Mchungaji Aibuka na Kikombe. Ruvu Darajani nao wakumbukwa

Nyenyere

JF-Expert Member
Sep 9, 2010
14,770
10,650
Gazeti la majira la leo limeripoti habari hizi. Anaitwa mchungaji Kennedy Mwasomola wa kanisa la mitume wapya kusanyiko la Tukuyu mjini. Ameoteshwa na Mungu mti na majani yake yanayotibu magonjwa sugu baada ya kuchemsha na kunywa kikombe. Aliota yuko kwenye foleni ya babu Loliondo. Alipokaribia kufika kupata kikombe akagundua kuwa hana hela (500). Akatoka kwenye foleni na kusimama pembeni. Ndipo akaona umbo mithili ya malaika. Akamponya uvimbe mkononi. Akamchukua mpaka kwenye mti uitwao mpandapanda. Akamwambia, " kwa kuwa wewe ni mwenyeji mwombe mzee mwenye mti huo uitwao mpandapanda ili ukatwe kwa ajili ya dawa." Mzee huyo akakubali kutoa mti bila kinyongo. Ndipo mchungaji akaamka. Akautafuta mti huo na ameshaanza kugawa dozi ya kikombe. Zaidi ya watu 2000 tayari wamekunywa. Anasema ameonyeshwa kuwa ni tawi la babu wa Loliondo.

Mwingine ni John Agunda mkazi wa Ruvu Darajani. Kaoteshwa na malaika. Ameshatoa tiba kwa zaidi ya watu 100. Hatozi hata senti moja. Haulizi mtu anaumwa nini. Ukienda kwa imani tu utapona.
 
Sikujua watanzania wanaamini ndoto kwa kiasi hicho. Na zaidi sikujua watz ni wacha Mungu hivyo. Yaani mtu akisema tu ameoteshwa ndoto inatosha sana kuamini. Sasa naamini kuwa kwa "IMANI" tuko juu
 
ndugu zangu watanzania napata mashaka na wote wanaodai kuoteshwa. Kwanini wote wanaoota wawe wa asili ya Mbeya? Mwasapila, mwasomola,etc wote hawa ni asili ya Mbeya, Tafakarini kwa makini sana kabla ya kwenda kunywa hivyo vikombe. Huenda ni siku za mwisho, naombeni mlio wakristo mrejee maandiko matakatibu yalivyotabiri kuwa siku za mwisho kila mmoja atadai ni nabii. Hebu anayejiamini kwamba alipima kuwa na ukimwi na alipoenda Loliondo sasa amepima na kupewa cheti kuwa kapona atupe ushuhuda. Jamani rudini katika maandiko matakatifu hizo ni dalili za siku ya mwisho. Hata wanaooteshwa hawajui kuwa wanatimiza unabii kwasababu imeandikwa lazima itimie.
 
Unaweza ota umejenga angani!
Anganiiiiiiiiiiiiiii kuhifadhi ndoto ya kazi ganiiiiiiiiiiiiiiiii?weweeeeeeeeeeeeeee!!! anyway kama zinauwezo wa kuponya we have to thank God kwa mi magic healing aliotuoteshea bana hehehehehehe!!!!!!
 
Loliondo, Mabatini, Tarakea, Tabora, Tukuyu, Ruvu... nadhani kesho na mtondo itakuwa Ikulu ya Magogoni!
 
Hii ni shida sasa kila siku kuoteshwa ina maana Tz pekee ndiyo ina wagojwa? kuna watu wanataka kujinufaisha kupitia mgongo wa imani.
 
Mwasomola, Mnyakyusa mwingine tabibu wa kikombe.
Atakuja Mwakiswalele naye ataanza kutibu kwa bluetooth
 
Gazeti la majira la leo limeripoti habari hizi. Anaitwa mchungaji Kennedy Mwasomola wa kanisa la mitume wapya kusanyiko la Tukuyu mjini. Ameoteshwa na Mungu mti na majani yake yanayotibu magonjwa sugu baada ya kuchemsha na kunywa kikombe. Aliota yuko kwenye foleni ya babu Loliondo. Alipokaribia kufika kupata kikombe akagundua kuwa hana hela (500). Akatoka kwenye foleni na kusimama pembeni. Ndipo akaona umbo mithili ya malaika. Akamponya uvimbe mkononi. Akamchukua mpaka kwenye mti uitwao mpandapanda. Akamwambia, " kwa kuwa wewe ni mwenyeji mwombe mzee mwenye mti huo uitwao mpandapanda ili ukatwe kwa ajili ya dawa." Mzee huyo akakubali kutoa mti bila kinyongo. Ndipo mchungaji akaamka. Akautafuta mti huo na ameshaanza kugawa dozi ya kikombe. Zaidi ya watu 2000 tayari wamekunywa. Anasema ameonyeshwa kuwa ni tawi la babu wa Loliondo.

Mwingine ni John Agunda mkazi wa Ruvu Darajani. Kaoteshwa na malaika. Ameshatoa tiba kwa zaidi ya watu 100. Hatozi hata senti moja. Haulizi mtu anaumwa nini. Ukienda kwa imani tu utapona.

Kwa anayetaka kupata habari za siku nyingi za huyo John Agunda na atempt nyingi alizowahi kufanya ili 'atoke' aende eneo linaloitwa Mbezi Msakuzi. Wazee wa sikunyingi wa hapo wanamjua inside out!.
 
Safina ya NUHU yaja soon.Desperateness ni mbaya. watanzania wengin wameshindwa kwenda Nigeria kuchukua annointing water kwa sababu inaitaji process nyingingi sana. Mchukue babu loriondo mpleke Uingereza uone kama kuna mtu atajairbu au kuthubutu. Hii inaonyesha tumeshakata tamaa za maisha, kutwa tunakimbizana na mambo ya ulimwengu, hatumjui Mungu.

