Mimba imemfanya amtoroke mumewe

BASHADA

JF-Expert Member
Jul 13, 2011
513
148
Wana JF, heshima mbele.

Nina rafiki yangu wa karibu mno kiasi cha kuitana ndugu. Alifunga ndoa mwaka jana october. Mwisho wa mwezi December mkewe akapata ujauzito. Kazini kwake ni Mikoani lakini yuko Dar kimasomo. Jamaa anasoma masters na mrs ni graduate and degree moja.
Mwezi november alienda kazini kwake akiwa anashughulikia ujenzi wa nyumba yake ambayo sasa anapaua, akakaa mpaka january.
Hakupanga chumba ila akawa amefikia kwa rafiki yake wa karibu sana ambaye ana nyumba kubwa ambako muda wote amekuwa akifikia hapo, tangia aende masomoni, ukizingatia kuwa wakati wa kwenda shule alirudisha nyumba aliyokuwa amepanga.

Tatizo lake, mkewe tangu apate mimba hataki kumwona wala kusikia sauti yake. She just hate him. Hivi majuzi mkewe alipangiwa kutuo cha kazi hapo hapo ambapo ni karibu na kazini kwa jamaa, baada ya jamaa kuhangaikia ili awe karibu na mkewe. Kwa kuwa alikuwa Dar, akamuomba huyo rafiki yake kuwa mkewe aendelee kukaa kwake kwa muda wakati anamalizia finishing ya nyumba yake. Jamaa akamkubalia na huyo mwanamke akaja. Ikawa jamaa akimpigia simu mwanamke hapokei, msg hajibu, akitumiwa hela hata hasemi kama amepata na hakuna kumshukuru kwa jinsi amavyomjali sana.

To make story short, wakakaa siku nne hakuna mawasiliano, jamaa akaamua kumtafuta huyo mwenye nyumba ili amfikishie ujumbe. Siku iliyofuata, binti akachukua taxi akachukua kilicho chake akakomba kila kitu akaondoka wakati mwenye nyumba hayupo, akaaga kwa majirani kuwa anaenda kuripoti kazini then anasafiri. Mumewe alipoanza kumtafuta mwenye nyumba akatoa ripoti kamili, jamaa akapigwa na butwaa. Kumbe huyo mwanamke hakusafiri wala nini, ni kwamba alipanga chumba sehemu nyingine. Jamaa alipoona hivyo, akapanda gari kuja kushuhudia kilichotokea, wakanza kumtafuta binti next day wakisaidiana na mwenye nyumba huyo, binti alivyogundua kuwa mumewe kaja, yeye akapanda gari kwenda Dar, wakati jamaa yuko mkoani.
Jamaa yangu huyu amechanganyikiwa wadau nimsaidieje?
 
Labda mimba sio yake na mke hana tu ujasiri wa kumwambia/kuomba talaka.

Wenye ndoa mna kazi kweli!!
 
mimba nyingine balaa, hata mumeo hutaki kumuona, unaona kero yaani ukimtia machoni tu nafsi inachafuka...
 
Sioni ajabu mwanamke kama yuko kwenye mimnba anaweza kufanya lolote.
 
hata kama ni mimba,lakini huyu m.ke amezidi.au labda kuna kisa kingine.ndio unaweza uka behave tofauti,lakini hee anayofanya huyu m.ke ni over the top.bora huyo mume,amsubiri mpaka atakapojifungua
 
Huyo ana afadhali, nina shemegi yangu huyo anatuma kama muhindi! Istoshe hachagui amtume nani atakae katiza ndo huyo huyo. Chamsingi mwambie avumilie ndivyo mimba zilivyo.
 
avumilie tu mana mimba zina vituko sana, mie rafiki yangu alikuwa anapenda miguu ya kuku kila siku mumewe lazima arudi na miguu ya kuku asiporudi nayo ni balaa mpaka mumewe akaitafute ampatie na roho itulie, so avumilie tu.
 
Mtasingizia na mimba sasa,hata kupokea simu?haya mimba haimtaki mumewe na huyo shemeji je,alishindwa nini kumuaga?am not buying this..
 
