Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,429
- 1,045
Katika taarifa ya habari ya juzi usiku, Mzee Mengi aliwataja watu watatu wanaompa ujasiri wa kupambana na ufisadi. Alikuwa akijibu swali juu ya wapi na nani anampa ujasiri. Alimtaja Mwenyezi Mungu, Rais JK na Maskini/wanyonge kuwa ndiyo nguzo za ujasiri wake.
Kati ya nguzo alizotaja nina wasiwasi na ya Rais JK. Lakini jinsi alivyomtega ni vigumu JK kukubali au kukataa hadharani kuwa yeye ni nguzo ya Mzee Mengi.
Eti Wana-JF, mnaonaje kuhusu jibu la Mzee Mengi, JK kweli ni nguzo iliyo upande wa wapinga ufisadi au ni ngao ya adui zetu (mafisadi)?
Kati ya nguzo alizotaja nina wasiwasi na ya Rais JK. Lakini jinsi alivyomtega ni vigumu JK kukubali au kukataa hadharani kuwa yeye ni nguzo ya Mzee Mengi.
Eti Wana-JF, mnaonaje kuhusu jibu la Mzee Mengi, JK kweli ni nguzo iliyo upande wa wapinga ufisadi au ni ngao ya adui zetu (mafisadi)?