa hakutegemea kama angekutana na shule zote, hivyo akaahidi kukabidhi jezi nyingine kwa mbunge wao.
Dk. Ngasongwa au Mkuu wa Wilaya ili waliokosa nao wapate jezi hizo.
Wanafunzi hao ambao idadi yao ilizidi 500, bila kuchelewa, nao wakazomea kwa nguvu pindi alipotajwa Ngasongwa ambaye kwa wakati huo alikuwepo jukwaani.
Wanafunzi hao walizomea baada ya Mama Salma kusema zawadi nyingine za shule saba, atamkabidhi yeye (Ngasongwa).
Hata hivyo wanafunzi hao walikataa zawadi zao asipewe mbunge na badala yake ampatie Mkuu wa Wilaya (Dk. Lutengwe) ili awafikishie.
Ili kuua soo, Mama Salma aliingilia kati na kutumia busara, akisema kuwa atampatia seti mbili za jezi Dk. Ngasongwa ili azigawe kwa baadhi ya shule na nyingine atampa Mkuu wa Wilaya kama walivyotaka wanafunzi hao.
CHANZO: ALASIRI
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete, amejikuta akikumbana na mauzauza ya aina yake katika ziara yake ndani ya wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro baada ya wananchi kibao kuzomea mfululizo, kisa kikiwa ni kumpinga mbunge wa jimbo lao la Ulanga Magharibi, Dk. Juma Ngasongwa.
Mauzauza hayo ya zomeazomea kwa mbunge (Ngasongwa), mbele ya mke wa Rais, yalitokea jana wilayani humo, ikiwa ni mara tu baada ya wananchi kutajiwa jina la Dk. Ngasongwa.
Kwa ujumla, sakata lenyewe ambalo aibu yake ilizidi maradufu baada ya wanafunzi kibao wa shule za sekondari kuungana na watu wazima katika kuzomea lilikuwa hivi:
Kwanza, Mama Salma na msafara wake waliwasili katika Tarafa ya Malinyi kwa ajili ya kuendelea na ziara yake ya kukagua na kuhamasisha shughuli mbalimbali za maendeleo ya wanawake wilayani Ulanga.
Kama kawaida yake, Mama Salma alipokewa kwa furaha, chereko na na watu kibao waliofurika kumshuhudia wakati akiendelea na shughuli zake, ikiwa ni pamoja na kugawa misaada ya vifaa vya afya katika kituo cha Afya cha Mtimbira ambacho hutoa huduma kwa wajawazito.
Wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa hivyo vya afya kwa kituo cha Mtimbira, ndipo mauzauza yalipotokea, mara tu baada ya Mkuu wa Wilaya ya Ulanga,
Dk. Rajabu Rutengwe kumtambulisha Ngasongwa.
Mkuu wa Wilaya alipolitaja tu jina la Ngasongwa, umati wa watu uliokuwepo ukalipuka ghafla kwa kelele za kuzomea bila kukoma, huku wengine wakipiga miluzi ya kebehi.
Hata hivyo, mbunge huyo hakuwepo kwenye hafla hiyo huku taarifa nyingine zikidai kuwa machale yalishamcheza kitambo, kwani awali alionekana akishiriki mapokezi ya Mama Salma na kuongozana naye hadi katika tarafa hiyo.
Baadaye tena, wakati Mkuu wa Wilaya akisoma taarifa ya maendeleo wilayani humo na kumtaja Ngasongwa, wananchi walilipuka tena na kuzomea kwa jazba, huku wakipinga hatua ya kutajwa tajwa kwa mbunge huyo waliyedai hana msaada wowote kwao.
Hali hiyo ilielekea kuvuruga utaratibu na kumfanya Mama Salma aingilie kati na kumfanya Mkuu wa Wilaya aseme 'Mtimbila oyeee...!'.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Issa Machibya, pia alishangazwa na wananchi hao ambao walizomea kwa nguvu pale naye alipolitaja jina la Ngasongwa.
"Hana msaada kwetu... hayupo pamoja nasi na siku zote hujitokeza pale viongozi mbalimbali wanapofanya ziara zao huku, wakiondoka naye haonekani... nadhani ndio maana watu wanazomea kila wanaposikia jina lake," akasema mmoja wa wananchi waliokuwepo kwenye hafla hiyo.
Kama hiyo haitoshi, tukio kama hilo pia lilijitokeza tena katika Shule ya Sekondari Kipingo wakati Mama Salma alipotembela na kugawa zawadi ya jezi kwa moja kati ya shule nane ambazo wanafunzi wake walikusanyika hapo (Sekondari ya Kipingu) kwa ajili yake.
Mama Salma alikutana na mauzauza hayo pale alipowaambia wanafunzi wa shule zote nane ambao walikusanyika kwa ajili yake kuwa hakutegemea kama angekutana na shule zote, hivyo akaahidi kukabidhi jezi nyingine kwa mbunge wao.
Dk. Ngasongwa au Mkuu wa Wilaya ili waliokosa nao wapate jezi hizo.
Wanafunzi hao ambao idadi yao ilizidi 500, bila kuchelewa, nao wakazomea kwa nguvu pindi alipotajwa Ngasongwa ambaye kwa wakati huo alikuwepo jukwaani.
Wanafunzi hao walizomea baada ya Mama Salma kusema zawadi nyingine za shule saba, atamkabidhi yeye (Ngasongwa).
Hata hivyo wanafunzi hao walikataa zawadi zao asipewe mbunge na badala yake ampatie Mkuu wa Wilaya (Dk. Lutengwe) ili awafikishie.
Ili kuua soo, Mama Salma aliingilia kati na kutumia busara, akisema kuwa atampatia seti mbili za jezi Dk. Ngasongwa ili azigawe kwa baadhi ya shule na nyingine atampa Mkuu wa Wilaya kama walivyotaka wanafunzi hao.
CHANZO: ALASIRI