Mil. 90 Zinahitajika kuokoa Uhai wa Dr. Ulimboka

Mi nadhani wakati watanzania wanachangia, Madaktari waendelee kuwahudumia wagonjwa wanaoweza kutibiwa hapa hapa nchini haitakuwa kitu cha msingi watanzania wakahangaika na mtu mmoja wakati Mamia ya Wagonjwa wanakufa mahospitalini.

Halafu ni kweli Madaktari wanalamika dawa hakuna hospitali au ni pendekezo lao la kulipwa Mshahara wa Milioni 3.5 kwa mwezi, katika hili nawaelaza Madaktari wafanye analysis waje na data kama inawezekana ila
Prof analipwa 2.5M ambaye anamfundisha Daktari.

Mbunge 2.5M. Nakushauri kaombe Salar slip ya Mbunge wako wa Jimbo atakupa
Hlafu 60% ya Madai yametekelezwa hata lile mlilotaka kukopeshwa Magari, Posho kuongezwa yametekelezwa, na Mashine mliyokuwa mnahitaji Itengenezwe Wataalam wanakuja kutoka kule mashine ilikokuwa imetengenezwa, Mlikuwa hammtaki waziri ametotolewa ten pamoja na Katibu Mkuu ndugu Blandin Nyoni waelezeni watanzania Ukweli wa Madai yenu kupitia vyombo vya Habari kwa sababu watanzania ndio waajiri wenu Mnalipwa mishahara kodi za Watanzania.
 
Prof analipwa 2.5 ambaye anamfundisha Daktari
Mbunge 2.5..

Nikuchukulia kuwa hizo figure zako ni sahihi, sasa shida iko wapi kama Daktari anayefanya kazi usiku na mchana, anayeweza akaitwa hata wakati yupo katika kutafuta mtoto kwenda kusaidia mtu mmoja apone kuwazidi mishahara hao uliowataja? unadhani wewe kuwa hao ndio watu muhimu sana kwenye jamii yetu wanaopaswa kuwa na mishara ambayo haiwezi kuzidiwa na mshahara wa mfanyakazi wa sekta nyingine yoyote? Pia Angalia mbunge allowance alizowekewa?? Hat hivyo suala la mishahara sio issue we can always Negotiate, issue ni mazingira ya Hospitali zetu mkuu. Unasemaje kuhusu hilo??
 
Vp kuhusu namba za akaunti wekeni wazi kama mmejitolea tumsaidie huyu ndugu yetu .
 
Polisi mmoja wa kikosi cha FFU ameuliwa wakati wengine kadhaa wamejeruhiwa vibaya leo na raia wenye hasira maeneo ya Tegeta Namanga. Pamoja na skari, kuna raia wawili pila waliouliwa na askari hao wa FFU huku wengine wengi wakiwa wameumizwa vibaya. Hii ilitokea kwenye purukushani iliyoanzhishwa na mmiliki wa kituo cha mafuta aliyeanza kuvunja makazi ya wananchi hao.

Yawezekana wengi wamepoteza maisha yao, ila kwa macho yangu nimemuona Askari mmoja kauliwa na Wananchi wawili ila walioumia ni wengi sana. Hali ilikuwa ni mbaya sijawahi kuona. Nimeona ile kwenye TV. Nilijua tu vitu kama vile vinatokea Afghanistan, Syria na Iraq siyo Tanzania. Mbaya zaidi rais mwenye kapita na kuacha mapambano yakiendelea

Mapambano kati ya polisi na raia yameendelea kwa muda mrefu hata baada ya rais kupita, ambako pia gari la rais na msafara mzima lilirushiwa mawe.....Inabidi polisi waseme ukweli kuhusiana na hili jambo.. hali bado tete kwani wananchi wana hasira na serikali kuruhusu mwekezaji huyu kujichukulia sheria mikononi mwake ya kuwahamisha na kuvunja makazi yao

Chanzo, nilikuwepo eneo la tukio
 
"serikali kwa unafiki wao walijipendekeza eti wapo tayari kugharimia matibabu ya dr. Ulimboka, madaktari wamegoma kuwa hawawezi kupokea fedha kutoka kwa yuda eskarioti"
nipo tayari kuchangia pesa.nitawaambia wadau wenzangu huku usa.tutakuwa na mkutano kesho,vijana wote hapa washington dc.tusipokea pesa kutoka serikalini hatutaki tunaweza sisi wenyewe kumpeleka nje.tunawapongeza kwanza kwa kutomruhusu huyu vasco da gama kutokuja hapo hosptal asanteni sana.ulinzi muhumi.alafu tunaomba kama dr ulimboka anaweza kuongea chukueni data kwa video ,na audio ili tuwe na data kamili.tunaomba apone haraka sana.
 
NDIO mkuu. Inaonekana majeruhi yake ya ndani ni makubwa sana, LABDA itahitajika kubadirisha Ini kabisa?? LAKINI kwa Dr. Ulimboka ni muhimu aokolewe kwa gharama yoyote ile, kwani ataweza kusaidia kuleta ukweli wa mambo. Pia hii itakuwa ndio mwanzo wa kukuzwa Demkrasia ya kuheshimiana mawazo. La Sivyo wakishajua hii njia inasaidia watu wengi watanyamazishwa.

Shukran kwa kunipa ufafanuzi wa kina, tumuombee Mungu apone haraka


Sent from my NOKIA 3310 using Tapatalk HD
 
kama uko jikoni huko serikalini waambie hospitali ya mkoa wa Tanga A.K.A bombo Hospital haina xray....
 
Mi nadhani wakati watanzania wanajiandaa kuanza kuchanga, Madaktari waendelee kuwahudumia wagonjwa wanaoweza kutibiwa hapa hapa nchini haitakuwa kitu cha msingi watanzania wakahangaika na mtu mmmoja wakati Mamia ya Wagonjwa wanakufa mahospitalini
Halafu ni kweli Madaktari wanalamika dawa hakuna hospitali au ni pendekezo lao la kulipwa Mshahara wa Milioni 3.5 kwa mwezi, katika hili nawaelaza Madaktari wafanye analysis waje na data kama inawezekana il
Prof analipwa 2.5 ambaye anamfundisha Daktari
Mbunge 2.5..Nakushauri kaombe Salar slip ya Mbunge wako wa Jimbo atakupa

Watanzania imefika mahali tupime Unga na Mchanga Tuache Ushabiki wa Kisiasa kwenye Maisha ya Watanzania

Mkuu siasa wanaingiza serikali na watendaji wake.. Mnashikilia suala la mishahara mbona hamzungumzii vitendea kazi..? ITV kwenye habari za uciku wameonyesha mgonjwa hospital ya bombo ameshindwa kupiga xray.. Karibu hospital zote Tanga mashine za xray hazifanyi kazi..! Muhimbili Tscan inakufa kila ciku.. Hamsemi hayo..!
 
Napendekeza apelekwe germany,they have very modern technology and expertise,Dr.Ulimboka has to survive by all necessary measures,hima tuchangie..let us not give them the satisfaction that they managed to silence him
 
fREE WORLD Unakanyagwa nini chadema hili sio swala la utani wala siasa. mku....u wako. samahani mode usinibun!
 
Sichangi hata Mia mdogo wangu alipoteza maisha kwa kukosa care ya Madaktari Leo mjinga mmoja achangiwe mil 90? Mwache afe ....!!
 
Sina la kusema ila laana ndani ya mwezi huu mtukufu kwa waliofanya dhambi hii inawatosha! Je wao hawatakaa wafe? Je hawana uhakika wa kukutana na mola wao?, Je ni kweli kuna haja ya kuendelea kuapa kwa msahafu na bibilia?, Je wanadhani Watanzania ni wajinga na hawawezi kufikri?, Je wanadhani kuua mtu mmoja ndo kumaliza matatizo ya nchi hii? Je wataua wangapi? " NAOMBA KWA WANYONGE WOTE WA NCHI HII KUOMBA NA KUFUNGA DHIDI YA DR. ULIMBOKA ILI APONE NA ASEME UKWELI UPATIKANE NA NAOMBA MADAKTARI WAWE MAKINI DHIDI YA UHAI WA MWENZAO KWANI YAWEZEKANA AKAMALIZILIWA UGHAIBUNI KATIKA MATIBABU HAKIKA TUMENYONYWA VYA KUTOSHA NA WAKOLONI WEUSI " Tumwombe Allah atuepushe na balaa (mauaji/kuawa kwa wapigania haki za wanyonge) na atupitishe katika kipindi hiki salama cha migomo ya kila aina. Tumwombwe Allah awaumbue wote walofanya njama hii ili kila mmoja atambue na tumwombe Allah kwa pamoja (wanyonge wote wa nchi hii) awakosanishe walofanya dhambi unyama huu wa umwagaji wa damu ya HAKI ili watajane na waumbuane na mwisho wananchi waamue cha kufanya. AN INJURED TO ONE IS AN INJURED TO EVERY ONE IN THIS COUNTRY
 
Back
Top Bottom