ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,051
- 49,736
Mbunge wa Jimbo la Ushetu Emmanuel Cherehani Mkoani Shinyanga amemuangukia Waziri wa Maji Jumaa Aweso akimuomba maji kwani Amesema Wilaya Majimbo yaote ya Mkoa wa Shinyanga yamefikiwa na Mji ya kutoka Ziwa Victoria isipokuwa Jimbo lake.
Akiongea Kwa unyenyekevu, uchungu na masikitiko bwana Cherehani amesema kati ya Kata 15 za Jimbo lake Kata 11 hazina maji hivyo kuwa Changamoto kubwa Kwa Wananchi wake.
Akijibu Maombi hayo Waziri wa Maji Jumaa Aweso amesema tayari Rais Samia amesikia Kilio Cha Wana Ushetu na Serikali Imetoa maelekezo ya kutangazwa tenda haraka ambapo ndani siku 30 mkandarasi atakuwa site kuanza usambazaji wa Maji Kwa Wananchi maji ya uhakika kutoka Ziwa Victoria.
My Take: Kuelekea Uchaguzi tutaona Mengi, wale wote waliopitishwa na Jiwe kama hawakuwa na sifa ndio imekula kwao.
View: https://www.instagram.com/p/C16S-qIrvkt/?igsh=MXJzdXVjOGE5ZGEwbQ==