Mkakati wa CCM Kulitumia Bunge kujisafisha na Mauaji ya Mtu Iramba

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,798
71,218
Wakuu nimefuatilia michango ya Wabunge wa CCM kwenye Budget ya Ulinzi leo hii na imejionyesha dhahiri kuwa kuna mkakati wa pamoja wa wabunge wa CCM katika kupotosha ukweli juu ya mauaji yaliyofanyika huko Ndago Iramba.
Kila Mbunge kabla ya kuchangia alitafuta maneno yatakayo onyesha huruma waliyo nayo juu ya kupotezwa maisha kwa mtu huyo. Pia kutuhumu Chadema moja kwa moja kuwa inahusika wakati suala hilo liko chini ya Polisi kwa uchunguzi.
Hata Mbunge wa Serengeti alipotamka kuwa Chadema inahusika na mbunge wa Upinzani alipoomba taarifa Spika Makinda alimtolea nje.
Nadhani CCM kwa vile wanajua kuwa Bunge linafuatiliwa kwa karibu na Watanzania wengi kwa sasa wamejipanga kutumia nafasi hiyo kuficha njama za Mwigulu zilizopelekea kadhia ya kifo cha mmoja wa Wana CCM.
 
Ushahidi wa kwanza migulu amesema marehemu alikuwa msaidizi wake. Ahojiwe anamsaidia nini, maana maandiko yanasema Mungu alimuumba mwanamke amsaidie mwanamume. Msaidizi wa migulu ni wake zake
 
tumeshawazoea hawana cha maana hao wabunge wa ccm .kazi yao ni kuunga mkono kila hoja na uongo unahalishwa kuwa ukweli.Mwisho wao umefika na watanzania wengi wameanza kufunguka .Tunaomba Mungu afunge na kukisambatisha kabisa chama cha mafisadi hakuna kinachofanya katika kutatua shinda za wananchi.kimebaki na kulubuni vijana walalahoi kufanya kila utekaji na uuaji kwa kuwapa ahadi na viroba.
 
Ushahidi wa kwanza migulu amesema marehemu alikuwa msaidizi wake. Ahojiwe anamsaidia nini, maana maandiko yanasema Mungu alimuumba mwanamke amsaidie mwanamume. Msaidizi wa migulu ni wake zake

Hata baada kumuuwa binadamu mwenzenu bado mnapata ujasiri wa kumtusi?
 
Ee Mungu yote unayaona na ninaamini hakuna litakalopita kile ulichokipanga........
kusema kweli ninachokiona haiwezekani mfa maji akaacha kutapatapa! hivyo sioni la ajabu ktk hili!
 
huyo mbunge wa ccm aliyesema cdm inahusika na hayo mauaji je amepewa siku saba alete ushahidi kama akina mnyika wanavyoambiwaga??
 
Ikiwezekana wekeni jina la kila mbunge atakayeonekana kudandia haya mauaji. Ni vizuri wananchi wajue level ya usaliti wa wabunge wa CCM. Hii list iwekwe itafaa sana 2015.

Kwa sasa hivi ni wazi, wabunge wa CCM wameamua kuchapa usingizi kwenye kitanda cha mafisadi na ndio maana hawastuki hata pale polisi inapopeleka vichaa mahakani. Mbunge kama huyo wa Serengeti hakusema chochote kuhusu mauaji ya Arumeru. Yuda Eskarioti watupu, wameweka vipande 30 Swiss na huku wanaangamiza wananchi. Jangwani bado inaendelea.
 
Hata baada kumuuwa binadamu mwenzenu bado mnapata ujasiri wa kumtusi?

usitafute kujiosha mwingulu wewe ndio chanzo cha kifo cha msaidizi wako!
Tuambie msaidizi wako alimtuma akarushe mawe kwenye mkutano wa cdm?

Usitafute huruma ya watanzania umechangia mauaji ya mwenyekiti wako!
 
