Mistari ya JK: hivi hii mmeishaiona?

Ms Judith

JF-Expert Member
Dec 24, 2010
2,563
918
Swali: Mheshimiwa Rais je unawajua wamiliki wa kampuni ya Dowans?


Jibu:
Nasema mimi sijui, ni kina nani sijui,
Wanatoka wapi sijui, walifikaje sijui,
Kama nawafahamu sijui, kama wananijua sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Mheshimiwa Rais, lakini waliingia nchini na kupata Mkataba wa Richmond na kuleta majenereta katika kutekeleza mpango wako wa kupunguza tatizo la umeme nchini kweli huwajui?


Jibu:
Nasema mimi sijui!, kwanini walikuja sijui,
Uhusiano wao siujui, Kama nao Richmond sijui,
Waliingia kwa lipi sijui, na walirithishana vipi sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Lakini ulisema kuwa Richmond ni kampuni Hewa kama Kamati ya Mwakyembe ilivyoonesha na kudai, na ukatoa pongezi! Unawaeleza vipi Watanzania kuwa Taifa liko tayari kuheshimu mkataba wa kampuni ya kitapeli?


Jibu:
Nasema tena sijui!Kama kampuni hewa sijui,
Kama ni matapeli sijui, Kama walibebwa sijui,
Wahusika kina nani sijui, Mwakyembe alijuaje sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!




Tulikoanzia sijui, tumefika vipi sijui,
Nahusika vipi sijui, nimuulize nani sijui,
Niwaridhishe vipi sijui, nianzie wapi sijui!
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Lakini Rostam Aziz ametajwa kuhusika kuanzia mwanzo wa sakata hili na yeye mwenye amekiri kuhusika na hili kwanini usimuulize ili ujue?


Jibu:


Nitamuanza vipi sijui, Rostam huyu sijui,
Kama mwingine sijui, anahusika vipi sijui
Nimuamini nani sijui, kama ni kweli sijui!
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Lakini, inawezekana vipi usijue wakati una vyombo vingi vya usalama ambavyo vingeweza kukupata taarifa mbalimbali za kiinteligensia kama walivyoweza kuzipata kule Arusha na kuvunja maandamano ya Chadema? Kwanini hujapatiwa taarifa za kiinteligensia kuhusu Dowans?


Jibu:


Intelligensia mimi sijui, nani anipe sijui,
Kwanini wanipe sijui, nifanye nayo nini sijui,
Wasiponipa sijui, kama nadaganywa sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Nani awaagize sijui, kama nini mimi sijui,
Au makamu sijui, Waziri Mkuu sijui,
Wajitolee tu sijui, au ni Bunge mimi sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Sasa msimamo wako wewe binafsi kama Rais ni upi, Dowans walipwe au wasilipwe?


Jibu:


Msimamo gani sijui! Kama ninao sijui,
Nilikuwa nao sijui, nitakuwa nao sijui,
Kama walipwe sijui, na wasilipwe sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Wizara ilipe sijui, Au Tanesco sijui,
Au huko hazina sijui, au hapa Ikulu sijui,
Bunge litenge fedha sijui, au Mahakama sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Sasa mheshimiwa inaonekana hujui mambo mengi tu; kuna mambo mengine yoyote unayoyajua?


Jibu:
Kwanini masikini sijui, Kagoda ni nani sijui,
Meremeta nani sijui, Dipu Grini nani sijui,
Mbona elimu duni sijui, wanagomea nini sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Sijui mimi sijui, mengine mengi sijui,
Ya kilimo siyajui, ya Sayansi siyajui,
Mambo ya maji sijui, umeme ndiyo sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!




Kama napendwa sijui, kama nachukiwa sijui,
Nafurahiwa sijui, au nakejeliwa sijui,
Kama ninachekewa sijui, au nakebehiwa sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Mheshimiwa swali la mwisho; asante sana kwa kutupa nafasi hii na kwa hakika umetuelewesha na tumeelewa kuwa hujui mambo mengi sana. Labda uwaambie Watanzania, je wewe ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?


Jibu:


Sijui mimi sijui, ninarudia sijui,
Kama miye sijijui, mtajuaje sijui
Kama najua sijui, kama sijui sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji -BGM)
 
MM alisahau hii, KWANINI SISI NCHI MASKINI SIJUI, INGAWA TUNA MADINI SIJUI,NA MBUGA ZA WANYAMA SIJUI,MLIMA KILIMANJARO SIJUI,NASEMA TENA SIJUI...LOL,
 
nilikuwa nimekasirika lakini kwa hii siku imekwisha vizuri kwa kicheko, asanteni wana jf
 
HApa Mwanangu Museveni haoni ndani, mistari anashuka, Hii singo inatoka lini kama mmefuatilia kwa karibu?
 
Jioni yangu imekuwa njema kwa hizi rylics.Na huo ndio upeo wake kweli wala sio utani.
 
MM alisahau hii, KWANINI SISI NCHI MASKINI SIJUI, INGAWA TUNA MADINI SIJUI,NA MBUGA ZA WANYAMA SIJUI,MLIMA KILIMANJARO SIJUI,NASEMA TENA SIJUI...LOL,

Napia alisahau kuuliza kwa nini anasafari nyingi zisizoisha nchi za nje

Kama nasafiri sijui, naenda wapi sijui
Naenda kubembea jamaika sijui, mimi ni mtalii sijui
Marekani mimi sikujui, Obama simjui
Safari zina tija sijui, natangaza njaa sijui
 
Maisha bora kwa mtz,sijui. Kama nlihadi sijui,kama nlihaidi mgao wa umeme sijui. Kama majenereta ya Ali alidaiwi yamezimwa sijui,kama yamewashwa sijui. Na cdm wanikera sijui,kama nahandaa hotuba ya kuikimbia ikulu sijui,na lini sijui. Wananchi hawanitaki sijui,kama ntamwachia kiti makamba Jr. Sijui au Riz1 sijui. Mh. Mtangazaji anayenihoji,nawe sikujui. Kusema kwa heri sijui. Mh mtangazaji mimi sijui,nasema yote sijui. Sijui kwa kuwa sijui. Sijui mimi sijui.
 
dah,sijui kama sijui,....hahahaha na watanzania wengi hawajui kama wana raisi ambaye hajui
 
Aaah aaah am happy now I was furious on the way our prime minister is doing things but these lyrics have made my day ...-lol
 
Swali: Mheshimiwa Rais je unawajua wamiliki wa kampuni ya Dowans?


