Plato
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 420
- 94
Mwandishi wa maneno haya ni mkatoliki anayejua uzito wa kauli ya baba askofu.Anapenda kuamini kuwa askofu ametoa msimamo wake binafsi na siyo tamko la kanisa wala maoni hayo siyo mafundisho rasmi ya kanisa.Askofu anapinga mgomo wa madaktari kwani ni kinyume cha maadili,anawataka wawe na huruma na watumie mbinu mbadala kudai madai yao.
Hata hivyo anakubali na kusema kuwa hawa ni watu muhimu sana.Sasa kwa nini nampinga askofu.Kwanza askofu hakuweka lawama zake sawasawa kwa upande wa serikali badala yake amewaangalia tu madaktari,pili askofu anajaribu kujenga picha kuwa madaktari ndiyo wanasababisha wagonjwa kukosa huduma kwa kugoma kwao badala ya serikali ambayo imekataa kutimiza madai ya madaktari.
Fundisho la kanisa linaruhusu migomo kama hatua muhimu na wakati mwingine ya lazima kwenye kudai haki za raia.Kanisa linataka serikali iimarishe na kuboresha huduma za jamii ili wale wanaofanya kazi wafurahie matunda ya kazi zao na wajisikie kufanya kazi zaidi,pia serikali inapaswa kuhakikisha uwepo wa haki za binadamu.Katekisimu ya Kanisa Katoliki inasema kuwa mshahara wa haki(siyo mkubwa) ni matunda halali ya kazi.kukataa kulipa au kuzuia malipo ni grave injustice..
Mishahara inapaswa kumwezesha mtu kuendesha maisha yenye staha kwake mwenyewe, watoto na familia yake.
Migomo ni halali kimaadili(KKK) Pale inapokuwa haiwezi kuzuilika au ikiwa njia nyingine zimeshindikane au ikiwa ni lazima ili kupata faida fulani (proportionate benefit) .Sasa baba askofu anaweza pia kuulizwa maswali haya.je serikali imetoa mishahara ya haki kwa madaktari? na wanaendesha decent life?
Je serikali imeimarisha huduma za jamii zikiwemo matibabu kiasi cha kuwafanya wafanyakazi kufurahia kufanya kazi zao? je, mgomo wa madktari umetokea kwa sababu madaktari wamependa au ni baada ya njia zote kushindikana kutokana na serikali kawadharau na kutowasikiliza?
Kama majibu yote ni hapana ni vipi tena askofu asipinge ukosefu wa haki serikali inaofanya kwa watanzania hawa badala yake anakemea madaktari. na je mantiki inaonyeshaje kawa madakatari na siyo serikali ndo wanasababisha mateso ya watu,mimi nadhani lawama zote ziende kwa serikali,Tatizo kwa askofu kilaini anayeongoza serikali kwake ni chaguo la Mungu na hajawahi kusema kama Mungu alishajitenga naye.Labda anaona akikemea serikali atakuwa amefanya kufuru kwani atadharau mteule wa mungu.
Vinginevyo Mgomo wa madaktari haujavunja maadili yoyote ya taifa, dini na hata udaktari wenyewe.Napingana na baba askofu na ninaunga mkono mgomo wa madaktari hadi serikali itakapotimiza madai yao au itakapojiuzuru.maswali kama watu wanakufa nk yanayo majibu ya kuridhisha(ANDISHI HILI NI MWITIKO KWA HABARI ILIYO KWENYE www.mjengwablog.com)
Hata hivyo anakubali na kusema kuwa hawa ni watu muhimu sana.Sasa kwa nini nampinga askofu.Kwanza askofu hakuweka lawama zake sawasawa kwa upande wa serikali badala yake amewaangalia tu madaktari,pili askofu anajaribu kujenga picha kuwa madaktari ndiyo wanasababisha wagonjwa kukosa huduma kwa kugoma kwao badala ya serikali ambayo imekataa kutimiza madai ya madaktari.
Fundisho la kanisa linaruhusu migomo kama hatua muhimu na wakati mwingine ya lazima kwenye kudai haki za raia.Kanisa linataka serikali iimarishe na kuboresha huduma za jamii ili wale wanaofanya kazi wafurahie matunda ya kazi zao na wajisikie kufanya kazi zaidi,pia serikali inapaswa kuhakikisha uwepo wa haki za binadamu.Katekisimu ya Kanisa Katoliki inasema kuwa mshahara wa haki(siyo mkubwa) ni matunda halali ya kazi.kukataa kulipa au kuzuia malipo ni grave injustice..
Mishahara inapaswa kumwezesha mtu kuendesha maisha yenye staha kwake mwenyewe, watoto na familia yake.
Migomo ni halali kimaadili(KKK) Pale inapokuwa haiwezi kuzuilika au ikiwa njia nyingine zimeshindikane au ikiwa ni lazima ili kupata faida fulani (proportionate benefit) .Sasa baba askofu anaweza pia kuulizwa maswali haya.je serikali imetoa mishahara ya haki kwa madaktari? na wanaendesha decent life?
Je serikali imeimarisha huduma za jamii zikiwemo matibabu kiasi cha kuwafanya wafanyakazi kufurahia kufanya kazi zao? je, mgomo wa madktari umetokea kwa sababu madaktari wamependa au ni baada ya njia zote kushindikana kutokana na serikali kawadharau na kutowasikiliza?
Kama majibu yote ni hapana ni vipi tena askofu asipinge ukosefu wa haki serikali inaofanya kwa watanzania hawa badala yake anakemea madaktari. na je mantiki inaonyeshaje kawa madakatari na siyo serikali ndo wanasababisha mateso ya watu,mimi nadhani lawama zote ziende kwa serikali,Tatizo kwa askofu kilaini anayeongoza serikali kwake ni chaguo la Mungu na hajawahi kusema kama Mungu alishajitenga naye.Labda anaona akikemea serikali atakuwa amefanya kufuru kwani atadharau mteule wa mungu.
Vinginevyo Mgomo wa madaktari haujavunja maadili yoyote ya taifa, dini na hata udaktari wenyewe.Napingana na baba askofu na ninaunga mkono mgomo wa madaktari hadi serikali itakapotimiza madai yao au itakapojiuzuru.maswali kama watu wanakufa nk yanayo majibu ya kuridhisha(ANDISHI HILI NI MWITIKO KWA HABARI ILIYO KWENYE www.mjengwablog.com)