Tyson baada ya kuwa tishio ktk masumbwi alikuwa anafanya mazoezi ya speed na nguvu tu. akasahau pumzi! Evernda akaamua kufanya mazoezi ya pumzi. na alipokutana na Tyson round za mwanzo akafanya kukwepa makonde mazito ya Tyson hadi Tyson akaishiwa pumzi! Tyson akaishia kung'ata sikio la mwenzie badala ya kurusha makonde! ukawa ni mwisho wa Tyson! ccm vilevile ilizoea kupambana na waponzani wakt wa uchaguzi tu baada ya hapo wanajiachia hadi uchaguzi mwingineee.. sasa wamekutana na mwanaume wa ukweli alie na pumzi za kutosha! mwanzo mwisho! wameamua kung'ata! maana yake sasa itabaki kuwa historia kama ya Tyson..
 
Kwa maoni yangu Nchemba bado hajaelimika, kalewa cheo pamoja na zile pesa chafu za chama. Its very disgusting to listen to this kind of greedy leaders tena ndani ya jengo la heshima kwa nchi hii. That's is the place we expected to hear some critical thinkings/ideas for the country and her people. Lakini leo, kwa inshu hii siyo wanaJF wanaopata simanzi kutokana na hizi jeuri za wabunge wa CCM nazitawaliza soon or later. They will never be free kwani ukweli utazidi kuwatafuna. Lets wait and see!!
 
Amini nawaambieni watanzania wa leo si wa jana watakaouamini huo uongo ni ccm wenyewe.....kwani si walimsingizia shibuda kipindi cha uchaguzi kaua ili asishinde uchaguzi na akashinda............ivi kwenye mkutano wa wenzako umefuata unarusha mawe ili iweje...hiyo ni fimbo ya Mungu...ivi kuna lugha chafu kama ya lusinde na mbona hakupigwa mawe.Mwigulu ni shetani mwenyewe eti anatishiwa kuua si awataje wauaji mbona anawabania kama hizo msg hajajitumia mwenyewe
 
wakuu nimefuatilia michango ya wabunge wa ccm kwenye budget ya ulinzi leo hii na imejionyesha dhahiri kuwa kuna mkakati wa pamoja wa wabunge wa ccm katika kupotosha ukweli juu ya mauaji yaliyofanyika huko ndago iramba.
Kila mbunge kabla ya kuchangia alitafuta maneno yatakayo onyesha huruma waliyo nayo juu ya kupotezwa maisha kwa mtu huyo. Pia kutuhumu chadema moja kwa moja kuwa inahusika wakati suala hilo liko chini ya polisi kwa uchunguzi.
Hata mbunge wa serengeti alipotamka kuwa chadema inahusika na mbunge wa upinzani alipoomba taarifa spika makinda alimtolea nje.
Nadhani ccm kwa vile wanajua kuwa bunge linafuatiliwa kwa karibu na watanzania wengi kwa sasa wamejipanga kutumia nafasi hiyo kuficha njama za mwigulu zilizopelekea kadhia ya kifo cha mmoja wa wana ccm.

myika acha hizo ndio hii uliosema unakuja nayo sasa hivi
 
Tatizo kubwa kwa CCM ni kuwa asilimia kubwa ya Wabunge wake hawana sifa za kuwa wawakilishi wa watu.Na wameingia Bungeni kwa Rushwa,mizengwe,wizi wa kura na hata ushirikina.Wabunge wa hivyo siku zote hawajiamini na fikra zao bali wanabaki kusifia mabwana zao na kujipendekeza.
 
Hata baada kumuuwa binadamu mwenzenu bado mnapata ujasiri wa kumtusi?
Hivi ni nani vile alimchinja yule binadamu kule Arumeru baada ya uchaguzi? na Mwigulu alitoa kauri gani vile kuhusiana na yule mwenyekiti wa CCM kulikokutwa siraha za wauaji?
 
Back
Top Bottom