Mh Rais,utayaishi maneno yako?

pia,kwa mila za kiafrika,kumnyima mtu chakula,hasa mgeni,huwa ni jambo la mwisho sana,hizi sababu za kusema kumpa mgeni chakula ni gharama,ni aibu kubwa sana kwetu kama taifa,bora tutunge sababu nyingine tu,

Hivi hao wageni wakila chakula saaana,watamaliza gunia tatu za mchele(kama laki nne hivi)

Hivi wakila sana watamaliza kuku mia tatu (kama laki sita hivi Tsh)

wakinywa sana,watamaliza vinywaji vya milioni 5?

yaani milioni kama ishirini kukirimu watu,kubadilishana mawazo na viongozi wa ndani na nje ni gharama? hata ikiwa milioni 50?

eti unawaambia mabalozi na wageni kama mzee mwinyi,leo hakuna kula! hivi kula kwao ni nini hasa kwa mtu kama balozi wa uingereza,marekani,canada,rwanda!

kweli kula nayo ni ishu!!!

unasema unabana matumizi watu wasile wakati viongozi wakuu na wakuu wa wilaya na mikoa wana vxx8 za milioni 300!!
Tumeshajua mapungufu yake kwenye kujenga hoja!msingi wa mada hii,je hoja hizo na mapungufu yake yuko radhi kuzisimamie?Au leo nguruwe haramu kesho halali
 
Huo ni wimbo wa kawaida sana, mawaziri wengi walisema kabla ya Sept wote watakuwa Dom mpaka leo bado wapo town, mzee town pazuri sana ndiyo maana hata vichaa hukimbilia town.
Kukiwa na ofisi na makazi yao dodoma,wakirudi dar si itakuwa kwa gharama zao ilimradi kila j3 mpaka ijumaa wawe ofisini dodoma?
 
Nina uhakika gharama zimepungua sana huenda kwa 50% kwa sababu wale watoto wa halaiki walikuwa wanatumia pesa nyingi sana pia ile dhifa,security ya viongozi waalikwa wa nje ambao mwaka huu hawakuja,zile military shows hazikuwepo am sure gharama imepungua sana japo hakusema ni bei gani
 
Kukiwa na ofisi na makazi yao dodoma,wakirudi dar si itakuwa kwa gharama zao ilimradi kila j3 mpaka ijumaa wawe ofisini dodoma?
Rais kwa mujibu wa ratiba ambayo ilitolewa ni kwamba yeye kuhamia ni mpaka 2019, sasa baraza la mawaziri litaendeshwaje kila mwenzi?
 
Hivi mtumishi atasafiri bila posho au chakula? hata viongozi wa dini wanapewa posho wakitaka kusafiri mkuu. Taja nchi ambayo haitoi posho
Mimi nilimaanisha posho ya chakula ambayo Magufuli kaifutilia mbali. Uswisi ni nchi mojawapo ambapo posho ya chakula imefutwa. Utarudishiwa pesa za usafiri na malazi tu, pale unapoenda nje ya kituo cha kazi, kikazi.

Posho utolewa kwa safari za kikazi tu. Na siyo sherehe. Kwa mfano, watumishi wengine wa serikali wanaishi Zurich; hivyo wana-commute kila siku kwenda Bern (makao makuu ya nchi) ofisini. Hawa wanapoenda Bern kwenye sherehe za serikali hawalipwi chochote, kila kitu is on them.

Besides, mfumo wa posho wa nchi nyingi za Ulaya ni wa kutumia na kurudishiwa. Siyo kupewa beforehand kama Tanzania. Hivyo utarudishiwa pesa yako jinsi ulivyotumia kwa kuonyesha risiti halali. Na kwa vile kila malipo yanapatiwa risiti, huwezi kugushi kama wafanyavyo Tanzania.

Katika jambo ambalo namuunga mkono kwa kiasi fulani Magufuli hadi sasa ni hilo la posho. Ingawa bado hajawa consistent katika hili. Na haswa bado suala linategemea matamshi yake, badala ya kuongozwa na sheria/kanuni za utumishi wa umma. Kwa mfano, sijaelewa logic behind kufanya sherehe mwaka huu, kama lengo la kutofanya mwaka jana lilikuwa ni kuokoa fedha, kwa sababu watanzania wengi bado wanakumbana na matatizo ya huduma za kijamii. Kwani matatizo yameisha? Hilo la kusema kwamba sherehe za mwaka huu zaweza kuwa za mwisho kufanyika Dar, nalo halina mantiki kwa kuzingatia sababu za mwaka jana. Kama lengo ni kuacha legacy ya sherehe za uhuru Dar, kuna mambo mengi yangefanyika pasipo kutumia gharama kubwa. Kwa mfano: kujenga mnara wa kumbukumbu; kufanya huduma za kijamii (mfano wa kufanya usafi kama mwaka jana); kuhutubia taifa kutokea Ikulu n.k.

Kwa mtazamo wangu sioni ulazima wa viongozi kutoka mikoa yote kusafiri hadi sehemu moja kwa ajili ya sherehe ya masaa machache tu. It isn't worth it kiuchumi. Ingekuwa kwamba uwepo wao ni wa muhimu sana kwa ajili ya sherehe, angalau ningeelewa. Lakini wanaenda kuongeza idadi ya wahudhuriaji tu. Sherehe kama hizo zinapaswa kuhudhuriwa na viongozi waishio eneo ambapo sherehe zinafanyika. Hivi ndivyo kubana matumizi kunapaswa kuwa.
 
Yeye kasema zote, mtajie nchi isiyotoa posho ili abadilli msimamo wake
Nimeshamtajia.
Kwa upande mwingine, kwani ni lazima tuige kila kitu kutoka kwingine? Halafu mbona tunapenda kuiga mambo ambayo yananufaisha wachache tu? Mbona hatuigi mambo mazuri kutoka nchi zingine yenye faida kwa wengi? Kwa mfano: mbona hatuigi utaratibu wa matokeo ya urais kupingwa mahakamani? Mfumo wa kuwa na tume huru ya uchaguzi? Mishahara ya viongozi wa serikali kuwa public? Rais kulipa kodi? Viongozi waandamizi wa serikali na umma kutumia vyombo binafsi vya usafiri? N.k.
 
Inzi umeleza vizuri, tatizo langu kwa miundombinu ya Uswizi na Tz na ardhi na mbingu mkuu, PM amehamia Dom, kutoka Dom mpaka Dsm kaenda na watumishi siyo chini ya 50. Issue ya chakula hata mimi siungi mkono isipokuwa perdiem ni haki yao.
 
One day atakuja na wazo kwamba watumishi wa serikali wote wasilipwe mshahara sababu hawawezi kulipwa mishahara wakati waTZ hawana madaraja ya kutosha..Nawaza Tu
 
Mimi nampongeza sana kwa sababu nahisi waliokuwa wanachangia kuongezeka kwa gharama ni pamoja na kualika Marais kutoka nchi nyingine nao ni lazima uwagharimie tena kwa pesa nyingi, lkn mwaka huu ni sisi tu humu ndani so lazima gharama zimepungua sana
 
Mimi nampongeza sana kwa sababu nahisi waliokuwa wanachangia kuongezeka kwa gharama ni pamoja na kualika Marais kutoka nchi nyingine nao ni lazima uwagharimie tena kwa pesa nyingi, lkn mwaka huu ni sisi tu humu ndani so lazima gharama zimepungua sana
Je,atayaishi maneno yake?
 
Siyo kweli. Siyo nchi zote duniani zinatoa posho kaka..
Haitoshi kusema siyo nchi zote duniani. Hoja yako ingekuwa na nguvu kama ungezitaja baadhi ya nchi ambazo hazilipi posho.
Mtaishia kubishana "zinalipa".... " hazilipi" na wote mtaonekana siyo gt.
 
Back
Top Bottom