Unless mwandishi awe amekosea ila kama ndiyo reasoning ya polisi wetu hiko hivi mbona tumekula hasara! mwizi kashikwa na ngozi unasema ana tabia nzuri? Mh. Hebu tuambie manake najua unapokea briefing kutoka kwa walio chini yako kila siku.
Polisi akamatwa na risasi 35 mwenzake wadai ni mtu mwema
Na Mwandishi Wetu
ASKARI polisi mmoja wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, ameiba risasi 35 za bunduki na kuzihifadhi katika duka moja la dawa baridi la Alpho lililopo Oysterbay, jijini Dar es Salaam.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili jana, zimeeleza kuwa tukio hilo lilitokea Aprili 3, mwaka huu katika duka hilo la dawa na kufahamisha kwamba, askari huyo alikwenda katika duka hilo akiwa na mzigo huo na kuomba wamhifadhie hadi saa 2:00 usiku atakapokwenda kuuchukua.
Mmiliki wa duka hilo, Norbert Marealle aliliambia gazeti hili jana kwamba, askari huyo alifika dukani kwake na kumkuta mfanyakazi wake mgeni akamuomba amhifadhie mzigo huo hadi saa 2:00 usiku atakapokwenda kuuchukua.
Alidai kuwa askari huyo alimweleza mfanyakazi huyo mgeni kwamba, amtaarifu mwenzake anayeitwa Mariam Abdul ambaye hakuwepo wakati huo.
Marealle alidai kuwa baada ya Mariamu kurejea aliambiwa juu ya mzigo huo ambao ulikuwa umefungwa ndani ya mifuko miwili ya Rambo na kwamba alipouona alishituka na kuamua kuufungua ili waone kilichomo.
Alidai kuwa walipoufungua ndani walikuta kasha mbili ambazo walizifungua na kukuta zimesheheni risasi, wakaamua kumpigia simu (Marealle) na kwamba; kwa vile alikuwa mbali na eneo hilo aliwaambia wakatoe taarifa haraka katika Kituo cha Polisi Oysterbay.
Walienda kule na kupewa askari kanzu sita ambao walienda kuweka doria ili wamtie mbaroni mhusika lakini siku hiyo, hakutokea, alisema Marealle.
Alindelea kusimulia akisema: Kesho yake askari hao waliendelea kuweka doria lakini hakutokea na wakafanya hivyo kwa siku mbili na siku ya tatu (Aprili 5) askari doria wakiwa hawapo, askari huyo alifika kuuchukua.
Ikabidi mmoja wa wauzaji wangu aingie chumbani na kuwapigia simu polisi na walipofika wakamtia mbaroni. Polisi walikiri kuwa wanamfahamu mtuhumiwa huyo na kwamba ni askari mwenzao kisha walimchukua na kuondoka naye kwenda kituoni, alidai Marealle.
Alidai kuwa siku hiyo usiku, mkewe alikwenda kituo cha polisi Oysterbay na kutoa maelezo na kuhifadhiwa kwa kumbukumbu namba OB/RB/6137/2009.
Alidai kuwa baadaye waliarifiwa na polisi kuwa asiwe na wasiwasi kwa sababu askari aliyebambwa hana historia mbaya ya kikazi na hazikuchukuliwa hatua zozote.
Hata hivyo, Marealle alisema alipata wasiwasi juu ya maelezo hayo ikizingatiwa kuwa suala la risasi ni nyeti na si jambo la kawaida kwa polisi kwenda kuzihifadhi kwa raia, hivyo aliamua kutoa taarifa kwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova ambaye alimpigia simu mkuu wa kituo hicho cha polisi ambaye alimjibu kuwa hana taarifa.
Baadaye mkuu huyo wa kituo akaomba kuonana na mmiliki wa duka hilo la madawa ambaye alipofika alimwambia ampe maelezo ambayo aliyaandika.
Mwananchi lilipowasiliana na Kamanda Kova, alikiri kupewa taarifa za tukio hilo na mmoja wa wanafamilia ya Marealle, lakini akamtaka awasiliane na Kamanda wa Polisi Mkoa (RPC) wa Kindondoni.
Ni kweli kuna mama mmoja aliniambia juu ya tukio la namna hiyo nikamuelekeza awasiliane na RPC. Sasa nashangaa hadi sasa hajaenda kumuona, alisema Kova na kusisitiza kuwa atalifanyia uchunguzi suala hilo na kulitolea taarifa.
Gazeti hili lilipowasiliana na RPC wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye kutaka ufafanuzi wa suala hilo, akajibu kuwa ofisi yake haina taarifa yoyote kuhusiana na tukio hilo.
Sina taarifa hiyo, alisema Kalunguyeye ambaye huwa hapendi kuzungumza na waandishi wa habari. Hata katika tukio la hivi karibuni la kuuawa kwa dereva teksi, kwa kupigwa risasi na polisi maeneo ya Kimara jijini Dar es Salaam, alipoulizwa na gezeti hili alijibu kuwa hana taarifa ya tukio hilo.
