Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Hii nimekumbana nayo jana pale mtaani kwetu. wakati tukiwa tunasubiri kuangalia mechi ya Man Utd na AC Milan, ghafla nilistushwa na zogo nje ya nyumba ninayoishi. Nilipotoka kujua kulikoni nilishangazwa na nilichokuta. Binti wa kama miaka 23 hivi na namfahamu kwani huwa namuona hapo mtaani, amekunjwa gauni lake na mama mmoja kisa eti alikuwa anawachungulia huyo mama na Mr. wake wakiwa kwenye malovee yao kwa kweli alimkwangua makofi ya hatari... Najua kupiga chabo si jambo geni ingawa kwa ufahamu wangu mara nyingi hufanywa na wanaume/wavulana. Sasa huyu ni binti...Hii imeakaaje jamani...