Mengi awataja wanaompa kiburi

Hilo ni kanyaboya. Huyu mzee anamtumia JK kama ngao lakini hamaanishi. Kwani huwezi kuwa umezungukwa na mafisadi mpaka kwenye familia harafu wewe usiwe. Unaweza usiwe lakini ukafaidika na matunda ya ufisadi. Hivyo huyu mzee anamtumia kama shield ili asema na jamaa waufyate.

JK kama anadhani kuwa nyota yake inang'ang'aa kachemsha kwa sababu anatumiwa tu.

Mkuu Mugenzi, Mengi hana ubavu wa kumuanika JK hata kama angekuwa na kila ushahidi wa lolote ambalo angeweza kulianika. Mkuu, JK ana immunity, ni kiongozi mkuu wa nchi, Amiri jeshi mkuu wa majeshi yote. Huwezi kwenda public na kumsema hovyo ukaendelea kutesa mtaani.

Mtu yeyote mwenye akili timamu asingeweza kufanya hivyo kwa uwazi kiasi hicho.Mbinu ya kumshirikisha JK katika mapambano haya, yanamuweka Mengi kwenye hali ya usalama zaidi.

Nakumbuka kusikia miaka ya nyuma viongozi wa Afrika walikuwa wakitumiwa delegation (wanapokwenda kinyume na matakwa ya nchi za magharibi) kuambiwa kuwa usalama wao hautakuwa na guarantee. Mkuu Mengi anahitaji guarantee ya usalama wake.
 
Nilichogundua binafsi ni kwamba hakuna mwenye uchungu na nchi hii, kila mtu anafanya kile ambacho kina maslahi kwake, hata Mengi vivyo ivyo. Atawahadaa wananchi wa kawaida ambao uwezo wao wa kufikiri ni mdogo na wanasubiri Mengi afikiri kwa niaba yao. Tunahitaji kuenrol wanafunzi wengi vyuo vikuu ili kuongeza ukubwa wa jeshi la kweli katika mapambano ya kuikomboa nchii toka mikononi mwa wenye fedha na walionunuliwa na wenye fedha. JK, Mengi, RA, Manji, na wengineo wote wapo mafisadi kwa degree na aina tofauti.
 
Shangazi, Igunga ni choka mbaya. Nilikwenda huko week chache zilizopita. Sikuamini kuwa Mbunge wao ndiye FISADI mkuu katika nchi hii. Yaani kule ni umasikini wa hali ya juu ndio unaoonekana dhahiri.


Lakini vipi uliweza kuuliza mtazamo wa wananchi wa Igunga kama wanamuonaje Rostam?
 
waswahili wanasema wapemba hujuwana kwa vilemba,
na mie nasema mafisadi hujuwana kwa ufisadi.
usanii mtupu sie hata mlo mmoja hatupati wao kazi yao kwenda hewani kutuletea hizi pumba.rostam,mengi,serikai ya chama cha mafisadi(ccm)lao moja wanajuwana hao hawapo kwa ajili ya masikini hata siku moja.
 
Naona kuna watu wanaingia ubongoni mwa Mengi na kusema lile analowaza! sijajua kwa stahili hii tutafanya kitu gani observable!

Nasema, kusema kuwa anamsaidia au yuko nyuma ya JK ni kumtukana JK!
 
Nakumbuka ITV ilikuwa ikionyesha picha za mauaji ya Rwanda na wakieleza kuwa wananchi wakichagua upinzani tanzania itakuwa na mauaji kama hayo.

Lakini mi nadhani hapa ilikuwa ni suala la biashara kwa sababu matangazo yale yalikuwa yanalipiwa na CCM

Mkuu Magezi, Mengi sio mtangazaji ingawa anamiliki vyombo vya habari. Lakini kama kumbukumbu zangu ni sahihi, yeye mwenyewe aliongoza hivyo vipindi vya kuwatisha watanzania wasichague wapinzani kwa kisingizio kwamba itatokea vita. Kama ilikuwa ni biashara na CCM ililipia kwanini Mengi ndiye aliendesha hivyo vipindi?

Mengi ni kada wa CCM na hii kelele anayopiga sasa kwamba fulani na fulani ni mafisadi ninahisi ni kwa kuwa hakushirikishwa kwenye hizo deal otherwise anawaunga mkono CCM na mimi ninakuwa na matatizo kumwamini yeyote anayesema anapiga vita ufisadi wakati huo huo ni kada wa CCM.

Kwamba anayempa nguvu Mengi ni JK, siamini la sivyo viranja wa JK wasimgemjia juu mengi alivyowataja marafiki wa JK kwamba ni mafisadi.

Inabidi tufumbuke macho!!!!!!!!
 
Fisadi Mengi apewa kiburi na Mwenyekiti wa Chama cha Mafisadi. Amedhihirisha kuwa he is one of them fisadis. Halafu mnamwita mpiganaji, mpiganaji vita dhidi ya ufisadi.

Kawaruka kweupeee kalaghabaho.


hahahaha KALAGABAHO.....Nimekupata hapa "yaani umeniquote vizuri sana"....
 

Shangazi, Igunga ni choka mbaya. Nilikwenda huko week chache zilizopita. Sikuamini kuwa Mbunge wao ndiye FISADI mkuu katika nchi hii. Yaani kule ni umasikini wa hali ya juu ndio unaoonekana dhahiri.

