Mjue Laila Ali (The Iron Lady) malkia wa ngumi ulimwenguni

Akilihuru

JF-Expert Member
May 20, 2022
1,444
2,833
Naomba nitoe salam kwa member wenzangu wa JF.

Kwa mara nyingine, leo nawaletea historia ya mwanamasumbwi bora wa kike wa muda wote, na wa uzito wote (The GOAT) Laila Ali au unaweza kumwita 'She bee stingin' ni mtoto wa King wa mchezo huo duniani Muhammad Ali 'The Greatest'.

Laila Ali alizaliwa Dec 30, 1977. Huko Miami beach, Florida nchini Marekani. Pamoja na kusomea mambo ya biashara, kupata shahada mbali mbali na kumiliki baadhi ya biashara zake mwenyewe including kuanzisha kituo cha TV, kumiliki saluni nk.

Kama wasemavyo waswahili kuwa mtoto wa simba ni simba au maji hufuata mkondo, Laila alijikuta anaingia katika mchezo wa ngumi na kujizolea ushindi mkubwa katika mchezo huo wa pili kwa mashabiki duniani kama ilivyokuwa kwa baba yake Muhammad Ali. Alijiunga rasmi na mchezo huo mwaka 1999 na kustaafu mwaka 2007.

Katika historia yake ya miaka 8 katika mchezo huo, aliingia ulingoni kupigana mapambano 24 na mabondia tofauti tofauti. Na katika mechi zote hajawahi kupigwa hata moja.

Ameshinda mapambano 24.

Kati ya hayo mapambano 24, mapambano 21 alishinda kwa KO, na matatu kwa ushindi wa point, huku akiwa amewaacha wapinzani wake katika hali mbaya ya kipigo kikali kutoka kwake. Alistaafu huku chama cha mchezo huo kikiwa bado kinamuhitaji kutokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao katika mchezo huo.

Huyo ndio Laila Ali aka She bee stingin, Pretty baby au Madame Butterfly ambae alikuwa kipenzi kikubwa cha baba yake Mohammad Ali.

Hapo chini nitaweka picha mbali mbali za ushindi wake


images (13).jpeg


Laila Ali baada ya ushindi akiwa na baba yake mzazi ambae pia ndio King wa mchezo wa ngumi duniani Mohammad Ali (The Greatest)
images (14).jpeg


Laila akiwa tena na baba yake Muhammad Ali, baada ya ushindi.
laila-ali-muhammad-ali-death.jpg


Laila Ali akiwasulubu wapinzani wake kisawa sawa.
images (12).jpeg
images (7).jpeg
images (10).jpeg


Laila akiwa na tuzo zake
images (9).jpeg


Enzi za baba yake Muhammad Ali
images.jpeg
 
Jackie Frazier alipigwa kama mtoto na Laila. Hivyo Laila ndio malkia na hajawahi kupigwa na bondia yoyote toka aanze ngumi mpaka anastaafu.
Acha utani mkuu hiyo mechi ilikuwa draw Laila alipewa ushindi wa point kwa heshima tu lakini hakumpiga Wakili msomi Jackie Frazier ambae wakati wa pambano alikuwa na miaka 39 huku Laila akiwa na miaka 23/24.
 
Acha utani mkuu hiyo mechi ilikuwa draw Laila alipewa ushindi wa point kwa heshima tu lakini hakumpiga Wakili msomi Jackie Frazier ambae wakati wa pambano alikuwa na miaka 39 huku Laila akiwa na miaka 23/24.
Mkuu tuongee tu ukweli sio kwa sababu mtu umeamua kuwa opinion wa upande fulan. Mechi inaonesha wazi kuwa Jackie alipigwa katika pambano kuanzia mwanzo hadi mwisho. Katika boxer hakunaga cha ushindi wa hovyo hovyo eti kwa sababu ya heshima.

Maana kama heshima wote wazazi wao walikuwa na heshima katika mchezo huo.
 

Attachments

  • Screenshot_20240228-212431.jpg
    Screenshot_20240228-212431.jpg
    472.9 KB · Views: 1
  • images (15).jpeg
    images (15).jpeg
    28.2 KB · Views: 1
  • images (8).jpeg
    images (8).jpeg
    47.4 KB · Views: 1
Mapambano 24 tuu.. mbona machache ivo
Alipigana kwa miaka 8 tu akaamua kustaafu kutokana na umri, pia alikuwa amesomea mambo mengine ya kibiashara hivyo akaamua kujikita katika biashara zake. Huku akiwa hajawahi kulishwa udongo hata siku 1
 
Mkuu tuongee tu ukweli sio kwa sababu mtu umeamua kuwa opinion wa upande fulan. Mechi inaonesha wazi kuwa Jackie alipigwa katika pambano kuanzia mwanzo hadi mwisho. Katika boxer hakunaga cha ushindi wa hovyo hovyo eti kwa sababu ya heshima.

