Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,969
- 22,161
MMOMONYOKO wa maadili unaelekea kuiathiri jamii ambapo sasa baadhi ya viongozi wa dini wanazidi kuingia matatani kutokana na kushiriki katika vitendo vya ngono.
Mchungaji wa kanisa la African Inland- (AIC) ambaye pia ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Chona, wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Pasia Dickson (36), ametuhumiwa kufumaniwa Jumatano akifanya mapenzi na mwanafunzi wa darasa la saba.
Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Daudi Siasi amethibitisha tukio hilo akisema kwamba, mtuhumiwa ameshatiwa mbaroni na amefikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kubaka na kushambulia.
Siku ya tukio mwalimu huyo alikwenda nyumbani kwa mwanafunzi huyo na kufanya naye tendo la ndoa chumbani kwa mama wa mwanafunzi, ambaye wakati wa tukio hilo alikuwa amekwenda gulioni kununua mahitaji ya nyumbani.
Naye Diwani wa Kata ya Chona iliyopo umbali wa kilomita zaidi ya 50 kutoka Kahama Mjini, Mabala Mlolwa amesimulia tukio akisema kwamba, alishiriki kwa kiasi kikubwa katika kuyaokoa maisha ya mchungaji huyo.
Ni tukio la kweli, na mimi nimeshiriki katika kumnusuru kwa sababu baada ya fumanizi alijiokoa kwa kumngata kaka wa binti na baadaye alitimua mbio akiwa mtupu hadi kwenye ghala la kuhifadhia nafaka katika nyumba ya jirani. Wananchi wenye hasira walitaka kummaliza huko huko ghalani, nikawasihi wasubiri polisi na kweli baadaye polisi walikuja kumchukua, mimi ndiye niliyemchukulia nguo, na sasa wanamshikilia
Mashuhuda wa tukio hilo wanaeleza kwamba, Mchungaji huyo alikuwa na uhusiano wa muda mrefu na mwanafunzi huyo. Hata siku ya tukio, jamaa alikwenda akijua kabisa ratiba ya mama wa mwanafunzi, bila woga alikwenda na pikipiki akaiegesha nje naye kuzama ndani na hawara yake
Kaka mtu ndiye aliyeshitukia mchezo mchafu wa mchungaji, kwani alipofika nyumbani alishangaa kuona pikipiki nje, baada ya kuingia ndani alimkuta mchungaji huyo katika kitanda cha mama yao akiwa utupu wakifanya mapenzi na mdogo wake mwenye umri wa miaka 16.
Ndipo katika kukurupushana huku mchungaji akitaka kutoka akiwa utupu na kaka mtu akijitahidi kumzuia kutoka huku akipiga kelele, mchungaji aliamua kumngata kaka mtu na kukimbia, lakini hakufika mbali kwa sababu hakuwa na nguo, alisema Mlolwa. Kesi ya Mchungaji Dickson inatarajiwa kuendelea Aprili 30, mwaka huu.
Mchungaji wa kanisa la African Inland- (AIC) ambaye pia ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Chona, wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Pasia Dickson (36), ametuhumiwa kufumaniwa Jumatano akifanya mapenzi na mwanafunzi wa darasa la saba.
Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Daudi Siasi amethibitisha tukio hilo akisema kwamba, mtuhumiwa ameshatiwa mbaroni na amefikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kubaka na kushambulia.
Siku ya tukio mwalimu huyo alikwenda nyumbani kwa mwanafunzi huyo na kufanya naye tendo la ndoa chumbani kwa mama wa mwanafunzi, ambaye wakati wa tukio hilo alikuwa amekwenda gulioni kununua mahitaji ya nyumbani.
Naye Diwani wa Kata ya Chona iliyopo umbali wa kilomita zaidi ya 50 kutoka Kahama Mjini, Mabala Mlolwa amesimulia tukio akisema kwamba, alishiriki kwa kiasi kikubwa katika kuyaokoa maisha ya mchungaji huyo.
Ni tukio la kweli, na mimi nimeshiriki katika kumnusuru kwa sababu baada ya fumanizi alijiokoa kwa kumngata kaka wa binti na baadaye alitimua mbio akiwa mtupu hadi kwenye ghala la kuhifadhia nafaka katika nyumba ya jirani. Wananchi wenye hasira walitaka kummaliza huko huko ghalani, nikawasihi wasubiri polisi na kweli baadaye polisi walikuja kumchukua, mimi ndiye niliyemchukulia nguo, na sasa wanamshikilia
Mashuhuda wa tukio hilo wanaeleza kwamba, Mchungaji huyo alikuwa na uhusiano wa muda mrefu na mwanafunzi huyo. Hata siku ya tukio, jamaa alikwenda akijua kabisa ratiba ya mama wa mwanafunzi, bila woga alikwenda na pikipiki akaiegesha nje naye kuzama ndani na hawara yake
Kaka mtu ndiye aliyeshitukia mchezo mchafu wa mchungaji, kwani alipofika nyumbani alishangaa kuona pikipiki nje, baada ya kuingia ndani alimkuta mchungaji huyo katika kitanda cha mama yao akiwa utupu wakifanya mapenzi na mdogo wake mwenye umri wa miaka 16.
Ndipo katika kukurupushana huku mchungaji akitaka kutoka akiwa utupu na kaka mtu akijitahidi kumzuia kutoka huku akipiga kelele, mchungaji aliamua kumngata kaka mtu na kukimbia, lakini hakufika mbali kwa sababu hakuwa na nguo, alisema Mlolwa. Kesi ya Mchungaji Dickson inatarajiwa kuendelea Aprili 30, mwaka huu.