Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,902
- 945
MBUNGE WA HANANG, ENG. HAYUMA AILILIA SERIKALI, ATHARI ZA MAFURIKO YA HANANG
Mbunge wa Jimbo la Hanang, mkoani Manyara, Eng. Samwel Hayuma ameingukia serikali akiiomba kuwatazama kwa jicho la pili wafanyabiashara ambao wamepoteza mali zao kutokana na mafuriko ya maporomoko ya tope yaliyotokea Desemba 3, 2023.
Amesema licha ya Mafuriko hayo kusabisha vifo, yameleta hasara kubwa kwa baadhi ya wafanyabiashara kwa kuwa baadhi yao wamepoteza mitaji huku wengine wakiwa na mikopo umiza.
Eng. Hayuma amesema ni vyema serikali ikawatambua wafanyabiashara hao ikiwemo wa soko kuu la kateshi linalojumuisha wafanyabiashara wadogo na wakubwa, ambapo licha ya kuwapa mitaji, ikiwezekana zile bima mikopo walizokuwa wamezikata, zitumike kulipa madeni yao.