Maana kama heshima wote wazazi wao walikuwa na heshima katika mchezo huo.
Hilo pambano lipo You Tube bana mkuu na.kila mtaalamu wa ngumi anasema it was a draw. Hata mtangazaji kuna muda anasema " This is not a fight that Laila want to fight "

Laila alidhibitiwa sana that day. Jackie Frazier fighting skills are unmatched.

Laila Ali alipewa ushindi kwa upendeleo maalumu kwa sababu tu ya kulinda brand yake ( she was only 23 and Jackie was 39)

Jackie Frazier kaanza kupigana.ngumi akiwa na.miaka.38..it was more of just fun for her. Alikuwa mwanamichezo anaependa michezo mbalimbali . Aliamua kuingia kwenye boxing just for fun. Wakati anapigana na Laila hiyo mwaka 2001 Jackie Frazier alikuwa judge huko nchini Marekani. So unaweza kuona kwanini referees waliamua kumpa Laila.ushindi. it was better for them to.protect Laila's brand kwa sababu Laila alikuwa bado anapigana na industry ilikuwa bado inamuhitaji. Yeye alikuwa ndio nembo ya boxing kwa wanawake at that time.

Hata ingekuwa wewe ndio judge. Pambano limeisha round zote bila KO. Umpe ushindi huyu career boxer mwenye umri wa miaka.23 ambae bado ana miaka.mingi ya kuendelea kupigana na kuuinua zaidi mchezo wa boxing plus ili uendelee kuikuza brand yake na mchezo wa boxing kwa.ujumla au umpe huyu judge mwenye miaka 39 ambae anapigana as her part time job? Unapaswa kuzitambua siasa za boxing.

Ni kama ilivyo tokea kwa Evander vs George Foreman mwaka.91, hapo Evander ndjo bondia wangu bora wa wakati wote lakini kwenye hiyo.mechi.alipewa ushindi wa heshima.


Kwenye boxing maamuzi ya judges kwenye pambano lililoisha round zote mara zote huwa discretional
 
Hilo pambano lipo You Tube bana mkuu na.kila mtaalamu wa ngumi anasema it was a draw. Hata mtangazaji kuna muda anasema " This is not a fight that Laila want to fight "

Laila alidhibitiwa sana that day. Jackie Frazier fighting skills are unmatched.

Laila Ali alipewa ushindi kwa upendeleo maalumu kwa sababu tu ya kulinda brand yake ( she was only 23 and Jackie was 39)

Jackie Frazier kaanza kupigana.ngumi akiwa na.miaka.38..it was more of just fun for her. Alikuwa mwanamichezo anaependa michezo mbalimbali . Aliamua kuingia kwenye boxing just for fun. Wakati anapigana na Laila hiyo mwaka 2001 Jackie Frazier alikuwa judge huko nchini Marekani. So unaweza kuona kwanini referees waliamua kumpa Laila.ushindi. it was better for them to.protect Laila's brand kwa sababu Laila alikuwa bado anapigana na industry ilikuwa bado inamuhitaji. Yeye alikuwa ndio nembo ya boxing kwa wanawake at that time.

Hata ingekuwa wewe ndio judge. Pambano limeisha round zote bila KO. Umpe ushindi huyu career boxer mwenye umri wa miaka.23 ambae bado ana miaka.mingi ya kuendelea kupigana na kuuinua zaidi mchezo wa boxing plus ili uendelee kuikuza brand yake na mchezo wa boxing kwa.ujumla au umpe huyu judge mwenye miaka 39 ambae anapigana as her part time job? Unapaswa kuzitambua siasa za boxing.

Ni kama ilivyo tokea kwa Evander vs George Foreman mwaka.91, hapo Evander ndjo bondia wangu bora wa wakati wote lakini kwenye hiyo.mechi.alipewa ushindi wa heshima.


Kwenye boxing maamuzi ya judges kwenye pambano lililoisha round zote mara zote huwa discretional
😀😀 Haya banah, hii comment yako inanikumbusha story fulan ya zamani eti Zanzibar ilicheza na Tanzania bara, sasa mechi ilichezewa Zanzibar kwenyewe hivyo wenyeji walikuwa na uwezo wa kutufunga kutokana na kuonesha kuudhibiti mchezo kwa chenga kali na vionjo vya hapa na pale. Cha kushangaza Zanzibar ilikuwa hata ikifinga katika lango letu hawapigi shuti golini, wao wanarudisha tena katikati ya uwanja chenga zinaendelea.

Kuja kutaamaki mechi imeisha tumewapiga goli tatu bila. Wanahojiwa sababu ya kufungwa kwao, na wakati mchezo waliumiliki wao, kauli yao ikawa "yakhe kutufunga kweli mwatufunga, lakini na sie chenga twawalaa" 😀😀😀
 
Back
Top Bottom