MGOMO WA MADAKTARI: Waziri wa Afya kitanzini

2mbaku

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
316
67
JINAMIZI la mgomo wa madaktari bado linaendelea kuitafuna serikali baada ya jana, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na wanaharakati kutoa matamko mawili tofauti wakitaka Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Haji Mponda na naibu wake Dk. Lucy Nkya kujiuzulu nyadhifa zao au kuwajibishwa.

Wanaharakati pia wamempa wiki moja Waziri Mkuu Mizengo Pinda, awe ametangaza hasara na madhara ambayo wananchi na taifa wamepata kutokana na mgomo wa madaktari uliosababisha vifo kadhaa.

Aidha wamemtaka Spika wa Bunge Anne Makinda kuuomba radhi umma wa Watanzania kutokana na hatua na kauli zake walizodai ni za kibabe ndani ya Bunge za kuzima hoja za wabunge katika kutafakari mgogoro huo.

CHADEMA katika tamko lao mbali ya kuwataka viongozi hao wawili wa kisiasa kuwajibika, walieleza kushangazwa na ukimya ulioonyeshwa na Rais Jakaya Kikwete katika kipindi chote cha wiki tatu cha mgomo huo wa madaktari uliosababisha kuzorota kwa huduma katika hospitali zote kuu za serikali.

Mbali ya hilo, chama hicho pia kilielekeza lawama zake kwa Pinda kwa kuchelewa kuchukua hatua za haraka za kuzima mgomo huo hata kusababisha madhara makubwa ya kibinadamu.
 
Back
Top Bottom