Jibu:
Nasema mimi sijui, ni kina nani sijui,
Wanatoka wapi sijui, walifikaje sijui,
Kama nawafahamu sijui, kama wananijua sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Mheshimiwa Rais, lakini waliingia nchini na kupata Mkataba wa Richmond na kuleta majenereta katika kutekeleza mpango wako wa kupunguza tatizo la umeme nchini kweli huwajui?


Jibu:
Nasema mimi sijui!, kwanini walikuja sijui,
Uhusiano wao siujui, Kama nao Richmond sijui,
Waliingia kwa lipi sijui, na walirithishana vipi sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Lakini ulisema kuwa Richmond ni kampuni Hewa kama Kamati ya Mwakyembe ilivyoonesha na kudai, na ukatoa pongezi! Unawaeleza vipi Watanzania kuwa Taifa liko tayari kuheshimu mkataba wa kampuni ya kitapeli?


Jibu:
Nasema tena sijui!Kama kampuni hewa sijui,
Kama ni matapeli sijui, Kama walibebwa sijui,
Wahusika kina nani sijui, Mwakyembe alijuaje sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!




Tulikoanzia sijui, tumefika vipi sijui,
Nahusika vipi sijui, nimuulize nani sijui,
Niwaridhishe vipi sijui, nianzie wapi sijui!
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Lakini Rostam Aziz ametajwa kuhusika kuanzia mwanzo wa sakata hili na yeye mwenye amekiri kuhusika na hili kwanini usimuulize ili ujue?


Jibu:


Nitamuanza vipi sijui, Rostam huyu sijui,
Kama mwingine sijui, anahusika vipi sijui
Nimuamini nani sijui, kama ni kweli sijui!
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Lakini, inawezekana vipi usijue wakati una vyombo vingi vya usalama ambavyo vingeweza kukupata taarifa mbalimbali za kiinteligensia kama walivyoweza kuzipata kule Arusha na kuvunja maandamano ya Chadema? Kwanini hujapatiwa taarifa za kiinteligensia kuhusu Dowans?


Jibu:


Intelligensia mimi sijui, nani anipe sijui,
Kwanini wanipe sijui, nifanye nayo nini sijui,
Wasiponipa sijui, kama nadaganywa sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Nani awaagize sijui, kama nini mimi sijui,
Au makamu sijui, Waziri Mkuu sijui,
Wajitolee tu sijui, au ni Bunge mimi sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Sasa msimamo wako wewe binafsi kama Rais ni upi, Dowans walipwe au wasilipwe?


Jibu:


Msimamo gani sijui! Kama ninao sijui,
Nilikuwa nao sijui, nitakuwa nao sijui,
Kama walipwe sijui, na wasilipwe sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Wizara ilipe sijui, Au Tanesco sijui,
Au huko hazina sijui, au hapa Ikulu sijui,
Bunge litenge fedha sijui, au Mahakama sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Sasa mheshimiwa inaonekana hujui mambo mengi tu; kuna mambo mengine yoyote unayoyajua?


Jibu:
Kwanini masikini sijui, Kagoda ni nani sijui,
Meremeta nani sijui, Dipu Grini nani sijui,
Mbona elimu duni sijui, wanagomea nini sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Sijui mimi sijui, mengine mengi sijui,
Ya kilimo siyajui, ya Sayansi siyajui,
Mambo ya maji sijui, umeme ndiyo sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!




Kama napendwa sijui, kama nachukiwa sijui,
Nafurahiwa sijui, au nakejeliwa sijui,
Kama ninachekewa sijui, au nakebehiwa sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Mheshimiwa swali la mwisho; asante sana kwa kutupa nafasi hii na kwa hakika umetuelewesha na tumeelewa kuwa hujui mambo mengi sana. Labda uwaambie Watanzania, je wewe ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?


Jibu:


Sijui mimi sijui, ninarudia sijui,
Kama miye sijijui, mtajuaje sijui
Kama najua sijui, kama sijui sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji -BGM)

Mwanakijiji.
Ingia studio bwana. Mistari imetulia sana hiyo na uhakika utauza hiyo singo kwa mamilioni ya pesa.
Tehetehete !!!
 
Chorus-sitaki nijue kama mimi "sijui" unauliza "sijui" kitugani "sijui" mwandishi "sijui" karibu tena"siiijuuuiiiiii"
 
Ngojeni tu... naona hii ni mara ya tatu hii mistari inazungushwa tena.. the first time mojawapo ya hizi kazi imeonekana kuvutiwa na watu. Shukrani!!
 
Chorus-sitaki nijue kama mimi "sijui" unauliza "sijui" kitugani "sijui" mwandishi "sijui" karibu tena"siiijuuuiiiiii"
 
Chorus-sitaki nijue kama mimi "sijui" unauliza "sijui" kitugani "sijui" mwandishi "sijui" karibu tena"siiijuuuiiiiii"
 
PHP:
My body belongs to God, I am just holding it in TRUST

I JESUS CHRIST we trust...............................................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom