KXY
JF-Expert Member
- Dec 31, 2011
- 880
- 327
Nawasalimu wakuu!
Wana jamvi naomba tusaidiane mawazo na tuelimishane kuhusu huu mjadala, kipi ni kipi, kiongozi ni mwakilishi, mwakilishi ni kiongozi au yote majibu/si majibu?
Ili kupata mwanga ni vizuri kujua maana ya haya maneno, samahani nitatumia tafsiri zake za kiingereza ili niweze kunukuu(nimekosa kamusi pepe/softcopy)
lead·er
noun
1. a person or thing that leads.
2. a guiding or directing head, as of an army, movement, or political group.
rep·re·sent·a·tive
noun
1. a person or thing that represents another or others.
2. an agent or deputy: a legal representative.
3. a person who represents a constituency or community in a legislative body..
Kutokana na maana hizo hapo juu(kwa uelewa wangu), kiongozi ni mtoa muongozo na uongozi wake utatumia utashi wake zaidi anaweza kuwashirikisha au asiwashirikishe katika maamuzi anayochukua kikubwa awe na ushawishi kwa kundi lake.
Tukija kwa mwakilishi huyu jukumu lake kubwa ni kuwakilisha waliomtuma na sio kufanya kile anachofikiria yeye, ukifikiria kiundani zaidi dhana ya uwakilishi ni vyema anayewakilisha akiwa na maono sawa na anaowawakilisha ili aweze kuamini katika anachokipigania.
Kutoa mfano wa maana hizo hapo juu, Mh Mbowe ni kiongozi wa chama chake na ni mwakilishi wa jimbo lake kama mbunge.
Kuna mwanafilosofia mmoja wa karne ya 18 Edmund Burke alitoa kauli iliyoleta utata kuhusu uwakilishi, alisema;
A representative owes the People not only his industry, but his judgment, and he betrays them if he sacrifices it to their opinion.
Kwa maelezo ya huju jamaa ni kwamba mwakilishi anatakiwa asimamie maamuzi yake hata kama yatapingana na maoni ya anaowawakilisha. Huu ni uwakilishi au ni uongozi?
Nimeweka hii mada jamvini ili tuweze kufahamu nani ni nani katika jamii yetu na ana majukumu gani. Tukiweza kujua yupi ni kiongozi na yupi ni mwakilishi na tukijua maana ya hizo nafasi tunaweza kutambua mjumbe, mbunge, waziri na wengineo wanatakiwa watufanyie nini.
Naomba mchango wenu wadau, tunaweza kuwatumia hawa na wengine kama mifano, wabunge, mawaziri, madiwani, Rais.
Nawasilisha,
KXY.
Wana jamvi naomba tusaidiane mawazo na tuelimishane kuhusu huu mjadala, kipi ni kipi, kiongozi ni mwakilishi, mwakilishi ni kiongozi au yote majibu/si majibu?
Ili kupata mwanga ni vizuri kujua maana ya haya maneno, samahani nitatumia tafsiri zake za kiingereza ili niweze kunukuu(nimekosa kamusi pepe/softcopy)
lead·er
noun
1. a person or thing that leads.
2. a guiding or directing head, as of an army, movement, or political group.
rep·re·sent·a·tive
noun
1. a person or thing that represents another or others.
2. an agent or deputy: a legal representative.
3. a person who represents a constituency or community in a legislative body..
Kutokana na maana hizo hapo juu(kwa uelewa wangu), kiongozi ni mtoa muongozo na uongozi wake utatumia utashi wake zaidi anaweza kuwashirikisha au asiwashirikishe katika maamuzi anayochukua kikubwa awe na ushawishi kwa kundi lake.
Tukija kwa mwakilishi huyu jukumu lake kubwa ni kuwakilisha waliomtuma na sio kufanya kile anachofikiria yeye, ukifikiria kiundani zaidi dhana ya uwakilishi ni vyema anayewakilisha akiwa na maono sawa na anaowawakilisha ili aweze kuamini katika anachokipigania.
Kutoa mfano wa maana hizo hapo juu, Mh Mbowe ni kiongozi wa chama chake na ni mwakilishi wa jimbo lake kama mbunge.
Kuna mwanafilosofia mmoja wa karne ya 18 Edmund Burke alitoa kauli iliyoleta utata kuhusu uwakilishi, alisema;
A representative owes the People not only his industry, but his judgment, and he betrays them if he sacrifices it to their opinion.
Kwa maelezo ya huju jamaa ni kwamba mwakilishi anatakiwa asimamie maamuzi yake hata kama yatapingana na maoni ya anaowawakilisha. Huu ni uwakilishi au ni uongozi?
Nimeweka hii mada jamvini ili tuweze kufahamu nani ni nani katika jamii yetu na ana majukumu gani. Tukiweza kujua yupi ni kiongozi na yupi ni mwakilishi na tukijua maana ya hizo nafasi tunaweza kutambua mjumbe, mbunge, waziri na wengineo wanatakiwa watufanyie nini.
Naomba mchango wenu wadau, tunaweza kuwatumia hawa na wengine kama mifano, wabunge, mawaziri, madiwani, Rais.
Nawasilisha,
KXY.