Mchakato wa kurejesha mali za CCM kwa wananchi

lukindo

JF-Expert Member
Mar 20, 2010
8,466
9,028
Nawasalimuni

Ni wazi kuwa hakuna hata Mtanzania mmoja anayekubali na atakayekubali kuwa mali wanazomiliki Chama Cha Mapinduzi - CCM ni halali yao. Hii ni kwa hata CCM wenyewe pale wanapotakiwa kueleza ukweli juu ya mali hizo.

Kwa kifupi ni kuwa mali nyingi kama sio zote zilipatikana kwa nguvu ya wananchi (umma), na kwa vile kulikuwa hakuna vyama vingi hata mtu asie na chama ilimpasa kuchangia na hii inaeleweka kwa kila mmoja wetu. (Mwenye mawazo tofauti katika hili tunaomba atufafanulie)

Jinsi gani ziliangukia mikononi mwa chama?
Kwa vile mali nyingi zilipaswa kusimamiwa kama tunavyofahamu na halmashauri, manispaa au jiji na hizi taasisi zilitumika kuwakilisha wananchi maana serikari isingweweza kusimamia moja kwa moja. Hivyo ilikuwa ni sawa kupitia taasisi hizi kuwa wasimamizi wa mali husika kwa niaba ya wananchi.

Kwanini zirudishwe kwa wananchi sasa?

Tumeshuhudia kwa miaka ya karibuni kuwa umeingia mgawanyiko na ubinafsi wa hali ya juu katika chama hiki kikongwe ambao unahatarisha usalama wa mali hizi za wananchi (sio za CCM kumbuka). Mfano wa karibuni ni jengo la makao makuu ya Umoja wa Vijana ambapo sasa litamilikiwa na watu wachache katika mkataba tata kama CCM wenyewe walivyoainisha. Huu ni mfano mmoja kati ya mamia ya jinsi tunavyokaribia kupoteza urithi wa nchi waziwazi.

Ili kunusuru mali hizi tuanze na viwanja kama KIRUMBA wa Mwanza na SHEIKH ABEID wa Arusha virejeshwa kwa Harmashauri husika ili waviendeleze. (Nasema hizi sehemu mbili kama sample tu). Hilo ni pendekezo la jinsi ya umiliki wa mali hizi unavyoweza kuwa, yaani chini ya Halmashauri husika. Ikiangukia CCM, CUF, NCCR, TLP, CDM nk ndiyo wawe na jukumu la usimamizi kwa 'sense' ya uwakilihi wa wananchi. Pia tunaweza kupitia report ya Jaji Nyalali ili kuwa na uhakika wa jinsi walivyoliona ili suala.

Tahadhali:
Kuchelewa kuchukua hatua kunaweza kupotezea taifa vitu vya msingi na thamani, wananchi wake pamoja na vizazi vijavyo. Sidhani kama anaweza kusimama mtu sasa hivi ndani ya CCM na kutuhakikishia (katika hali ya uungwana, uzalendo na ukweli) usalama wa mali hizi.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI DUNIA

Nawakilisha
 
Utahangaika sana na believe me your work or plan even your idea is irrelevant!

CCM nao watatudai vya kwao; watadaienzi za zidumu fikra za mwenyekiti wa chama, watadai wakati zinachukuliwa tulikuwa wapi, watadai ujamaa na kujitegemea! watadai kila kitu......

Mwisho utadai kwa nini ulizaliwa na baba mweusi, na utadai kwa nini rais wa kwanza alikuwa Nyerere! utadai na utadaiwa tu

Kuna kitu kimoja naamini na kimetangazwa ni mali ya woote na yeyote akitakaye nacho ni top kuliko kirumba stadium n.k NACHO NI IKULU!!

IKULU is free for everyone na our goal is to reach there, tukifanikiwa kuiondoa CCM magogoni what is kirumba anyway??