Sorry kama nitawakwaza; tulioo hapa nani anasoma walau kila siku iendayo kwa Mungu verse kwenye biblia au Msahafu (qoran). Hiyo imani haba ya kukubali vikombe bila kufikiria inatoka wapi wakati hata kusoma kitabu cha mwenyezi mungu ni mgogoro? Tuombee wananchi watanzania kama ni siumu nafikiri nchii itakuwa makaburi mengi sana.

Nisameheni kama nimewaudhi, ni mtu tu!
 
Caroline Danzi, hapa umenikuna. Mimi nimsikilizaji mzuri sana wa sauti kutoka dunia nyingine, Biblia naisoma vizuri na kuielewa sana. naweza isoma hata 5 times per day at no interval. hasa nikisikia nenda kasali, hujua kuna msg. Jambo la HIV tukiwa ktk maombi ya wanawake wa Tanzania mwaka 2002 Nov, kuna mwombaji mmoja aliitunyamazisha na kusema haya,"msiombe juu ya HIV tena, Tanzania, kwani nimeisha itoa dawa yake!!!" Sasa ndo najionea baada ya miaka 9. Nilipouliza ktk kusali ni nini maana ya utitiri wa vikombe jibu lilikuwa ni manabii wa uongo!! Lakini ninayemwona ktk maombi na hata nikilala ni mtu mzee na ambaye nimekuwa nikimwona kwa takriba miaka saba hivi, hasa mwaka 2009 na hata jana usiku I saw this oldman in my visions. Kazi kwenu. WENGI WATAKUJA KWA JINA LANGU NA WATAWAPONYA WENGI NA WATAFANYA MAAJABU MENGI, BUT MSIWAFUATE NA ISHARA YA KUWAJUA NDIZO HIZI......na wewe katafute biblia usome usijali dini.
 
Kweli ni rahisi sana kuibia watu waliokata tamaa....:bored:!!!
Sio kukata tamaa, lile fungu la ' watu wangu wanangamia kwa kukosa maarifa' linatimia. Leo hi unawaona wana ibiwa kesho, usipo kuwa makini, na wewe utaibiwa. Shetani anafanya miugiza ya ajabu kuliko wowote. Usalama wako na wangu, Tusome Maandiko na tuukubali ukweli kama ulivyo kwenye Biblia. au sio hivyo tukiuakata, 2 Thess 2:9-11 inaeleza kitakachotokea. ( 9Even him, whose coming is after the working of Satan with all power and signs and lying wonders, 10And with all deceivableness of unrighteousness in them that perish; because they received not the love of the truth, that they might be saved. 11And for this cause God shall send them strong delusion, that they should believe a lie)
 
Caroline Danzi, hapa umenikuna. Mimi nimsikilizaji mzuri sana wa sauti kutoka dunia nyingine, Biblia naisoma vizuri na kuielewa sana. naweza isoma hata 5 times per day at no interval. hasa nikisikia nenda kasali, hujua kuna msg. Jambo la HIV tukiwa ktk maombi ya wanawake wa Tanzania mwaka 2002 Nov, kuna mwombaji mmoja aliitunyamazisha na kusema haya,"msiombe juu ya HIV tena, Tanzania, kwani nimeisha itoa dawa yake!!!"[/COLOR] Sasa ndo najionea baada ya miaka 9. Nilipouliza ktk kusali ni nini maana ya utitiri wa vikombe jibu lilikuwa ni manabii wa uongo!! Lakini ninayemwona ktk maombi na hata nikilala ni mtu mzee na ambaye nimekuwa nikimwona kwa takriba miaka saba hivi, hasa mwaka 2009 na hata jana usiku I saw this oldman in my visions. Kazi kwenu. WENGI WATAKUJA KWA JINA LANGU NA WATAWAPONYA WENGI NA WATAFANYA MAAJABU MENGI, BUT MSIWAFUATE NA ISHARA YA KUWAJUA NDIZO HIZI......na wewe katafute biblia usome usijali dini.


Naomba msaada, 'Sauti kutoka dunia Nyingine'; What do u exactly mean?
Ukwimi dawa yake nini na ipo wapi?
Nabi wa uongo utamjuaje?
Ashante
 
Hii, inaonyesha kuwa wa TZ wameshindwa maisha,,,na wamekata tamaa kutokana na matatizo waliyonayo.
na hii ni hatali sana kwa Taifa zima,, iweje kila siku kunaibuka kikombe na watu bado hawasikii na wala hawaelewi nini kinaendelea,,
Je? hii si dalili za watanzania kukata tamaa?

Mungu iepusha TZ na hili balaa.
 
Hii ni shida sasa kila siku kuoteshwa ina maana Tz pekee ndiyo ina wagojwa? kuna watu wanataka kujinufaisha kupitia mgongo wa imani.
Kuna jambo linaendelea hapa, sio tanzania tu. Hebu Fikiria what's going on in the Arab world, events in Japan, in the U.SA. (spiritualism/medium at its peak amongst others ), economic uncertenities in Europe yaani kila sehemu kuna vitu which occupy peoples' minds and draw them away from their Creater!
Kuna Vita inaendelea na ni vita ya Kiroho. You are either for Christ or for the devil hakuna uwanja wa katikati

Rev 14: 7 'Fear God, and give glory to him; for the hour of his judgment is come: and worship him that made heaven, and earth, and the sea, and the fountains of waters.
 
Back
Top Bottom