Taarifa za kuaminika kutoka UDOM zinasema kuwa, Mh. Mizengo K.P. Pinda, leo alikuwa na mkutano na wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kwa takribani masaa 3. Akiwa Chuoni hapo wahadhiri waliimba nyimbo za Solidality, na walionekana kuwa hawako tayari kuletewa siasa kwenye madai yao. Inasemekena hata kama saikolojia hujasoma, ungepata ujumbe huo toka kwenye nyuso zao....
Pinda alilazimika kutumia busara ya ziada kuwashawishi wahadhiri hao, kwanza alianza kwa kuongea na uongozi wao (UDOMASA) kwa zaidi ya nusu saa kabla ya kuingia ukumbini CHIMWAGA kuongea nao. Nusanusa walishampelekea taarifa kuwa mzee, usiingie na story! Kabala hajaongea na wahadhiri wote kwa ujumla wao, wahadhiri hao waliutaka uongozi wa UDOM uwaombe radhi wahadhiri hao kwa kuwadharau: Kusema (kwenye vyombo vya habari) kuwa madai yao si ya msingi, kudai kuwa hawana uelewa mkubwa na kudai kuwa uongozi wa UDOM ulikuwa unafanya mikutano na UDOMASA mara kwa mara wakati wa mikutano yao endelevu (Mgomo wao). Prof. Kikula, kwa kusoma upepo, aliomba radhi kwa unyeyekevu mkubwa.
Wakichangia hoja baada ya kuridhika na kuombwa msamaha, baadhi ya wajumbe walionekana kuwa na hasira kubwa na Prof. Mlacha, ambaye ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo-PFA). Walisikika wakisema, hatumtaki, mwondoe, kondoo mweusi, nk. Maneno hayo yalimfikia moja kwa moja Mh. Pinda na alisononeka sana.
Mh.Pinda amesema kuwa, Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ataingia UDOM JUMATATU 17/01/2011 kufanya ukaguzi na kuandika ripoti yake. Ripoti hiyo inayotarajiwa kuwasilishwa kwa Mh. Pinda baada ya wiki 2, itaisadia serikali kufanya maamuzi stahiki. Dalili za awali zinaonyesha kuwa moto waweza kumwakia Prof. Mlacha au mtu mwingine au watu wengine kati ya uongozi wa juu wa Chuo.
Mh.Pinda ameahidi kuwalipa wahadhiri hao madai yao yoooote kufikia mwishoni mwa Februali 2011. Madai haya ni pamoja na:
1. Pesa zilizoibiwa kwenye mishahara yao,
2. Nyongeza ya mishahara yao,
3. Pesa za kujikimu,
Madai mengine ya waalimu hao ni pamoja na Pesa za mizigo pamoja na kuwapatia Salary slips zao (maana zile walizokuwa wakipewa, yasemekana si halali; ni za kuchakachua)!
Yaonekana wahadhiri hao wameamua kumsikiliza na kumkubalia Mh. Pinda kuahirisha mgomo (mikutano yao hiyo endelevu) na kuona kama ahadi ya Mh. Pinda itakuwa imetekelezwa ifikapo 28/02/2011. Inaelekea kuwa wahadhiri wamekubali kwa shingo upande.
Mambo ya kujiuliza:
1. Je, serikali kwa kutumia vyombo vyake ilikuwa haijui kuwa kuna wizi?
2. Je, Prof. Mlacha (ambaye amejiita kondoo mweusi) ndo mhusika pekee wa matatizo ya UDOM? Je, ujasiri wa kuchakachua mishahara na haki zingine ya Wahdhiri alikuwa akiupata wapi?
3. Je, serikali kweli itamwajibisha ikiwa ataonekana anahusika? Au itamhamishia Chuo kingine au kumpa cheo kingine?
Mimi naamini kama kweli Prof. Mlacha kahusika, basi si yeye peke yake.......
Karibuni kwa hoja
Pinda alilazimika kutumia busara ya ziada kuwashawishi wahadhiri hao, kwanza alianza kwa kuongea na uongozi wao (UDOMASA) kwa zaidi ya nusu saa kabla ya kuingia ukumbini CHIMWAGA kuongea nao. Nusanusa walishampelekea taarifa kuwa mzee, usiingie na story! Kabala hajaongea na wahadhiri wote kwa ujumla wao, wahadhiri hao waliutaka uongozi wa UDOM uwaombe radhi wahadhiri hao kwa kuwadharau: Kusema (kwenye vyombo vya habari) kuwa madai yao si ya msingi, kudai kuwa hawana uelewa mkubwa na kudai kuwa uongozi wa UDOM ulikuwa unafanya mikutano na UDOMASA mara kwa mara wakati wa mikutano yao endelevu (Mgomo wao). Prof. Kikula, kwa kusoma upepo, aliomba radhi kwa unyeyekevu mkubwa.
Wakichangia hoja baada ya kuridhika na kuombwa msamaha, baadhi ya wajumbe walionekana kuwa na hasira kubwa na Prof. Mlacha, ambaye ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo-PFA). Walisikika wakisema, hatumtaki, mwondoe, kondoo mweusi, nk. Maneno hayo yalimfikia moja kwa moja Mh. Pinda na alisononeka sana.
Mh.Pinda amesema kuwa, Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ataingia UDOM JUMATATU 17/01/2011 kufanya ukaguzi na kuandika ripoti yake. Ripoti hiyo inayotarajiwa kuwasilishwa kwa Mh. Pinda baada ya wiki 2, itaisadia serikali kufanya maamuzi stahiki. Dalili za awali zinaonyesha kuwa moto waweza kumwakia Prof. Mlacha au mtu mwingine au watu wengine kati ya uongozi wa juu wa Chuo.
Mh.Pinda ameahidi kuwalipa wahadhiri hao madai yao yoooote kufikia mwishoni mwa Februali 2011. Madai haya ni pamoja na:
1. Pesa zilizoibiwa kwenye mishahara yao,
2. Nyongeza ya mishahara yao,
3. Pesa za kujikimu,
Madai mengine ya waalimu hao ni pamoja na Pesa za mizigo pamoja na kuwapatia Salary slips zao (maana zile walizokuwa wakipewa, yasemekana si halali; ni za kuchakachua)!
Yaonekana wahadhiri hao wameamua kumsikiliza na kumkubalia Mh. Pinda kuahirisha mgomo (mikutano yao hiyo endelevu) na kuona kama ahadi ya Mh. Pinda itakuwa imetekelezwa ifikapo 28/02/2011. Inaelekea kuwa wahadhiri wamekubali kwa shingo upande.
Mambo ya kujiuliza:
1. Je, serikali kwa kutumia vyombo vyake ilikuwa haijui kuwa kuna wizi?
2. Je, Prof. Mlacha (ambaye amejiita kondoo mweusi) ndo mhusika pekee wa matatizo ya UDOM? Je, ujasiri wa kuchakachua mishahara na haki zingine ya Wahdhiri alikuwa akiupata wapi?
3. Je, serikali kweli itamwajibisha ikiwa ataonekana anahusika? Au itamhamishia Chuo kingine au kumpa cheo kingine?
Mimi naamini kama kweli Prof. Mlacha kahusika, basi si yeye peke yake.......
Karibuni kwa hoja