Sasha Fierce
JF-Expert Member
- Feb 7, 2009
- 361
- 5
Mwenyekiti wa chama cha Democratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila, leo aligeuka kioja baada ya kutinga katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam, akiwa amenyuka suti kali na tai lakini miguuni akiwa amevaa kiatu kimoja cheusi na kandambili nyekundi huku akitembelea mkongojo.Hali hiyo iliibua kimbembe Mahakamani hapo kiasi cha kuwafanya watu kusahau hata kufuatilia kesi kubwa ya ufisadi inayowakabili Yona, Mgonja na Mamba.Akionekana hana tyme na mtu, Mtikila alitinga hadi katika chumba cha mawakili na kuwasabahi Yona, Mramba na Mgonja.
Mwandishi aliamua kumstopisha Mwanasiasa huyo mkongwe na kumuuliza kulikoni alikuwa ameripuka kwa staili hiyo, ambapo alijibu kuwa mnamo Februari 16 akiwa nchini Zimbabwe alivamiwa ndani na Joka kubwa aina ya Kobra ambalo lilimgata mguu, lakini hakuweza kupata matibabu kwa siku tatu ingawa alikuwa anakesha na kuomba.Wakati mtandao huu ulipokuwa ukichonga na Mtikila watu kibao wakiwemo mawakili, walikuwa wamemzunguka wakimshangaa ikiwa ni pamoja na kucheka, lakini hali watu walizidi kuvunja mbavu baada ya kueleza kuwa alikaa siku tatu bila matibabu na alipona bila kutibiwa .
Du! Mchungaji huyu kwa kamba Fix hajambo, inawezekaba vipi mtu ukapona baada ya kungatwa na Kobra mwenye sumu kali bila matibabu? Labda alingatwa na nge, maana Kobra ni masaa machache tu mtu anavutaalisikika kijana mmoja akisema.