Mengi, Mrema, Msuya, Mwaka na Manara, wote walikosea wakafunga Ndoa badala ya kuoa

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,068
40,730
Sikuwa na lengo ka kuanzisha uzi katika muda mbovu kama huu, ila nimeshindwa kujizuia. Kelele nilizoziona kwa wingi ni juu ya kufunga ndoa au kutokufunga ndoa; lakini je, tunataka watu wafunge ndoa au waoe? Ni kwanini mtu afunge ndoa badala ya kuoa? Au kwanini mtu aoe badala ya kufunga ndoa? Nafafanua hapa kwa marefu na mapana.

-Nitamtolea mfano mzee wetu Dr. Reginald Mengi (R.I.P). Binafsi naelewa maumivu ya ndani kwa ndani aliyokuwa akiyapata kwa kutoletewa wajukuu na watoto wake wote; kuna yule Rodney Mengi, wakati Mola anamwita kwenye makazi ya milele, alikuwa na miaka 30, na kwa mapenzi yake mola hakuacha mtoto. (nasikia tu). Kuna mwingine wanamwita Abdiel Mengi, naambiwa ni over 50yrs, naye hadi Mengi anondoka hakuwa ameleta mjukuu (Nasikia tu).

Na kuna mwingine anaitwa Isabel Mengi nadhani, sijui, ila probably yupo above 40, na hadi Dr.Mengi anaitwa na mola wake, hakuwa ameona mjukuu kwa binti yake (nasikia tu); in such a scenario mtu unaweza kuogopa kizazi chako kufutika huku unajiona mubashara kabisa. Sasa je utakubali?

Mengi akaona isiwe tabu, akamuoa Jackline Mengi ili apte wajukuu ambao pia ni watoto wake (mapacha). Lakini je, alipomuoa Jackline Mengi, kulikuwa na ulazima gani wa kufunga nae ndoa? Kwani angemzalisha na kuishi nae tu kwa umri ule angepungukiwa na nini kikubwa hasa?

Matokea ya kufunga ndoa ndio hayo tumeayaona, kawaishwa pengine mapema zaidi ya muda aliopanga mola (Nasikia tu); na hadi sasa kinachoendelea huko mahakamani ni vita na mateso makali kwa familia yake. Hapa Mengi ilipaswa aoe tu na kulea watoto wake, ila sio kufunga Ndoa! Kataa ndoa!

-Sasa nahamia kwa Mrema masikini ya Mungu, mzee wa watu alishajimalizia yake yote hapa ya duniani, alikuwa anasubiri tu safari yake ya Mwisho; kibaya kilichotokea, alikuja kufunga ndoa na tapeli kabisa, maana alikuwa ni mke wa mtu ambaye alikuwa natumia hina feki la Doreen nadhani, matokeo yake , kawaishwa na kesi ya kugombea mali ipo mahakamani nadhani.., hapa huyu mzee alipaswa kuoa tu, na sio kufunga ndoa, kataa ndoa!

- Haya, Msuya nae, alishamaliza yake yote, ilikuwa ni kujipumzikia na kutafuna totoz at will, nae badala ya kuoa dogodogo wake na kuweka ndani, yeye akafunga ndoa tena ya kanisa! Nae kawaishwa kwa muumba wake, sijajua kama palitokea ugomvi wa mali, jamani, kataa ndoa!

Kuna huyu ndugu yetu mwenye changamoto ya ngozi, Bwana Haji Sunday Manara, alifunga ndoa ya kwanza, ya pili na ya tatu back to back! Hii ya tatu nasikia alioata mshtuki na kuanguka, sasa kama mtu una mke aliyefunga nae ndoa, huyu mwingine ilibidi uoe tu, haoakuwa na haja ya ndoa.., akizingua unaweka pembeni, sasa hapa tusubiri huyu Rushaynah kwenda mahakamani kudai talaka na mgao wa mali, the bi*tch seem so devious! Kataa ndoa!

Haya, hiki sakata ka mwisho ka Ndugu yetu, mganga wa Miti Shamba, Dr. Mwaka Juma Mwaka, alifunga ndoa ya kwanza, ya pili na ya tatu, hii ya Queen imeleta tafrani hadi Watz wote sasa wanaogopa kufunga ndoa, na walio kwenye ndoa wanatetemeka kwa ahili yake, hadi Sheikh mkuu katumbuliwa, at the heart of it all ni nyumba inagombewa, yaani Dokta Mwaka afanye kazi kama mbwa koko kujenga nyumba yake halafu mtu from nowhere aje kudai apewe kiulaini tu, nyie wanawake, hivi hamna huruma,?! Kwanini msijengage zenu ili na sisi wanaume tuje tudai tupewe?! Hamna hata chembe ya huruma kwa jasho la binadamu wenzenu?! Ni binadamu gani msio na huruma nyie! Mungu atawalipa.

=========================
Mbinu hii hapa

 
Back
Top Bottom