OSOKONI
JF-Expert Member
- Oct 20, 2011
- 10,965
- 5,336
Meli tatu za kivita za Jeshi la Wanamaji kutoka Japani zimewasili nchini na kutia nanga katika Bandari ya Dar es Salaam.
Kuwasili kwa meli hizo kuliambatana na kupigwa mizinga ya baridi 21 huku zikiingia kwa zamu kuanzia saa tatu asubuhi ambapo mpaka kufikia saa nne asubuhi zote zilikuwa zimeshatia nanga.
Meli hizo zilizokuwa zimebeba mabaharia 1,176, zitakuwa nchini kwa ziara ya siku tatu kwa ajili ya mafunzo kwa maafisa waliohitimu mafunzo ya kijeshi.
Kiongozi wa meli hizo, Rear Admiral Hidetoshi Funchnoue, alisema kuwa katika ziara hiyo watafanya mazoezi ya matukio ya dharura katika meli za vita kama vile majanga ya moto na uharibifu wa nchi huku zikiwa bandarini.
Balozi wa Japani hnchini, Masaki Okada, alisema meli hizo zilipaswa kuja mwaka jana wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania.
Kuwasili kwa meli hizo kuliambatana na kupigwa mizinga ya baridi 21 huku zikiingia kwa zamu kuanzia saa tatu asubuhi ambapo mpaka kufikia saa nne asubuhi zote zilikuwa zimeshatia nanga.
Meli hizo zilizokuwa zimebeba mabaharia 1,176, zitakuwa nchini kwa ziara ya siku tatu kwa ajili ya mafunzo kwa maafisa waliohitimu mafunzo ya kijeshi.
Kiongozi wa meli hizo, Rear Admiral Hidetoshi Funchnoue, alisema kuwa katika ziara hiyo watafanya mazoezi ya matukio ya dharura katika meli za vita kama vile majanga ya moto na uharibifu wa nchi huku zikiwa bandarini.
Balozi wa Japani hnchini, Masaki Okada, alisema meli hizo zilipaswa kuja mwaka jana wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania.