Filipo
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 9,342
- 5,536
Kuna uzinduzi wa sherehe za miaka 50 ya uhuru unaofanyika kimkoa katika kiwanja cha jengo la azimio la Arusha, jirani na mnara wa mwenge jijini Arusha. Viongozi wa halmashauri zote wamehudhuria wakiwemo madiwani na viongozi wa dini zote. Pia yupo Mary Chatanda na "Mstahiki Meya". Kati ya viongozi wa dini, hakuna Askofu hata mmoja wa majimbo yote ya Arusha. Badala yake wapo wawakilishi tu ambao ni wachungaji na mapadri.
Ninachojiuliza ni kwamba, bado wanaendelea na msimamo wao wa kutomtambua "Meya" na kutoshirikiana na Mary Chatanda?
Naomba kuwasilisha.
Ninachojiuliza ni kwamba, bado wanaendelea na msimamo wao wa kutomtambua "Meya" na kutoshirikiana na Mary Chatanda?
Naomba kuwasilisha.