Kiresua
JF-Expert Member
- May 13, 2009
- 1,184
- 259
- Thread starter
- #81
Ni wazi wengi waliochangia hii mada ni CDM damu halafu wafupi wa uelewa, mleta mada kaweka wazi nami nakubaliana nae kwamba alivyofanya JM ni kitu kizuri bila kuleta ushabiki wa chama yaani;
1. Kuanzisha ofisi ya maendeleo ya jimbo, ni wabunge wangapi wamefanya hivyo aidha wa CCM au CDM?
2. Kuanzisha free no ili wananchi wake waweze kumtumia kero zao bure kwa kutumia SMS wangapi wanayo hiyo?
3. Wabunge wangapi CDM au CCM wametumia hela zao za mikopo ya magari kuanzisha kitu ambacho wanatarajio kitongeza chachu ya maendeleo jimboni mwao?
Ni vema kama kina sie ambao hatujafungana upande wowote tunaangalia mambo kwa mapana zaidi kuliko kuwa kipofu wa kila kitu cha CCM au CDM hakifai sababu tu kimeanzishwa na mpinzani wako, kweli umaskini wa fikra mbaya sana.
Suala sasa kama ile ofisi ina tija ndio hoja, lakini wazo ni zuri nami pia lanipongeza ingawa hiyo shoo sikuiona.
halow, naunga mkono hoja yako, ingawa natofautiana nawe kweny eneo la ni wabunge wangapi wa cdm wametumia mkopo wao. Kwa tarf nilizo nazo, MH LEMA Ar alitumia takriban m 50 za ule mkopo kuanzisha taasisi ya mikopo kwa akina mama, mh Zitto na kgm dv org yake pia ni miongoni mwa mifano michache. Sasa kama leo nimejua ya mh Januari sina Nongwa kumpongeza