Lyimo
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 3,826
- 2,017
Inakumbukwa kuwa mwaka jana mwezi wa tano kulikuwa na vuta nikuvute kati ya Mh. Zitto Kabwe na waziri wa Fedha na Uchumi Mh. Mustafa Mkulo. Katika mkutano wa hadhara mjini Mbeya, Zitto alielezea habari ya kufilisika kwa serikali na hata kushindwa kulipa mishahara ya watumishi wake kwa wakati.
Mh. Mstafa Mkulo alimkanusha vikali na kumuita ni mzushi. Mh. Mkulo aliungana na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Ndg. Harry Kitilya katika mkutando na waandishi wa habari mjini Dodoma na kumkanusha vikali Zitto Kabwe huku akieleza jinsi serikali inavyokusanya mapato yake kutokana na kodi mbalimbali.
Pia alichanganua kiasi cha fedha katika ulipaji wa mishahara, lakini hakueleza uchangiaji wa serikali katika dshughuli za maendeleo na huduma mbalimbali. Tangu kipindi hicho, serikali imekuwa ikishindwa kuendesha shughuli zake nyingi kikamilifu (hasa huduma nyingi za kijamii na miradi ya maendeleo).
Taasisi zake nyingi zipo kwenye ukata mkali na wakuu wake wakihangaika kuzisimamia kutokana na ufinyu wa pesa walionao. Jana katika kikao cha Bunge, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) Mh. George Mkuchika alikubali kuwa Serikali imefilisika na imeshindwa kuendesha shughuli zake nyingi zinazosimamiwa na Halmashauri na taasisi zake nyingine.
Mara nyingi viongozi wa serikali yetu wamekuwa hawasemi ukweli katika mambo mablimbali, na hili ni tatizo kubwa nchini kwetu. Waziri mwenyedhamana anasema fedha zipo, wakati viongozi wa vitengo mbalimbali wanasimamisha shughuli na kutuambia serikali haina fedha. Maranyingine imetupelekea kuwalaumu viongozi wa vitengo kwa kuwa ni wafujaji wa pesa za serikali kumbe hawakupokea kasma stahili.
Kwa uongo wa Mh. Mkulo, anastahili kumuomba radhi Mh. Zitto na watanzania wengine tuliopotoka na kumlaumu Mh. Zitto kuwa ni mropokaji wa vitu si vya kweli.
Vilevile itatuwia vigumu sana kuamini matamshi yoyote ya viongozi wetu kwani hawana utamaduni wa kuwajibika pindi wanapobainika hawakuwa sahihi katika matamshi yao ama utendaji wao.
Mh. Mstafa Mkulo alimkanusha vikali na kumuita ni mzushi. Mh. Mkulo aliungana na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Ndg. Harry Kitilya katika mkutando na waandishi wa habari mjini Dodoma na kumkanusha vikali Zitto Kabwe huku akieleza jinsi serikali inavyokusanya mapato yake kutokana na kodi mbalimbali.
Pia alichanganua kiasi cha fedha katika ulipaji wa mishahara, lakini hakueleza uchangiaji wa serikali katika dshughuli za maendeleo na huduma mbalimbali. Tangu kipindi hicho, serikali imekuwa ikishindwa kuendesha shughuli zake nyingi kikamilifu (hasa huduma nyingi za kijamii na miradi ya maendeleo).
Taasisi zake nyingi zipo kwenye ukata mkali na wakuu wake wakihangaika kuzisimamia kutokana na ufinyu wa pesa walionao. Jana katika kikao cha Bunge, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) Mh. George Mkuchika alikubali kuwa Serikali imefilisika na imeshindwa kuendesha shughuli zake nyingi zinazosimamiwa na Halmashauri na taasisi zake nyingine.
Mara nyingi viongozi wa serikali yetu wamekuwa hawasemi ukweli katika mambo mablimbali, na hili ni tatizo kubwa nchini kwetu. Waziri mwenyedhamana anasema fedha zipo, wakati viongozi wa vitengo mbalimbali wanasimamisha shughuli na kutuambia serikali haina fedha. Maranyingine imetupelekea kuwalaumu viongozi wa vitengo kwa kuwa ni wafujaji wa pesa za serikali kumbe hawakupokea kasma stahili.
Kwa uongo wa Mh. Mkulo, anastahili kumuomba radhi Mh. Zitto na watanzania wengine tuliopotoka na kumlaumu Mh. Zitto kuwa ni mropokaji wa vitu si vya kweli.
Vilevile itatuwia vigumu sana kuamini matamshi yoyote ya viongozi wetu kwani hawana utamaduni wa kuwajibika pindi wanapobainika hawakuwa sahihi katika matamshi yao ama utendaji wao.