Mh.Kilango malchela na mswada wa marekebisho ya katiba

kajunju

JF-Expert Member
Jun 30, 2011
999
315
Mswada wa marekebisho ya katiba ulikuwa unajadiliwa bungeni jioni hii, mh kilango kaja na suara la wakuu wa wilaya kuendelea kuwa wahusika wakuu kwenye kamati ya uundwaji wa katiba mawilayani.kasema wapate recognition kwani wameteuliwa na rais.kwenye mswada wa awali uliwatambua ma-dc lakini mabadiriko ya sasa yanamtambua mkurugenz wa wilaya kuwa awe msimamizi na waripoti kwake mara kwa mara. Mh kilango kakomalia suara la ma-dc kwa kuungwa mkono na shekifu,said mkumba. Mvutano huu ata welema kawaogopa wabunge wa ccm na kashauri kinafiki.mama spika ametumia busara kwa kuwaagiza suara lirudishwe kwenye kamati ili waje na dc aendelelee kuwa mtu muhim kwenye kamati,mkurugenzi awe mhusika kama mswada mpya unavyoeleza au wafutwe wote dc na mkurugenzi.shekifu anasema dc apate heshima kwa kuwa ni mteule wa rais.dc ni kada wa chama na mjumbe wa vikao vya chama lakin kilango na shekifu wameendelea kutetea upupu huu. Ni maskitiko yangu kuwa mtu anaweza kuleta hoja isiyo na macho, kichwa wala miguu ili watu wajadiri. Nchi hii tumepata matatizo kwa sababu ya watu kupewa heshima<recognition> ambayo haiongezi kitu mfukoni bali inakula muda wa wa-tz. Mh kilango bado naisi ana mawazo ya mzee malchela alivyoitwa karandinga.je sasa hiv malchela na ukarandinga yako wapi?kama anatetea mbinu aliyotumia malchela kwa ma-dc kubadiri matokeo b'mulo kwa sasa nafasi hii haipo tena.mwisho naomba mungu anipe uhai wa miaka 10 mbele nione mh kilango na mh shekifu watakavyoendelea kuaibika. Nawasilisha
 
Back
Top Bottom