Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,183
- 10,920
Wanamgambo wa Houth baada ya kuteka meli yenye inayomilikiwa na kupeperusha bendera ya Israel bado haikukomea hapo kwani juzi kwa mara nyengine walirusha makombora kuelekea Israel.
Kwa bahati mlinzi wa Israel ameweka meli yake ya kivita ya kisasa kwenye bahari nyekundu ambayo ilifanikiwa kuyadaka makombora hayo pamoja na droni.
Hali ni tofauti kule kaskazini ya Israel ambako Iron dome zimeshindwa kazi kuzuia mizinga kutoka Lebanon.
Kule Iraq wanamgambo wengine wameahidi kuingia vitani rasmi na kambi za kijeshi za Marekani zilizopo nchini mwao wakiiona nchi hiyo kama mchokozi kwa kuwadondoshea mabomu mara kwa mara na kuiunga mkono Israel katika kuua raia wa kipalestina kule Gaza.
Kwa bahati mlinzi wa Israel ameweka meli yake ya kivita ya kisasa kwenye bahari nyekundu ambayo ilifanikiwa kuyadaka makombora hayo pamoja na droni.
Hali ni tofauti kule kaskazini ya Israel ambako Iron dome zimeshindwa kazi kuzuia mizinga kutoka Lebanon.
Kule Iraq wanamgambo wengine wameahidi kuingia vitani rasmi na kambi za kijeshi za Marekani zilizopo nchini mwao wakiiona nchi hiyo kama mchokozi kwa kuwadondoshea mabomu mara kwa mara na kuiunga mkono Israel katika kuua raia wa kipalestina kule Gaza.