Yaani tukipiga ikulu vingine vitajkiachia vyenyewe!! we should be strategic
 
ushahidi upo tosha mfano uwanja wa majimaji songea, watu walijitolea pale kufyatua tofali kwa wanaume wanawake walichota saaana maji pale. my mother in law alikuwa mwalimu kijiji flani kinaitwa maposeni walikuwa wakija songea town kila weekends kuchota maji kwa ajili ya ujenzi wa ule uwanja. kuna kitabu flani hivi sikikumbuki jina lkn kuna picha ya my dad, mkuu wa mkoa wakati ule Gama, mwl Nyerere na viongozi kibao wa mkoa wakikagua ujenzi wa uwanja. ilikuws ni amri kila kijana kwenda kufanya kazi ya ujenzi pale ingawa kwa ngazi ya kitaifa ilijulikana ni kujitolea so uwanja ulijengwa na wananchi wooote na si ccm peke yao.
Uwanja wa ally hassan mwinnyi tabora nao wananchi walijitolea pale na bidhaa zikaongezwa kodi ili kuchangia uwanja sidhani km wana ccm peke yao ndo waliolipia hizo kodi tuu. Viwanja hivyo ni nguvu ya wananchi na si ccm virudishwe kwa wananchi as soon as possible.
 
Utahangaika sana na believe me your work or plan even your idea is irrelevant!

CCM nao watatudai vya kwao; watadaienzi za zidumu fikra za mwenyekiti wa chama, watadai wakati zinachukuliwa tulikuwa wapi, watadai ujamaa na kujitegemea! watadai kila kitu......

Mwisho utadai kwa nini ulizaliwa na baba mweusi, na utadai kwa nini rais wa kwanza alikuwa Nyerere! utadai na utadaiwa tu

Kuna kitu kimoja naamini na kimetangazwa ni mali ya woote na yeyote akitakaye nacho ni top kuliko kirumba stadium n.k NACHO NI IKULU!!

IKULU is free for everyone na our goal is to reach there, tukifanikiwa kuiondoa CCM magogoni what is kirumba anyway??


Yaani tukipiga ikulu vingine vitajkiachia vyenyewe!! we should be strategic
umeupa mjadala huu nguvu zaidi ya ulivyoanzishwa. Hivyo mnaona wakati mikakati ya kuingia huko inafanyika kuna faida nyingi sana zinazopatikana kama ikifanikiwa na kila mtu inabidi kuona hilo badala ya unafiki, woga na porojo. Nimetoa uwanja wa Kirumba kama mfano maana sasa badala ya watu wa Mwanza kukarabati uwanja kwa faida ya hapo na maeneo jirani wanasubiri 'wakulu' kutoka RUMUMBA - DSM kufanya hivyo! Watu wenyewe sasa wamejaa Ukabila, udini, ubinafsi na kukosa uzalendo!
 
ile movement ya cdm moshi kurudisha maeneo ya wananchi imefikia wapi?:A S-coffee:
 
Hivyo viwanja vya CCM Kirumba Sheikh Amri Abeid n.k achana navyo hivyo vilijengwa enzi ya mfumo wa chama kimoja yaani TANU na baadae CCM, sasa kwa wale wanaifahamu Moshi vizuri mahali ilipo ofisi ya CCM wilaya karibu na Stend ya basi ipo Nyumba iliyokuwa Ofisi za serikali ya mkoloni tena mjerumani hata ule mtego uliotumika kunyongea watu walioipinga serikali ya Mjerumani upo hadi leo sehemu ya historia CCM wameichukua bila aibu na wanadai ni yao.AIBU KUBWA ikijengwa hiyo nyumba wakati huo hata CCM,TANU, na hao wanaodai ni yao walikuwa hata hawajulikani kama watazaliwa pengine hata babu zao,LEO WANADAI NI MALI YAO HIVI VICHWA VYAO VINAFIKIRIAJE?.NI HATARI SANA LAKINI SALAMA.
 
Utahangaika sana na believe me your work or plan even your idea is irrelevant!

CCM nao watatudai vya kwao; watadaienzi za zidumu fikra za mwenyekiti wa chama, watadai wakati zinachukuliwa tulikuwa wapi, watadai ujamaa na kujitegemea! watadai kila kitu......

Mwisho utadai kwa nini ulizaliwa na baba mweusi, na utadai kwa nini rais wa kwanza alikuwa Nyerere! utadai na utadaiwa tu

Kuna kitu kimoja naamini na kimetangazwa ni mali ya woote na yeyote akitakaye nacho ni top kuliko kirumba stadium n.k NACHO NI IKULU!!

IKULU is free for everyone na our goal is to reach there, tukifanikiwa kuiondoa CCM magogoni what is kirumba anyway??

Yaani tukipiga ikulu vingine vitajkiachia vyenyewe!! we should be strategic

ni nani kasema IKULU is for everyone?watanzania mil.40 wote wataenda/watapitia ikulu? kilumba could be for every one maana mfano viktokea vfo mwanza eg MV BK watu waweza kukusanywa pale as for G/Mboto in UHURU..kwa mantiki hii jamii inajivunia viwanja hivi kwa mambo mengi..lakini leo wangapi wanaitaka Ikulu,na wangapi wamekufa bila hata kuiona Ikulu? tofautisha kati ya(viwanja) Resources na IKULU (Abstract entity)
 
Ni swala la muda tuu. Ukweli ni kwamba siku ya CCM kuondoka Ikulu ndio mwanzo wa mambo mengi kuwekwa sawa. Mali hizo ni kidogo sana na mimi sioni uharaka wake. Kuna swala zito la kurekebisha national na social fabric ( yaani kurekebisha ule mtazamo wa Utanzania ) Watu sasa hivi wanafikiria kuiba tuu, kuishi maisha bora bila kufanyakazi; wezi, wauza unga na wale waliofanikiwa kimaisha kwa njia haramu wanapewa heshima na kuheshimika ndani ya jamii. Wale waadilifu, wachapa kazi, wanaokataa rushwa wanachekwa na jamii na kuonekana wajinga. HAPO NDIPO WATANZANIA WALIPO KWA SASA. Kwa hali hii ni vigumu kwa maendeleo ya kweli na ya haki kufikiwa na jamii iliyooza kiasi hicho. Ni lazima tujisafishe kwanza sisi kama jamii ili kuleta mtazamao mpya ndani ya nchi.

Tunahitaji "Cultural Revolution" kama ile ya wachina ili kusafisha maovu yote. Tutarudi hatua moja nyuma lakini tutapiga mbili mbele na kusonga mbele kimaendeleo. Huwezi kuwa na taifa ambalo vijana wake "wanataka wapishwe ile nao wale".

Kwa hiyo Kirumba, Amri Abeid kwangu mimi sio kipaumbele sana. Na hofia mustakabali wa nchi kama nilivyoeleza hapo juu. Mimi naona tunalo tatizo kubwa katika jamii. Yaani kule kuyeyuka kwa maadili kiasi kwamba maovu yakaonekana kama ndio sahihi. Hii ni hatari kubwa sana kwa Taifa. Leo hii ukiaanza kuhoji utajiri mkubwa walionao baadhi ya wanasiasa wetu unaonekana kama adui, hufai na utaandamwa sana. Tufikie mahali nchi yetu iheshimike kwa maadili mema ya watu na viongozi wake. Sasa hivi wakati mwingine unaona aibu kuitwa Mtanzania. Mara Dowans, Mara Kiwira, mara Rushwa, mara wachuna ngozi, mara Albino, mara wabakaji vitoto, nk. AIBU TUPU.
 
ni nani kasema IKULU is for everyone?watanzania mil.40 wote wataenda/watapitia ikulu? kilumba could be for every one maana mfano viktokea vfo mwanza eg MV BK watu waweza kukusanywa pale as for G/Mboto in UHURU..kwa mantiki hii jamii inajivunia viwanja hivi kwa mambo mengi..lakini leo wangapi wanaitaka Ikulu,na wangapi wamekufa bila hata kuiona Ikulu? tofautisha kati ya(viwanja) Resources na IKULU (Abstract entity)
point ni kuwa ikikamatwa ikulu, maeneo mengi yaliyosawa na Kilumba yatabainishwa na wananchi (kwa ujumla wao bila kujali rangi, dini, kabila, chama) pasipo na masharti wataona fahari ya matunda yao na kuyaendeleza
 
Ni swala la muda tuu. Ukweli ni kwamba siku ya CCM kuondoka Ikulu ndio mwanzo wa mambo mengi kuwekwa sawa. Mali hizo ni kidogo sana na mimi sioni uharaka wake. Kuna swala zito la kurekebisha national na social fabric ( yaani kurekebisha ule mtazamo wa Utanzania ) Watu sasa hivi wanafikiria kuiba tuu, kuishi maisha bora bila kufanyakazi; wezi, wauza unga na wale waliofanikiwa kimaisha kwa njia haramu wanapewa heshima na kuheshimika ndani ya jamii. Wale waadilifu, wachapa kazi, wanaokataa rushwa wanachekwa na jamii na kuonekana wajinga. HAPO NDIPO WATANZANIA WALIPO KWA SASA. Kwa hali hii ni vigumu kwa maendeleo ya kweli na ya haki kufikiwa na jamii iliyooza kiasi hicho. Ni lazima tujisafishe kwanza sisi kama jamii ili kuleta mtazamao mpya ndani ya nchi.

Tunahitaji "Cultural Revolution" kama ile ya wachina ili kusafisha maovu yote. Tutarudi hatua moja nyuma lakini tutapiga mbili mbele na kusonga mbele kimaendeleo. Huwezi kuwa na taifa ambalo vijana wake "wanataka wapishwe ile nao wale".

Kwa hiyo Kirumba, Amri Abeid kwangu mimi sio kipaumbele sana. Na hofia mustakabali wa nchi kama nilivyoeleza hapo juu. Mimi naona tunalo tatizo kubwa katika jamii. Yaani kule kuyeyuka kwa maadili kiasi kwamba maovu yakaonekana kama ndio sahihi. Hii ni hatari kubwa sana kwa Taifa. Leo hii ukiaanza kuhoji utajiri mkubwa walionao baadhi ya wanasiasa wetu unaonekana kama adui, hufai na utaandamwa sana. Tufikie mahali nchi yetu iheshimike kwa maadili mema ya watu na viongozi wake. Sasa hivi wakati mwingine unaona aibu kuitwa Mtanzania. Mara Dowans, Mara Kiwira, mara Rushwa, mara wachuna ngozi, mara Albino, mara wabakaji vitoto, nk. AIBU TUPU.
Kirumba na Amri Abeid imetolewa kama sample, tatizo liko kwenye nani wa kuamua ili kufanya hiyo 'cultural revolution'! Juzi tu Kenya walivyofanya mabadioliko ya katiba hakuna aliyefikiri kuwa Mzee Kibaki angeteua maofisa wa juu lakini umma ukakataa kupitia bunge. HIYO NI HATUA MBELE, hapa ni kujaribu kukomesha/kupunguza jeuri ya baadhi ya watendaji lakini safari ni ndefu. Au basi tupatie pa kuanzia (program of action/implementation)
 
Ni swala la muda na ni vizuri watanzania tukakumbushana na kuibua mijadala kama hii ili hata wale ambao kizazi chao hakikuweza kupata uwepo wa chama kushika hatamu wafahamu na watambue majukumu na haki zao za msingi mbele ya safari.

My Take:
Inaweza ikawa kesho, au baada ya miaka 10, 15,20 au 50, la maana hapa ni kwamba ipo siku mali hizi zote zilizotajwa zitarudi mikononi mwa serikali na sio chama.
Hii imetokea sehemu nyingi duniani na kwa ukaribu kabisa ni Kenya, Zambia na hata Malawi.
KANU imenyanganywa Jengo zuri na lilokuwa linawaingizia pesa kama kitega uchumi, ghorofa refu na limerudishwa serikali kuu.

Ukweli ni kwamba( hata CCM wanajua). Majengo na miundombinu yote iliyojengwa kwa ajili ya umma ilisimamiwa na CCM lakini kwa nguvu na kujitolea kwa Watanzania wote ( wakubwa kwa watoto, akinamama, vijana na wazee)
Viwanja vya Ilulu - Lindi, Sokoine- Mbeya, Umoja- Mtwara, Jamhuri - Morogoro, Lake Tanganyika - Kigoma, Kaitaba-Kagera,na karibu viwanjwa vyote vilivyopo mikoani vilijengwa kwa kujitolea.
Wafanyakazi walikuwa wakienda kupata huduma makao makuu hawahudumiwi hadi wamejotolea kujenga kati ya siku mbili hadi tatu, wanafunzi walikuwa ndio vibarua, wakulima na wafanyakazi walichanga mahindi, kunde, mbaazi, na kila aina ya michango. Mazao yao yaliwekea % ya makato kwa ajili ya ujenzi wa majumba na viwanja vya michezo. Hata ile CDA( yale majengo) yalijengwa na michango na makato ya wakulima wa pamba, alizeti, korosho, pareto Kahawa na.k.
Majengo yote ya CCM yawe ya Vijana, Wazee, wanawake na Jumuiya zingine kama vile OTTU zilichengwa kwa kukamuana.
Tatizo ni kwamba, kipengele hiki hakikuwa sehemu ya Hadidu za Rejea pale mwaka 1992 na hii ilifanyika kwa hila kudhani kwamba waTZ hawataweza fahamu na kukumbuka.
Ni swala la Muda na kil;a kitu kitakuwa Okay hata miaka 50 ijayo.
Majengo yote yarudi SERIKALINI vinginevyo CCM itakuja kupata aibu kama waliopata rafiki zako UNIP, KANU na wengi unaowajua.
 
mkuu, kwasasa hatuwezi kuzipata hizo mali, vumilia kidogo watoke madarakani watakuwa naka KANU.
 
Utahangaika sana na believe me your work or plan even your idea is irrelevant!

CCM nao watatudai vya kwao; watadaienzi za zidumu fikra za mwenyekiti wa chama, watadai wakati zinachukuliwa tulikuwa wapi, watadai ujamaa na kujitegemea! watadai kila kitu......

Mwisho utadai kwa nini ulizaliwa na baba mweusi, na utadai kwa nini rais wa kwanza alikuwa Nyerere! utadai na utadaiwa tu

Kuna kitu kimoja naamini na kimetangazwa ni mali ya woote na yeyote akitakaye nacho ni top kuliko kirumba stadium n.k NACHO NI IKULU!!

IKULU is free for everyone na our goal is to reach there, tukifanikiwa kuiondoa CCM magogoni what is kirumba anyway??

Yaani tukipiga ikulu vingine vitajkiachia vyenyewe!! we should be strategic


Hopo kweli umeboronga, kwani hukumbuki historia ujui kuwa kabla ya Ccm kulikuwepo vyama vya upinzani, Mwalimu alivyoviua kabisa na kuvipiga marufu na chama kushika Hatamu, hata hiyo jui, ccm kujimilikisha viwanja vya halmashauri ni sahihi,? mfano Drive in ccm WALAINZA KAMA mchezo wakaanzisha shina la wakereketwa sugu baadaye kukaanza gulio alafu gulio likafa na kuzungushiwa mabati na kujenga Oil Com, sasa zantel bado vingi tu viwanja vya wazi walivyochuyakua kwa vigezo vya ukereketwa
 
Kirumba na Amri Abeid imetolewa kama sample, tatizo liko kwenye nani wa kuamua ili kufanya hiyo 'cultural revolution'! Juzi tu Kenya walivyofanya mabadioliko ya katiba hakuna aliyefikiri kuwa Mzee Kibaki angeteua maofisa wa juu lakini umma ukakataa kupitia bunge. HIYO NI HATUA MBELE, hapa ni kujaribu kukomesha/kupunguza jeuri ya baadhi ya watendaji lakini safari ni ndefu. Au basi tupatie pa kuanzia (program of action/implementation)


Swala la kuanzia wapi ni complex sana. Lakini ninavyofikiri mimi mabadiliko haya ni vigumu kutokea chini ya utawala wa Chama kilichoko madarakani, kwani uzoefu umeonesha kwamba wao hupendelea kufanya window dressing na sio mabadiliko ya kweli. Wao hulindana kila panapotokea matatizo ya uvunjifu wa sheria. Sheria tunazo tosha za kukabiliana na maovu yote. Tunachokosa ni ile political will ya kwenda a step further kukabiliana na maovu.

Matumaini yangu yako kwenye hali inayojitokeza sasa ya watu kuanza kukataa hali ilivyo nchini. Mbegu hii ikikuwa na kushamiri there lies National Salvation. It is a process which no one can tell or give a time frame. THANKS.
 
Hatuna muda mwingine wa kuamua haya! Muda ni sasa, hatuja chelewa kama tunavyofikiri, tukizidi kupiga danadana ndio tunazidi kujichelewa! Wazo limekuja muda muafaka tuongeze shinikizo kwenye hadidu za rejea ili muswada mpya mambo hayo yaingizwe. Hatuwezi kuendelea kuvumilia zulma kutoka kwa ma ccm na kupenda kwao kuvimbiza matumbo kwa kunyang'anya na kujimilikisha hata visivyo vyao kama chama. Babu yangu na bibi yangu walishiriki kujenga kama umma wa kitanzania na si kama wanachama wa ccm kwa nini ziwe za chama?
 
Kutaifishwa ndio mpango mzima..........hata kama vilikuwa ni vya Tanu then CCM ambayo kilikuwa chama pekee hivyo hakukuwa na tofauti kati ya serikali na chama hivyo basi ni muda muafaka kuvirudisha kwa umma........:rip:CCM hahahahahah twataka urithi wetu kwani tushaona nyie mwafa sasa msije mkatupa tabu katika mirathi........:yield:
 
Back
Top Bottom