Mke hataki ndugu wa mume:Msaada please.

Mbona mnakuza mambo, Issue ni mke hataki ndugu za mme na limejionyesha wazi wazi baada ya ndugu yake kuja na hakuongea chochote..

hahaha!sawa crash lkn je,,amewahi kuongea nae mara ngapi juu ya hilo kabla ya kumtimua?
 
Duh Haika lah!

Tribaphobia! - right?
kwa kiasi, fulani.
pia phobia ya dini!!
kwanini useme eti hawa si waswahili tu!!! au si unajua tena wakristu au waislamu!! au
Eti wahaya, wangoni, wazaramo, wasukuma, mtu anaambiwa kafanya ishu fulani kw akuwa yeye ni kabila au dini fulani.
habari nzima inapoteza uzito wake!

mimi huwa naamini kuna wakati ndoa inafika mahali lazima ivunjike hapo ni wakati wahusika wote wawili wanapokuwa hawako radhi kubadilika ili kusikilizana tena kama awali. kama hawa inawezekana wameshafikia point of no return.
 
Kwa ndugu yake mbona hakujadili na bado hakuongea chochote....kifupi jamaa anatakiwa asimamie maamzi yake kama kicho cha familia na akileta msimamo wake wa kuto wataka ndugu za mme amtimue....

Hiyo alikuwa anafahamu sana kuwa ndugu yake anatakiwa kuja but kwa kumheshimu mume wake alimuomba huyo ndugu mwenye mtoto amuombe mume kama mkuu wa familia na hilo pia mume alitakiwa kulifikisha mezani but kwa kichwa chake cha mfume dume akona yeye ni final say. Sasa
 
Kwa ndugu yake mbona hakujadili na bado hakuongea chochote....kifupi jamaa anatakiwa asimamie maamzi yake kama kicho cha familia na akileta msimamo wake wa kuto wataka ndugu za mme amtimue....

Amtimue? vipi kama hapo wanapoishi ni kwa mwanamke?
 
Ngoja nikupe ushauri, mimi kama dada wa kichaga.
Kwa kuwa upependa kutaja kabila la mke bila kutaja kabila la mume unadhani huo ukabila wa mke ni muhimu katika ushauri unaotegemea?

Basi ni hivi,
1. Mwambie amuache huyo mwanamke atafute wa kabila lake au lako wewe.
2. Awape funzo ndugu zake wote wasijeoa wachaga kwani watawakataa ndugu zao na hao wanawake wataleta ndugu zao nyumbani.

Iwe onyo na fundisho kwao.
Pole sana mama,
lakini ni kweli wachaga walio wengi wamekuwa na tabia ya kutokutaka kukaa na ndugu za mme lakini linapokuja swala la ndugu wa zake haongei na tena utapaswa kuwapeleka shule kwa garama mme...ninamifano ya kutosha
 
ngoja nikupe ushauri, mimi kama dada wa kichaga.
Kwa kuwa upependa kutaja kabila la mke bila kutaja kabila la mume unadhani huo ukabila wa mke ni muhimu katika ushauri unaotegemea?

Basi ni hivi,
1. Mwambie amuache huyo mwanamke atafute wa kabila lake au lako wewe.
2. Awape funzo ndugu zake wote wasijeoa wachaga kwani watawakataa ndugu zao na hao wanawake wataleta ndugu zao nyumbani.

Iwe onyo na fundisho kwao.
pole dada kwa kuguswa na ukabila ,msamehe ila anahitaji ushauri kuna watu wamekuwa na stereo type hizi,mimimmke wangu ni mmeru huwa napata shida kuwa umeoa wanaofanan na wachaga ila ninavyo fahamu ubaya /ukatili upo kwa mtu
 
tatizo ni kutoshirikishwa amuombe msamaha tatizo wanaume neno samahani ni la kichina kwao hawalitamki kabisa . alipaswa kushauriana na mke wake hasa ukizingatia suala la malezi ni nyeti na kama kweli mtoto ni tukutu atawaharibu na wao wangeshauriana waone namna wangeweza kumlea .
duh na kwa bi dada huyo asiwe kama mwanamgambo wa taliban apunguze msimamo imeshakuwa ameletwa amlee kama mwanaye kwani angekuwa mtukutu asingemlea .
ila kama hataki kuelewa japo mm ni mwanamke lakini nasema apigwe talaka yake alale mbele
 
