Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), limewataka wanajeshi wake, kutoshabikia chama chochote cha siasa na badala yake kuwasikiliza wagombea na kumchagua mtu anayejali maslahi ya nchi.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa jeshi hilo nchini, Meja Jenerali , Samwel Kitundu, alipokuwa akifungua Kituo cha Afya cha Makutopora kilichopo Manispaa Dodoma Mjini.
Alisema "Sisi hatuhusiki kwa namna yoyote kushabikia chama chochote cha siasa...siku ya uchaguzi inapofika tunayo nafasi ya kwenda kushiriki kupiga kura kama raia wengine, haya yapo wazi kwetu."
Meja Jenerali Kitundu alisisitiza kuwa asingependa kuona inatokea dosari yoyote kwa mwanajeshi kufanya jambo ambalo ni kinyume cha maagizo hayo.
"Kwa ufahamu wetu tuwe tumewa pima vilivyo (wagombea) kwa hiyo tunapokwenda katika kutimiza wajibu wetu tunakwenda kuchagua kile ambacho tunaamini kwamba kitakuwa kwa maslahi ya nchi yetu," alisema.
Hata hivyo, alisema ni ruksa kwa wanajeshi kwenda kusikiliza mikutano ya kampeni lakini wawe wao binafsi na sio kama jeshi.
Alisema wanapokwenda katika mikutano hiyo wahakikishe wamevaa nguo za kiraia na si sare za jeshi.
Kwa upande wake, Kaimu Mganga wa kituo hicho, Dk. Felister Abdallah, alisema kituo hicho kinakabiliwa na upungufu wa waganga, wauguzi na wataalam wa maabara.
Pia alisema kituo hicho kinakabiliwa na tatizo la usafiri hasa inapotokea wagonjwa kupelekwa katika hospitali za rufaa na hivyo kuomba kupatiwa gari la wagonjwa.
Alisema hivi sasa wamekuwa wakiwapeleka wagonjwa katika hospitali za rufaa kwa kutumia usafiri wa lori.
Naye Kamanda wa Kikosi cha Makutopora, Meja Kapteni Damian Sanga, alisema kuwa kikosi hicho cha 834 KJ, kimefanya ukarabati wa wodi mbili na kujenga wodi mpya ya watoto.
"Majengo hayo pamoja na ukarabati wa jengo moja la nyumba ya Pstaff ambao haujakamilika umefanywa kutokana na fedha za maendeleo zilizotumwa kikosini kwa mwaka 2009/2010," alisema.
Aliongeza kuwa fedha za maendeleo zilizotumwa kwa mwaka huo zilikuwa sh. milioni 98.5.
Aidha, alisema ukarabati wa jengo la utawala na kituo cha ushauri nasaha na upimaji VVU, umefanywa na kampuni ya Farm Access.
Akijibu changamoto hizo, Meja Jenerali, Kitundu, alisema ameyachukua mapungufu wa hayo na kwamba suala la upungufu watendaji muhimu katika kituo hicho ni jambo ambalo watalishughulikia mapema.
Kuhusu gari la wagonjwa, alisema tatizo hilo lipo katika vikosi vyao vingi kwamba kila mwaka watakapopata magari watapeleka katika vikosi ili kupunguza tatizo hilo.
Kituo hicho cha afya mbali ya kuhudumia wanajeshi na familia zao, kimekuwa kikihudumia pia wakazi wa vijiji vya Mchemwa, Veyula, Gawaye, Chihanga, Msalato, Kongogo, Tinai, Mbalawala, Chukikwi na Babayu.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
My Take:
Hivi kwanini Shimbo hakuweza kusema kitu chepesi kama hiki au hadi kuja na mikwara.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa jeshi hilo nchini, Meja Jenerali , Samwel Kitundu, alipokuwa akifungua Kituo cha Afya cha Makutopora kilichopo Manispaa Dodoma Mjini.
Alisema "Sisi hatuhusiki kwa namna yoyote kushabikia chama chochote cha siasa...siku ya uchaguzi inapofika tunayo nafasi ya kwenda kushiriki kupiga kura kama raia wengine, haya yapo wazi kwetu."
Meja Jenerali Kitundu alisisitiza kuwa asingependa kuona inatokea dosari yoyote kwa mwanajeshi kufanya jambo ambalo ni kinyume cha maagizo hayo.
"Kwa ufahamu wetu tuwe tumewa pima vilivyo (wagombea) kwa hiyo tunapokwenda katika kutimiza wajibu wetu tunakwenda kuchagua kile ambacho tunaamini kwamba kitakuwa kwa maslahi ya nchi yetu," alisema.
Hata hivyo, alisema ni ruksa kwa wanajeshi kwenda kusikiliza mikutano ya kampeni lakini wawe wao binafsi na sio kama jeshi.
Alisema wanapokwenda katika mikutano hiyo wahakikishe wamevaa nguo za kiraia na si sare za jeshi.
Kwa upande wake, Kaimu Mganga wa kituo hicho, Dk. Felister Abdallah, alisema kituo hicho kinakabiliwa na upungufu wa waganga, wauguzi na wataalam wa maabara.
Pia alisema kituo hicho kinakabiliwa na tatizo la usafiri hasa inapotokea wagonjwa kupelekwa katika hospitali za rufaa na hivyo kuomba kupatiwa gari la wagonjwa.
Alisema hivi sasa wamekuwa wakiwapeleka wagonjwa katika hospitali za rufaa kwa kutumia usafiri wa lori.
Naye Kamanda wa Kikosi cha Makutopora, Meja Kapteni Damian Sanga, alisema kuwa kikosi hicho cha 834 KJ, kimefanya ukarabati wa wodi mbili na kujenga wodi mpya ya watoto.
"Majengo hayo pamoja na ukarabati wa jengo moja la nyumba ya Pstaff ambao haujakamilika umefanywa kutokana na fedha za maendeleo zilizotumwa kikosini kwa mwaka 2009/2010," alisema.
Aliongeza kuwa fedha za maendeleo zilizotumwa kwa mwaka huo zilikuwa sh. milioni 98.5.
Aidha, alisema ukarabati wa jengo la utawala na kituo cha ushauri nasaha na upimaji VVU, umefanywa na kampuni ya Farm Access.
Akijibu changamoto hizo, Meja Jenerali, Kitundu, alisema ameyachukua mapungufu wa hayo na kwamba suala la upungufu watendaji muhimu katika kituo hicho ni jambo ambalo watalishughulikia mapema.
Kuhusu gari la wagonjwa, alisema tatizo hilo lipo katika vikosi vyao vingi kwamba kila mwaka watakapopata magari watapeleka katika vikosi ili kupunguza tatizo hilo.
Kituo hicho cha afya mbali ya kuhudumia wanajeshi na familia zao, kimekuwa kikihudumia pia wakazi wa vijiji vya Mchemwa, Veyula, Gawaye, Chihanga, Msalato, Kongogo, Tinai, Mbalawala, Chukikwi na Babayu.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
My Take:
Hivi kwanini Shimbo hakuweza kusema kitu chepesi kama hiki au hadi kuja na mikwara.