X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
Mikoa mitatu iliyoanzishwa mwaka jana kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa madhumuni ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali ni:
Mkoa wa Njombe ambao unaundwa na wilaya za Njombe, Ludewa na Makete ambazo awali zilikuwa ndani ya Mkoa wa Iringa na wilaya mpya ya Wangingombe sehemu ya iliyokuwa wilaya ya Njombe.
Mkoa wa Geita unaoundwa na Wilaya za Geita (iliyokuwa mkoa wa Mwanza), Bukombe (kutoka Mkoa wa Shinyanga) na Chato (iliyokuwa ya Mkoa wa Kagera). Mkoa huu pia una Wilaya mpya ya Nyanghwale (imetokana na kugawanywa kwa Wilaya ya Geita).
Mkoa wa Simiyu ambao unaundwa na Wilaya za Bariadi, Meatu na Maswa (zilikuwa za Mkoa wa Shinyanga), Wilaya mpya ya Busega (awali ilikuwa mkoani Mwanza na Wilaya ya Itilima (inatokana na kugawanywa kwa iliyokuwa Wilaya ya Bariadi).
Kwa mamlaka aliyopewa, Rais anaweza kuigawa nchi katika mikoa au Wilaya ili kurahisisha na kuongeza ufanisi katika utendaji wa Serikali kuu kwa kupunguza ukubwa wa maeneo ya mikoa mama ili wananchi wapate huduma za kiutawala ngazi ya mikoa kwa karibu.
Mkoa wa Njombe ambao unaundwa na wilaya za Njombe, Ludewa na Makete ambazo awali zilikuwa ndani ya Mkoa wa Iringa na wilaya mpya ya Wangingombe sehemu ya iliyokuwa wilaya ya Njombe.
Mkoa wa Geita unaoundwa na Wilaya za Geita (iliyokuwa mkoa wa Mwanza), Bukombe (kutoka Mkoa wa Shinyanga) na Chato (iliyokuwa ya Mkoa wa Kagera). Mkoa huu pia una Wilaya mpya ya Nyanghwale (imetokana na kugawanywa kwa Wilaya ya Geita).
Mkoa wa Simiyu ambao unaundwa na Wilaya za Bariadi, Meatu na Maswa (zilikuwa za Mkoa wa Shinyanga), Wilaya mpya ya Busega (awali ilikuwa mkoani Mwanza na Wilaya ya Itilima (inatokana na kugawanywa kwa iliyokuwa Wilaya ya Bariadi).
Kwa mamlaka aliyopewa, Rais anaweza kuigawa nchi katika mikoa au Wilaya ili kurahisisha na kuongeza ufanisi katika utendaji wa Serikali kuu kwa kupunguza ukubwa wa maeneo ya mikoa mama ili wananchi wapate huduma za kiutawala ngazi ya mikoa kwa karibu.