Jamani acheni kumdanganya huyu jamaa,hiyo mimba sio yake na hakuna mke hapo. Mpaka mtu ukapange bado mnasema mimba?? kuna kitu anaficha huyo mwanamke...labda anaogopa kuzaa mzungu....hahhh
 
Anachotakiwa ni kukaa chini na huyo mkewe ili waliongelee, mwanamke anatakiwa aweke wazi namna anavyojisikia. Inawezekana kukawa na jambo ila mwanamke anatumia ujauzito wake km kinga.
 
hayo mambo ya mbadala si sahihi haiwezekani mimba ikahusishwa na masuala ya simu hata salam ni tabia na utukutu wa mtu ..

huyo jamaa mwambie asihangaike wala nini akae atulie aendelee na ratiba zake za kila siku
 
isije kuwa mwanamke alitaka sherehe maana siku hizi kuna ndoa za sherehe (muonekano)
 
Ushauri wa bure jamaa akapime viungo vya uzazi kama vinaweza kutungisha mimba.
Akikuta safi basi mimba changa hiyo inamkataa mmewe
 
Chakufanya apige kimya hakuna kumtafuta wala kumtumia hela ndo atatia akili manake ukionyesha sana mapenzi ndo madhara yake haya.Amwache angaike yeye mwenyewe atarudi.Atakuja kujua upumbafu anao fanya baadae.Kujiendekeza tu eti mimba inamchukia ni upumbafu tu tuliojijengea vichwani pambaf angenifanyia mimi mbona angejuta
 
Asanteni kwa ushauri, lakini kuna wadau hapa wamechangia kuwa wakae waongee, mii nadhani hawajaelewa mada. Ni kwamba Hataki hata kumwona, hapokei simu, na akishajua kuwa jamaa kaja yeye anasafiri sasa wataonanaje? Inanitia huruma because jamaa amekuja na anakesha usiku anaomba (anasali) na analia mpaka tunakosa raha sisi wenyewe. Jamaa anampenda sana mke wake mpaka nahisi it is a deep love, kitu ambacho kwa mkewe hakipo. Ukiwa pembeni unaweza kuchukulia simple lakini ikiwa ndo wewe, sijui itakuwaje.
 
Asanteni kwa ushauri, lakini kuna wadau hapa wamechangia kuwa wakae waongee, mii nadhani hawajaelewa mada. Ni kwamba Hataki hata kumwona, hapokei simu, na akishajua kuwa jamaa kaja yeye anasafiri sasa wataonanaje? Inanitia huruma because jamaa amekuja na anakesha usiku anaomba (anasali) na analia mpaka tunakosa raha sisi wenyewe. Jamaa anampenda sana mke wake mpaka nahisi it is a deep love, kitu ambacho kwa mkewe hakipo. Ukiwa pembeni unaweza kuchukulia simple lakini ikiwa ndo wewe, sijui itakuwaje.

hahitaji kutumia nguvu wala ninini.. mwambie akae chini atulizane hahitaji kufanya papara kwani afanyalo mwenza wake ni makusudi na anaelewa afanyalo .. yeye akae chini atulizane japo hata kwa week chache zijazo . kwani mwenza yawezekana ana jambo ambalo anataka kulifanya au amedhamiria kulifanya , maana ndoa bado mbich sana na haijaweza walau kufika miez 6 , asikurupuke atulie asome mchezo
 
Sina uhakika sana kama mimba kwa asilimia kubwa huchangia matatizo kama hayo ila kinachoonekana hapo ni kwamba MIFUMO YA MISINGI YA KIMAPENZI INA ULAKINI.Kuna elements nyingi sana za kuchukuliana rahisi rahisi baina yao.Hili ni tatizo ambalo si tu hujitokeza pale ujauzito unapokuwepo ila hata ktk mambo mbalimbali ya maisha yenu.Wanaume wengi hukosea hapo wanapoanzisha mahusiano mwishowe hupelekea matatizo mengi(ie dharau,kujisahau,kujiamini kupitiliza na kusikokua na msingi) kufumuka toka kwa mwanamke.Kwa lugha nyepesi mahusiano haya nayaita 'legelege'.Ukianzisha mahusiano ya namna hii matatizo ya kimapenzi utakuwa ukitembea nayo kila uendako.
Kitu cha kufanya kwa huyo rafikiyo.
Aangalie upya ujenzi wa misingi ya mahusiano yake na yeye anatakaje,ataisimamiaje na atafanikiwaje kuepuka na matatizo YASIYO YA LAZIMA.Its difficult kumshauri afanye a,b,c...kwa sababu am don't know charachers zake and his geniun.The way unavyoplan,the way unavyosimamia what you planned ndivyo outcome itakavyokuwa.
 
Back
Top Bottom