Hili ni tatizo kubwa kwa wanawake wengi sana, labda linahitaji utafiti kujua chanzo ni nini. Wengi hawapendi kabisa ndugu wa kiume. Ila kuntimua mke sio sahihi sana, kwani kosa moja haliachi mke.
 
hahaha!sawa crash lkn je,,amewahi kuongea nae mara ngapi juu ya hilo kabla ya kumtimua?
ukisoma mada utaelewa kuwa ni tatizo la siku nyingi na mwanamke amekuwa akisisitiza hamtaki yule mtoto yatima kisa hakushirikishwa kibusa kama hakushirikishwa kwenye swala kama hilo angemweleza mme wake asiwe anafanya maamzi kama hayo na siyo kumtaka aondolewe yule mtoto...aendewapi sasa huyu yatima...
 
tatzo jamaa anafanya maamuz bila kumshrikisha mkewe na ndo hapo tatzo linapotokea mwambie aache ukiritimba au umimi anaish na mkewe hvyo itakuwa flesh kama akimshrkisha mkewe kwanza ni hlo 2uu mm ndo ninalaliona japokuwa huyo mkewe nae anatatzo la kuchukia ndugu wa mume wake ila huwa wepesi kuelewa kama akiwashrkisha vzur sawa man
 
mie nadhani ndoa yenu haihang kwenye balance..huyo mwanamke anataka yeye ndio achukue nafasi ya huyo mwanaume na kuiendesha familia..
mie nakushauri kama wewe ndio 'provider' wa familia yenu then lazima u man-up na kuwa na final say!kuwa aggresive kidogo kny maamuzi na matendo yako usimruhusu akakuendesha...
kama wewe na mkeo wote ni provider wa familia yenu then jaribu kumshirikisha mkeo katika maamuzi yoyote yale...

cha kufanya kuwa na courage,mface mkeo na umwambie wazi kuwa tabia yake ya kugomba kuhusu huyo mtoto yatima na kuacha ndugu yake HUIPENDI,na asipojirekebisha utafanya maamuzi mazito ya kumtimua!:coffee:
 
Kuweni na akili kama nyoka na wajanja kama huwa.
Kwanza mpendwa mtoa mada kama umetaja kabila la huyu dada ili tutoe ushauri
kwa kuangalia na hilo, haujawa sahihi, labda ungetuambia na kabila la huyo baba.

Mwanaume ni kichwa cha nyumba ni kweli,
Tumeambia tuwatii waume zetu kweli, lakini katika mambo mema.

Mwanaume huyu asifanye maamuzi tu kwa sababu yeye ni wanaume hapana,
Aishi na mke wake kwa akili. Amshirikishe katika hali ya upendo, heshima na adabu.
Aaache mfumo dume wa kijinga. Kwa ajili ya ustawi wa ndoa yake, familia yake na ndugu zake.

Inavyoonekana wewe na jamaa wengine na mume mwenyewe mnaona kasoro kwa huyo zinatokana na kabila,
hamwezi kumaliza tatizo kwa mtazamo huo. Mtazameni yeye kama yeye, mwambie azungumze na mke wake,
waelewane wao wawili kwanza halafu watafikia mwafaka wa jinsi ya kumlea huyo mtoto.

Wakumbuke kwamba kumlea huyo mtoto ni wajibu wao wote, na Mungu atawabariki, hata kama asingekuwa
ndugu yao. (Mungu ni baba wa yatima, hata wasipomlea wao kwa kiburi chao, Mungu atainua watu kwa ajili yake)

Hapa wakubali kuwa wanyenyekevu waache kiburi na ukoloni, wajue tunaishi kwa neema,
Huyo baba ajitambue anakosea wapi ashuke na huyo mama ajitambue anakosea wapi ajishushe pia,
Kwa sabau hapo watu wanaishi kwa kiburi na ndo maana huyo baba kamkubali huyo ndugu wa mwanamke kwa kiburi,
ili aone mama atasema nini, na huyo mama nae kwa kiburi akanyamaza.

Kiburi ni tabia ya shetani. Kawaambie wote wawili waache kiburi.
Wakae wayamalize, maisha yaendelee,
Waambie wanajua je ju ya watoto wao. Je wanauhakika wataishi mpaka watoto wao waweze kujitegemea??
Mbona wanashindani katika mambo yasiyo na maana. ASK THEM DO THEY KNOW ABOUT THEIR TOMORROW??
 
Kuna jamaa yangu kaniomba ushauri juu ya tatizo linalomkabili. Yeye kaoa mke Mchagga. Baada ya kufiwa na mdogo wake wa kike, ndugu waligawana watoto wa marehemu na yeye(jamaa) akapewa mtoto m1 ili amtunze na hasa ikizingatiwa kuwa hakuwa na baba. Matatizo ya mke ndo yakaanza. Mara simtaki huyo mtoto kwa kuwa hukunishirikisha. Mara mtoto huyo ameshndikana huko alikotoka kwa kuwa ni mtundu. Mke ameendelea kusistiza kuwa hamtaki huyo mtoto licha ya kupita miaka 3 sasa. Kutokana na presha ya mke wake, jamaa aliamua kutafuta shule ya boarding ya watoto yatima lakini bila ya mafanikio. Pia aliwahi kumchukua ndugu yake mmoja ili amsaidie kwenye biashara zake lakini kelele za kumkataa zikasikika na hatimaye yule kijana akaondoka. Jamaa wiki iliyopita aliombwa na ndugu wa mke ampokee kijana wake akae kwake ili ajiandae kure-sit mtihani wa fm4 mwaka huu. Jamaa hakuwa na hiana akamkubalia bila ya kumshikisha mke wake huku akihofia kelele za mke wake kwa kutomshirikisha. Kijana kafika na hakuna kelele.

Atafute shule ya bdng sio lazima iwe ya watoto yatima, na mtoto akifunga shule akae nae siku chache ampeleke kutembea kwa ndugu wengine mpaka atakapokua mkubwa na anauwezo wa kujitetea ndo awe anakaanae akifunga shule. Ila kwa kiasi flani mama huyo hafai.
 
tatzo jamaa anafanya maamuz bila kumshrikisha mkewe na ndo hapo tatzo linapotokea mwambie aache ukiritimba au umimi anaish na mkewe hvyo itakuwa flesh kama akimshrkisha mkewe kwanza ni hlo 2uu mm ndo ninalaliona japokuwa huyo mkewe nae anatatzo la kuchukia ndugu wa mume wake ila huwa wepesi kuelewa kama akiwashrkisha vzur sawa man

Kuchukia ndugu mara nyingi hua inatokana na malezi alolelewa, kama ameishi akiona mamaake au baba anabagua ndungu wa upande mmoja mara nyingi atafuata hivyo. Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo, haitokei tu from no where.
 
Ngoja nikupe ushauri, mimi kama dada wa kichaga.
Kwa kuwa upependa kutaja kabila la mke bila kutaja kabila la mume unadhani huo ukabila wa mke ni muhimu katika ushauri unaotegemea?

Basi ni hivi,
1. Mwambie amuache huyo mwanamke atafute wa kabila lake au lako wewe.
2. Awape funzo ndugu zake wote wasijeoa wachaga kwani watawakataa ndugu zao na hao wanawake wataleta ndugu zao nyumbani.

Iwe onyo na fundisho kwao.

Acha ligi wewe, kataja kabila tu hakumaanisha wanawake wote wakichaga, pengine asingetaja watu wangemuuliza chakwanza, huyo mama ni kabila gani.
 
Baada ya msg kuwa delivered,
ushauri wangu wa ukweli ni kuwa:
1. mnapoingia kwenye ndoa muwe makini na kuangalia streghts za personalities zenu, na muwe tayari kuishi nazo. Mie sipendi kuona mtu anaishi na mkewe au mumewe huku anaogopa kuleta baadhi ya hoja mezani. Hio si ndoa ni ndoano, na lazima mmoja huyo atakuwa mnyonge na atatia huruma sana hata kwa ndugu na jamaa zake. ajitahidi kumatch up na arguments (hoja) za mkewe, aje na hoja mezani.
Ndoa za kiafrika wote tunaelewa ni za kiukoo zaidi kuliko mtu mmoja mmoja.
2. Kwa huyo jamaa yako bila kuwa wazi baba na mama, lazima kuna mambo mengi sana yametokea hapo nyuma, sie wanawake mara nyingi huwa tunaunganisha matukio mengi madogo madogo na kuyatafakari kwa ujumla wake, kuna habari hatuwezi kuijua hapa.
2. Ajiweke kwa ajili ya mke wake, bila kujidharaulisha, na abainishe wazi majukumu ya kulea ndugu,
KWA KIFUPI ATAMBUE MAANA YA KUITWA BABA, si sifa wa la cheo ni MAJUKUMU. Awe tayari kwanza kuwa BABA WA NYUMBA YAKE ndio ataweza kuwa msaada wa watu wengine.

hili ni tatizo kubwa sana kuliko tunavyodhania.
Personalities za wanaume kwa miaka ya karibuni mimi huwa naona kama wanaanza kukubali kuwaachia wanawake kuprovide security ya familia, hii itatucost, wote wanawake na wanaume.
Kuna mwalimu wangu alikuwa anasisitiza sana wanafunzi wa kiume wasome sana, wasikubali kupitwa na wasichana, alikuwa naogopa sana kuwa watakuja kudharauliwa baadae, mie kil amara huwa nakumbuka na kuzidi kuona ukweli wa maneno yake mengi kama haya:
- we mtoto wa kuime usikubali kudharauliwa,
- usiache familia yako isikutegemee, hakikisha unawatunza
- mwanaume anatakiwa awe radhi hata kukesha ili kulinda familia yake
- mtoto wa kiume halii mbele ya mtoto wa kike
- mwanaume anatakiwe awe jasiri wakati wote
- jibebeshe jukumu la kutunza familia yako kwa heshima
- usikubali mwanamke akulishe atakudharau au utajidharau
- mwanaume huwezi kusamehewa kwa kukosa uelekeo na msimamo wa maisha yako
nk nk

Haika nimekubaliana na ushauri wako. Hata mm yalinikuta kwa mtoto wangu wa kujifunzia na kesi ilienda mpaka ukweni,haikusaidia nilionekana simsikilizi mke mke wangu japo siyo kweli. Nisingeweza kumuondoa mtoto wangu wa kumzaa kisa mke wangu hampendi. Na wakati anaolewa alijua na kuwa nina mtoto. I stood up with my decision ya kukaa na mtoto wangu. Nilipopata transfer ya kazi haikuwa rahisi kuondoka na familia mara moja. Guess what happen nilipoondoka. Mtoto alisafirishwa kwa dada yangu faster, ilibidi niingie gharama ya kutafuta shule ya boarding ambayo nayo kutokana na umbali hela zilichakachuliwa na mtoto kupelekwa kijshule ambacho siku nimeenda likizo nilitamani kulia. Thanks God nipo na mke wangu na watoto wangu wote.Though najua kuna ugumu furani wa yeye kukaa na huyu mtoto but nina msimamo kwa watoto wote bila upendeleo. Sasa nikitaja kabila najua utanichapa acha niishie hapo. Ila ukweli kuna shida sana kwa akina dada kupendelea upande mmoja japo siyo wote.
 
Jamani msimlaumu Dada haika,
jamaa anayetaka ushauri amekosea kutaja kabila la huyo mwanamke, ina maana alikuwa anataka ushauri ambao utashirikisha kabila, Kwamba Uchagga wa huyo my wife wake ndio tatizo
pili inaonekana huyo ndugu yake anapewa lawama nyingi sana kwa kuoa mchaga, yaani matatizo yote yanasababishwa na Uchagga
ilikuwa haina sababu kabisa ya Kutaja kabila la huyo mama, Mi si Mchagga lakini inaboa kudiscuss Tabia ama Uamuzi wa mtu kwa kigezo cha kabial lake

Hapana jamaa hakutaja kwa nia mbaya, im sure asingetaja swali la kwanza angeulizwa huyo mwanamke ni kabila gani. Sidhani kama inaweza kumkasirisha mtu hee.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom