Mh. Werema amfundisha Lissu somo la sheria bungeni

napata kuelewa werema alipewa vipi ujaji na hata huu U AG...werema ni mbumbumbu....
 
Sasa kipi unacho bisha hapo ? Mh Werema amesema wazi watu wenye utaalamu na elimu ya sheria ya katiba ni kama Dr. Mwakyembe, Prof. Palamagamba Kabudi na sio Prof. Shivji, yeye hakusomea sheria ya katiba. Sikiliza Bunge acha uchovu


Yaani wewe unabebewa akili na Werema! Pole!
 
Mwakyembe na kabudi wameongea nn mlichokiona cha maana mpaka mseme ni magwiji wa katiba?ushabiki wa mambo ni ujinga unaoiweka nchi yetu hapa ilipo.mtu anajua sheria za katiba lkn mpaka leo tunaunda katba mpya no publication inayoonyesha usomi wao kuhusu katiba.wakionyesha ukakamavu kidogo tu uwaziri na ubunge wa kuteuliwa.Elimu aliyo nayo Lissu ndio inayotufaa sisi wanyonge ili tupate pa kuanzia.Msiwasifie watu kwa sababu Lisu comes 4rm m4c.Go on Lisu safari ya mabadiliko ni ngumu na yataka moyo.For sure ndani ya jamii forum kenge wamo na mamba pia.Mtu kasema gagulo la katiba linahitaji viraka anatoa elimu kwa mkakamavu mwenye hisia kali na jeans mpya.Haviendani kamwe.
 
Wewe ulitaka TL abishe ili atolewe nje? Mpumbavu akiongea muache ajifurahishe mwenyewe pamoja na wapumbavu wenzake wafurahie kwani ukibishana naye na wewe utaonekana mpumbavu.
 
Mh. Mwanasheria mkuu wa serikali Jaji Werema, amempa somo Tundu Lissu kuwa bado ni mchanga kwenye sheria, kwani yeye anajua sheria za mazingira tu na hajui sheria za katiba. Kwa maana hiyo basi, ameseme yeye amejitolea kumfundisha Lissu sheria za katiba ili aweze kutafsiri vizuri katiba na kujua maana yake. Hii yaonyesha kumbe Lissu ni mchovu wa elimu ya sheria ya katiba. Kitu kama hukijui Mh. Lissu , sema hukijui kuliko kupotosha wananchi kwa maana siyo.

Hapa wewe ndiye unayeonesha uchovu wa elimu kwa maana ukisikia tu maoni ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali basi unadhani ni kauli ya Mungu na ya wengine siyo sahihi. Hii ni 'reasoning' ya ajabu sana! Tafsiri ya sheria inazingatia mambo mengi sana na ndiyo maana wanasheria wanatofautiana na ni vizuri watofautiane. Kwani hujawahi kusikia wanasheria wanatofautiana - baadhi wanasema "adhabu ya kifo ni ya kikatiri ifutwe" na wengine wanasema ni "bado inafaa iendelee"? Hata majaji wenyewe wanatofautiana kutoa hukumu - wengine wanasema hivi na wengine vile. Hivyo, Mwanasheria Mkuu wa serikali kusema "Tindu Lissu ni mchanga wa sheria kwani yeye anajua sheria za mazingira tu na hajui katiba..." Ni errenous reasoning/falacy. Kwani ambao wanasaini mikataba mibovu kwa niaba ya serikali wanapata ushauri kutoka kwa nani? Serikali inapata ushauri wa kisheria kutoka kwa nani? Kama serikali imeweza kufanya madudu yote ambayo imeweza kuyafanya, Mwanasheria Mkuu wa Serikali anayejua Katiba alikuwa wapi? Hii ni lugha tu inayotumiwa kuwakandamiza wabunge wenye maoni na mitazamo tofauti. Kama serikali na chama tawala hawataki maoni ya wengine kwa nini wanaleta bungeni hoja zijadiliwe na watalazimishaje wabunge wajadili au watoe maoni yanayofanana na ya kwao tu?
 
Lisu ni jembe la ukweli kwenye sheria .werema ni gamba tena ni mshabiki asie ona mbali
 
Sikiliza Mtu anavyo RAP na useme kama huyu ni Mwana Sheria ya Mazingira.

Anaanza kwa kutofautiana na Mwalimu wake na anamwaga Mistari hadi watu wanashangilia.

Kama huna muda, sikiliza dakika mbili za mwisho......

"Utaratibu wa Tume ya Rais wa ku-Review katiba, haukubaliki. Ni mambo YALEYALE, na watu WALEWALE, kwa manufaa ya WALEWALE, hayatupeleki popote."

 
Last edited by a moderator:
Werema si mtaaramu wa mambo ya katiba,yeye amejikita kwenya maswala ya mikataba ya kibiashara. Hivyo basi yeye angemwambia Lissu, kuwa yeye Werema na Lissu hawakujikita zaidi kwenye maswala ya katiba kwenye elimu zao za sheria.Hivyo basi kati yao hakuna mwalimu na mwanafuzi.
 
Habari Waungwana
Naomba niulize ,
1.Je mtu hujifunza darasani tu ?

2.Je kila aliyesoma mada fulani katika mfumo. rasmi wa elimu ni lazima tabia yake ibadliswe na uelewa mpya alioupata ?

Kwa swali la kwanza :
Mtakubaliana na mimi kwamba elimu ya vyuoni inaweka misingi tu , ili mtu abobee lazima aendelee kuchimbuka zaidi kibinafsi , akitafiti na kujifunza zaidi maana dunia nayo inabadilika kwa kasi vivyo hivyo na watu wake na mambo yake yote (the world is so dynamic ). Hata kama mtu alipata 1st class na haendelei kujifunza zaidi na kujikumbusha aliyokwisha jifunza , kumbukumbu lake hufifia na uweledi wake hupungua pia na asipokuwa makini digrii yake inaweza kuwa ni nishani iliyopitwa na wakati !

Kwa swali la pili :
Sio lazima tabia ya mtu, mwenendo wake na hata utendaji wa mtu uendane na kile anachokijua na kukuiamini, dhamira ya mtu naa uadilifu wake unahusika sana hapa.

Wapo Madaktari wanaojua kuvuta sigara ni hatari lakina ni wavutaji wa mfululizo(chain smoker) na hawafanyi jitihada yote kuachana na uvutaji.

Wapo wahandisi wanaojua vizuri kabisa kazi yao lakini kwa makusudi wachakachua design zao ili kupunguza gharama/kujipatia kipato visivyo halali na matokeo yake tunashuhudia majengo yanayoanguka , barabara zisizo na viwango kila mahali hapa nchini. Sio kwamba hawa waadishi hawajui , hawana akili na hawakubobea kwenye fani zao la hasha . Vivyo hivyo hata katika uhasibu , utakuata mhasibu ana CPA anafanya madudu tu na wachumi kama akina Jk , prof Ndulu, Nchemba na wengine wanashindwa kuinua uchumi wa Tz . Wanaweka na kutetea utumbo tu katika bajeti na mipango yao isiyo na tija wala masilahi endelevu kwa taifa ,ila tu inawanufaisha wao binafsi.

Mifano hiyo hapo juu ndo inayotoa soma kwetu wananchi hata suala la katiba na ujinga wa kutambiana taaluma ulioibuka siku hizi kule bungeni . Suala ni elimu zao na ujuzi wao unatumika kutimiza dhamira gani ? Je wana uadilifu. ? Je wanatafiti na jujifunza zaidi hata hao wanaojiita maprof ?

Kwa maoni yangu katika suala la katiba , hakuna dhamira ya dhati inayooneshwa ya kuwaruhusu wananchi waweke katiba yao wenyewe kwa ustawi endelevu wa taifa lao.Mimi naona kuana mkakati wa kujilinda kisiasa tu

Haiwezekani watu wanaseme kwamba kweli zingine hazitakiwi zisemwe kuhusu muungano ! na bado tumwamini hao watu kama wana nia jema na taifa hili , yaana wanadhani wananchi watakuwa wajinga siku zote kutoona huo ukweli

Ushe?nz* kabisa huu
 
Sasa tunajuwa ni kwanini Prof Shivji hakuteuliwa kwenye Tume ya Warioba, wakubwa wanataka 'makada' na huyo Pof Kabudi ticks the box! Mkuchika naye baada ya kupenea chupuchupu ya re-shuffle anaonekana kupata nguvu ya kutetea serikali dhaifu. 48 years wanaulizwa faida za muungano wao wanakuja na ngonjera. Not any more.

Where does that leave prof Mwesiga Baregu Sir?
 
Mkuu kwenye fani ya sheria na wao wan a specialize kwenye specific areas tu na si kuwa kila mtu anajua kila kitu. Mh lissu yeye ni mtaalam wa sheria za mazingira na si mtaalam wa sheria za katiba. Magwiji wa utaalam wa sheria za katiba ni Dr mwakyembe na Pro palamagamba kabudi
Ni kweli Dume la Mbegu, ila AG naye mbona amewataja makada wa CCM tu na kumwacha Dk. S. Mvungi maana naye ni mtaalamu sana wa eneo hilo. Naona kama wakati mwingine AG Werema anakuwa kikada zaidi badala ya kuwa kitaaluma na kitaalamu
 
Werema angekuwa anajua sheria za katiba angeleta ule uvundo bungeni yeye na Celina Kombani wake na kuuita muswada wa katiba mpya? Pamoja na kejeli zake wakati huo lakini siku 40 baadaye wabunge walikaa tena na kuufanyia marakebisho! Hatuna mwanasheria mkuu, tuna msanii mkuu!

Kama ulimsikia vizuri Jaji Werema inaonesha "inferiority complex" mbele ya Lissu. Badala ya kutoa hoja anajilinganisha na Lissu kwa kusema "Na mimi nimesoma, tena nimesoma sana tu"... akaendelea " umesoma paper za Mwakiyembe? Umesoma za PalaMAGAMBA?..." ina maana kuwa alilala Library akitafuta jinsi ya Kuhimili vishindo vya Lissu. Kwa ku-quote hizo paper haina maana kuwa ana kisomo, tena kasoma sana tu kama alivyodai!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Hapa wewe ndiye unayeonesha uchovu wa elimu kwa maana ukisikia tu maoni ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali basi unadhani ni kauli ya Mungu na ya wengine siyo sahihi. Hii ni 'reasoning' ya ajabu sana! Tafsiri ya sheria inazingatia mambo mengi sana na ndiyo maana wanasheria wanatofautiana na ni vizuri watofautiane. Kwani hujawahi kusikia wanasheria wanatofautiana - baadhi wanasema "adhabu ya kifo ni ya kikatiri ifutwe" na wengine wanasema ni "bado inafaa iendelee"? Hata majaji wenyewe wanatofautiana kutoa hukumu - wengine wanasema hivi na wengine vile. Hivyo, Mwanasheria Mkuu wa serikali kusema "Tindu Lissu ni mchanga wa sheria kwani yeye anajua sheria za mazingira tu na hajui katiba..." Ni errenous reasoning/falacy. Kwani ambao wanasaini mikataba mibovu kwa niaba ya serikali wanapata ushauri kutoka kwa nani? Serikali inapata ushauri wa kisheria kutoka kwa nani? Kama serikali imeweza kufanya madudu yote ambayo imeweza kuyafanya, Mwanasheria Mkuu wa Serikali anayejua Katiba alikuwa wapi? Hii ni lugha tu inayotumiwa kuwakandamiza wabunge wenye maoni na mitazamo tofauti. Kama serikali na chama tawala hawataki maoni ya wengine kwa nini wanaleta bungeni hoja zijadiliwe na watalazimishaje wabunge wajadili au watoe maoni yanayofanana na ya kwao tu?
Nimekupata Father Magobe, la umenikumbusha darasa la Logic. Thank U very much
 
Mh. Mwanasheria mkuu wa serikali Jaji Werema, amempa somo Tundu Lissu kuwa bado ni mchanga kwenye sheria, kwani yeye anajua sheria za mazingira tu na hajui sheria za katiba. Kwa maana hiyo basi, ameseme yeye amejitolea kumfundisha Lissu sheria za katiba ili aweze kutafsiri vizuri katiba na kujua maana yake. Hii yaonyesha kumbe Lissu ni mchovu wa elimu ya sheria ya katiba. Kitu kama hukijui Mh. Lissu , sema hukijui kuliko kupotosha wananchi kwa maana siyo.

"A little knowledge in a variety of subjects makes any fool wise in the midst of fools"

Mkuu, walioanzisha specialisation katika somo la sheria kwamba kuwe na wataalamu wa katiba, haki za binadamu, mazingira, mikataba ya kimataifa nk. walifundishwa na nani? Maana historia ya dini inatuambia mtu wa kwanza duniani alikuwa Adam na kisha akaletwa Hawa (Eve).

Nadhani jibu ni kwamba walijifundisha wenyewe, wakadhani wameelewa, wakakutana kikundi wakakubaliana hii iitwe hivi na vile, na wakaweka kanuni zao na mwisho ikakubaliwa na kundi kubwa zaidi baada ya kuona manufaa yake, na hivyo kuingizwa vyuoni.

Kwa maana hiyo specialisation ni cheti tu ili utambuliwe kulingana na taratibu. Wapo watu wanajua sheria kwa kujisomea tu katika vitabu majumbani mwao na wanazijua haswa, lakini kwa kuwa hawajafuata taratibu hawatambuliwi kisheria.

Hivi kuna maabara ya sheria mpaka isemekane; huwezi kujua sheria ya katiba wewe hujasomea, wakati yamo katika vitabu ukitaka kujua waweza?

Msivimbishe watu vichwa bure. Kwani yule profesa Issa Shivji anayetoa somo la katiba katika ITV, ni mtaalamu wa sheria za katiba? Mbona anaichambua vizuri? Kama wapo hao wanaosemekana ni wamebobea katika katiba TZ, mbona katiba ya TZ in makosa mengi sana ya vifungu vinavyokinzana? Mfano kifungu cha mgombea binafsi. Walikuwa wapi wakati inatungwa? Na hao ma-AGs walikuwa wapi siku zote wasitoe mapendekezo ya marekebisho miaka yote hiyo?

Mbumbumbu ni mbumbumbu hata angeitwa kwa cheo gani.
 
Back
Top Bottom