Shangazi, huo umasikini uliouona Igunga ndio silaha ya rostam kuwa mbunge kule. Akiondoa huo umasikini atakuwa amejimaliza mwenyewe kwani silaha ya hawa jamaa ni umasikini uliopo among wapiga kura. Akimwaga pesa kidogo tu, watu wanampa kula. Kuna msomi mmoja aliwahi kuniambia kwamba CCM na viongozi wote wanaotokana na hicho chama wanajua kuwa silaha yao kubwa ya kuendnelea kubaki madarakani ni kuendelea kuwaacha watanzania walio wengi masikini ili ukifika wakati wa uchaguzi wanagawa kanga, tshirts, kofia, pilau na mchezo unakuwa umekwisha wanachaguliwa tena kwa miaka mitano. Nilikubaliana naye kwani huo ndio ukweli.

Tiba
 
Hapo ndipo anapokosea.JK hawezi kuwa inspiration ya mapambano dhidi ya ufisadi.Instead,yeye ni sehemu muhimu ya ustawi wa mafisadi.

Unachosema mlalahoi na sawasawa, na sina shaka Mengi anaelewa hivyo. Hapo anamtega Mzee mzima JK kwani sote tunajua kuwa Kikwete hawezi kukanusha na kusema "Mengi ni mwongo mimi siongozi vita dhidi ya ufisadi na mafisadi".

Si ulisikia viongozi walio karibu zaidi na Rais (wanamtandao/washkaji) ndio wanaomchokonoa na kumsakama Mengi? Rostam, Masha, Manji, Sophia Simba, etc. bila shaka wana baraka za JK kumsakama Mengi.

Hii inathibitishwa na misimamo inayofanana ya vyombo vya habari kuhusu suala la Mafisadi papa; vya Serikali (TBC, HabariLeo, Daily News), CCM (Uhuru) na Rostam (Mtanzania, Rai) na vijagazeti kadhaa vipya vinavyofadhiliwa na mafisadi.

Hivyo, Mengi kumtaja JK ni ili kupata fursa zaidi ya kutoa mchango wake kwenye vita dhidi ya mafisadi bila kufanyiwa bughudha ya waziwazi. JK anaumia kimyakimya ila anaona soo kukataa sifa feki anayopewa.
 
Katika taarifa ya habari ya juzi usiku, Mzee Mengi aliwataja watu watatu wanaompa ujasiri wa kupambana na ufisadi. Alikuwa akijibu swali juu ya wapi na nani anampa ujasiri. Alimtaja Mwenyezi Mungu, Rais JK na Maskini/wanyonge kuwa ndiyo nguzo za ujasiri wake.

Kati ya nguzo alizotaja nina wasiwasi na ya Rais JK. Lakini jinsi alivyomtega ni vigumu JK kukubali au kukataa hadharani kuwa yeye ni nguzo ya Mzee Mengi.

Eti Wana-JF, mnaonaje kuhusu jibu la Mzee Mengi, JK kweli ni nguzo iliyo upande wa wapinga ufisadi au ni ngao ya adui zetu (mafisadi)?

Huwezi ukapambana na ufisadi ndani TZ iwapo utamuweka rais kwenye kundi la mafisadi. Solution ni kumuweka mbali na mafisadi kwa kumlazimisha kukaa kundi moja na wapinga ufisadi. Kitendo chake cha kukaa kimya, ni kuunga mkono tosha jitihada zinazofanywa na wapinga ufisadi. BTW, ni nani anayefahamu kwa hakika kuwa JK alikuwa akijua kwa hakika chanzo cha pesa za kampeni yake?
 
katika taarifa ya habari ya juzi usiku, mzee mengi aliwataja watu watatu wanaompa ujasiri wa kupambana na ufisadi. Alikuwa akijibu swali juu ya wapi na nani anampa ujasiri. Alimtaja mwenyezi mungu, rais jk na maskini/wanyonge kuwa ndiyo nguzo za ujasiri wake.

kati ya nguzo alizotaja nina wasiwasi na ya rais jk. Lakini jinsi alivyomtega ni vigumu jk kukubali au kukataa hadharani kuwa yeye ni nguzo ya mzee mengi.

eti wana-jf, mnaonaje kuhusu jibu la mzee mengi, jk kweli ni nguzo iliyo upande wa wapinga ufisadi au ni ngao ya adui zetu (mafisadi)?

jakaya kikwete mwenyewe ni fisadi
 
Kama Mengi angejuwa anapewa jeuri na wanyonge basi angewalipa madai wafanyakazi wake wa the Guardian kwanza wapatao 80. Aliomba out of court settlement na kuahidi kuwa angekuwa amewalipa terminal benefits zao mwishoni mwa February 2009. Bwana mengi jisafishe wewe kwanza kabla ya kuona uchafu wa wenzako.
 
Huwezi ukapambana na ufisadi ndani TZ iwapo utamuweka rais kwenye kundi la mafisadi. Solution ni kumuweka mbali na mafisadi kwa kumlazimisha kukaa kundi moja na wapinga ufisadi. Kitendo chake cha kukaa kimya, ni kuunga mkono tosha jitihada zinazofanywa na wapinga ufisadi. BTW, ni nani anayefahamu kwa hakika kuwa JK alikuwa akijua kwa hakika chanzo cha pesa za kampeni yake?

Hiyo bold nimeipenda. Inabidi sasa alazimishwe, apende au asipende
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom