Mtumwa ni wewe ambaye muda wote unatetea kila kitu CDM wanachokifanya hata kama ni cha kipuuzi. Inabidi mkuu ubadilike, jifunze kuwa na mawazo huru. Kwa stahili hii CDM hawajengi bali wanazidi kubomoa na kujichimbia kaburi lao wenyewe!
Anatafuta umaarufu kwa nguvu sana huyu mchungaji. Badala ya leo kuwa kanisani na kondoo wa bwana, yupo busy anahatarisha amani ya nchi.
Naona sasa ni wakati wa kuwawajibisha viongozi wa aina hii ili iwe fundisho na kwa wengine.
Anatafuta umaarufu kwa nguvu sana huyu mchungaji. Badala ya leo kuwa kanisani na kondoo wa bwana, yupo busy anahatarisha amani ya nchi.
Naona sasa ni wakati wa kuwawajibisha viongozi wa aina hii ili iwe fundisho na kwa wengine.
Hivi chadema hawana njia nyingine ya kupiga siasa zaidi ya kuchochea vurugu na maandamano? Huyu msigwa anataka asikike tu ndio maana anachochea vurugu iringa. Iko siku viongozi wa chadema watavua nguo hadharani ili wasikike kwani hizi vurugu wananchi watazichoka na kutakuwa hakuna njia nyingine ya kuwafanya wasikike.
wanapenda kukamatwa na polisi ili waandikwe magazetini
Mkuu mimi binafsi huyu Msigwa nashindwa kumuelewa
Anafanya vurugu kwa makusudi ili na yeye aandikwe kama yule kubwa jinga wa Arusha.
Anyway, mwisho wake ni 2015 kwani nitahakikisha anarudi kuuza kisosk pale kihesa
Huyu naye ni gaidi tu safi amekamatwa
Taaarifa kutoka Iringa zinasema mbunge wa Jimbo la Iringa Peter Msigwa wa CHADEMA amekamatwa na jeshi la polisi muda huu na yuko chini ya Ulinzi wa jeshi hilo.
Mchungaji Msigwa amekamatwa kwa amri ya Kamanda wa Polisi wa mkoa huo Michael Kamuhanda kwa madai kwamba anawaunga mkono wafanyabiashara ndogondogo wa manispaa hiyo Machinga wanaopambana na polisi wanaowakataza kufanya biashara mjini.
Mchungaji Msigwa amekuwa mtetezi mkubwa wa wafanyabiashara ndogondogo kiasi kwamba kila anapoonekana maeneo ya manispaa hiyo hujikuta gari yake ikisukumwa na Machinga hao.
Itakumbukwa ni wiki iliyopita tu mbunge wa viti maalum Chadema Chiku Abwao alimshambulia vikali Waziri William Lukuvi kwamba analitumia jeshi la polisi Iringa kukandamiza Chadema na viongozi wake.
Mchungaji Msigwa ambaye pia ni mbunge machachari wiki iliyopita ametishiwa na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kufikishwa mahakamani kwamba amemtuhumu kufanya biashara haramu ya pembe za ndovu.
Wabunge wa cdm wasipoangalia wengi wao watapoteza uhai wao kwa kufanya mambo kwa kishabiki bila kufuata taratibu!
Huyu naye ni gaidi tu safi amekamatwa
kwa mafanikio aliyoyapata Msigwa kufikia kutembelea VX mwacheni achachawe maana si mchezo
Mwisho wa siku mchungaji Msigwa atakuwa shujaa mbele ya wanyonge, tatizo lipo wapi kuwaruhusu machinga wapige mzigo siku 2!! Ukizingatia ni week end na serikali itapata mapato kwa kukusanya ushuru.