CHANZO: Gazeti la Mwananchi
Polisi akamatwa na risasi 35 mwenzake wadai ni mtu mwema
Na Mwandishi Wetu
ASKARI polisi mmoja wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, ameiba risasi 35 za bunduki na kuzihifadhi katika duka moja la dawa baridi la Alpho lililopo Oysterbay, jijini Dar es Salaam.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili jana, zimeeleza kuwa tukio hilo lilitokea Aprili 3, mwaka huu katika duka hilo la dawa na kufahamisha kwamba, askari huyo alikwenda katika duka hilo akiwa na mzigo huo na kuomba wamhifadhie hadi saa 2:00 usiku atakapokwenda kuuchukua.
Mmiliki wa duka hilo, Norbert Marealle aliliambia gazeti hili jana kwamba, askari huyo alifika dukani kwake na kumkuta mfanyakazi wake mgeni akamuomba amhifadhie mzigo huo hadi saa 2:00 usiku atakapokwenda kuuchukua.
Alidai kuwa askari huyo alimweleza mfanyakazi huyo mgeni kwamba, amtaarifu mwenzake anayeitwa Mariam Abdul ambaye hakuwepo wakati huo.
Marealle alidai kuwa baada ya Mariamu kurejea aliambiwa juu ya mzigo huo ambao ulikuwa umefungwa ndani ya mifuko miwili ya Rambo na kwamba alipouona alishituka na kuamua kuufungua ili waone kilichomo.
Alidai kuwa walipoufungua ndani walikuta kasha mbili ambazo walizifungua na kukuta zimesheheni risasi, wakaamua kumpigia simu (Marealle) na kwamba; kwa vile alikuwa mbali na eneo hilo aliwaambia wakatoe taarifa haraka katika Kituo cha Polisi Oysterbay.
Walienda kule na kupewa askari kanzu sita ambao walienda kuweka doria ili wamtie mbaroni mhusika lakini siku hiyo, hakutokea, alisema Marealle.
Alindelea kusimulia akisema: Kesho yake askari hao waliendelea kuweka doria lakini hakutokea na wakafanya hivyo kwa siku mbili na siku ya tatu (Aprili 5) askari doria wakiwa hawapo, askari huyo alifika kuuchukua.
Ikabidi mmoja wa wauzaji wangu aingie chumbani na kuwapigia simu polisi na walipofika wakamtia mbaroni. Polisi walikiri kuwa wanamfahamu mtuhumiwa huyo na kwamba ni askari mwenzao kisha walimchukua na kuondoka naye kwenda kituoni, alidai Marealle.
Alidai kuwa siku hiyo usiku, mkewe alikwenda kituo cha polisi Oysterbay na kutoa maelezo na kuhifadhiwa kwa kumbukumbu namba OB/RB/6137/2009.
Alidai kuwa baadaye waliarifiwa na polisi kuwa asiwe na wasiwasi kwa sababu askari aliyebambwa hana historia mbaya ya kikazi na hazikuchukuliwa hatua zozote.
Hata hivyo, Marealle alisema alipata wasiwasi juu ya maelezo hayo ikizingatiwa kuwa suala la risasi ni nyeti na si jambo la kawaida kwa polisi kwenda kuzihifadhi kwa raia, hivyo aliamua kutoa taarifa kwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova ambaye alimpigia simu mkuu wa kituo hicho cha polisi ambaye alimjibu kuwa hana taarifa.
Baadaye mkuu huyo wa kituo akaomba kuonana na mmiliki wa duka hilo la madawa ambaye alipofika alimwambia ampe maelezo ambayo aliyaandika.
Mwananchi lilipowasiliana na Kamanda Kova, alikiri kupewa taarifa za tukio hilo na mmoja wa wanafamilia ya Marealle, lakini akamtaka awasiliane na Kamanda wa Polisi Mkoa (RPC) wa Kindondoni.
Ni kweli kuna mama mmoja aliniambia juu ya tukio la namna hiyo nikamuelekeza awasiliane na RPC. Sasa nashangaa hadi sasa hajaenda kumuona, alisema Kova na kusisitiza kuwa atalifanyia uchunguzi suala hilo na kulitolea taarifa.
Gazeti hili lilipowasiliana na RPC wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye kutaka ufafanuzi wa suala hilo, akajibu kuwa ofisi yake haina taarifa yoyote kuhusiana na tukio hilo.
Sina taarifa hiyo, alisema Kalunguyeye ambaye huwa hapendi kuzungumza na waandishi wa habari. Hata katika tukio la hivi karibuni la kuuawa kwa dereva teksi, kwa kupigwa risasi na polisi maeneo ya Kimara jijini Dar es Salaam, alipoulizwa na gezeti hili alijibu kuwa hana taarifa ya tukio hilo.
CHANZO: Gazeti la Mwananchi