Muheshimiwa Rais ni kwanini unasita kuwaeleza ukweli madaktari. Madaktari wa Tanzania hawana skills za kulipwa huo mshahara wanaohitaji, tulitegemea wangemtibu Ulimboka hapa hapa nchini ili kuonyesha mfano hata kwa wanasiasa kwamba wanauwezo wa kutibu badala ya kutumia ma milioni kupeleka wagonjwa nje ya nchi. Ninavyoamini mimi ni kwamba unapokuwa na taaluma fulani na kama unaipenda unaweza kujiendeleza wewe mwenyewe na kuwa competent. Madaktari wamejaa kiburi na wanataka kuonyesha kwamba fani yao ni ya muhimu kuliko fani zingine. serikali inautaratibu wake katika masuala ya ajira. Badala ya kuandamana kuhusu pesa tunataka waandamane kuhusu vifaa wanavyohitaji ili tusiwapeleke watanzania nje ya nchi kwa ajili ya matibabu. Tupo tayari kutoa michango kwa ajili ya vifaa vya matibabu tunaomba waviweke wazi. Kwa kweli tumechoka na hizi gharama za kupeleka wagonjwa nje ya nchi. Mbona mnajipigia debe wenyewe, vipi kuhusu manesi?