Mbunge wa Arumeru Mashariki mh. Joshua Nasari ahamasisha wananchi kugomea Mwenge wa Uhuru

Malengo ya awali ya kuwasha mwenge yalikuwa mazuri sana!

"Kuwasha mwenge, na kuuweka Kilimanjaro, umulike ndani na nje ya mipaka yetu, ulete tumaini, pale ambapo hapa matumaini, upendo mahali penye chuki, na heshima ambapo pamejaa dharau!"

Tatizo ni kwamba, wapo nje ya malengo! Kucheza ngoma na kuiambukiza vijijini!

mkuu, mwenge unamulika mipaka kvp au unaletaje amani na matumaini?
Hakukuwa na sababu ya kuwa na mwenge wala hauna tija na haukuwahi kuwa na tija.

Amani, upendo na matumaini vinatokana na watu wenyewe sio kitu kisicho na uhai.
Huko ni sawa na kuabudu sanamu lisiloweza kujifuta vumbi pale linapo chafuka nawe unalitegemea likukinge na shari.

Nasari kama mbunge angetakiwa kutoa hiyo hoja yake bungeni na sio kuanzia kwa wananchi.
Angetakiwa atumie wananchi kama silaha ya mwisho baada ya bunge kukataa hoja yake.
 
Nakumbuka tulikua tunachangia mafuta ya Mwenge, enzi hizo nilikua mdogo sana na nilijiona mkosaji kama ntaikosa Tsh 20. Ila baada ya kuona Kondom zinazokusanya punde baada ya mkesha wa mwengw nikawa na maswali mengi,
1:Kwa nini tunafagia barabara wakati wa Mwenge na si siku zote?
2:Tunapaka chokaa mawe ya pembeni mwa barabara na kuyapanga upya?
3:Twaenda na kuotesha maua ndani ya wiki moja na baadae kuyasahau?.
4:Madarasa mapya hayafunguliwi wala kutumiwa hadi mbio za mwenge hata kama yalimalizika miezi 9 iliyopita?
 
Mbunge wa Arumeru Mashariki kupitia chama cha CHADEMA amehamashisha wananchi wa Jimbo lake kugomea shughuri zote za mwenge wa Uhuru ktk Jimbo lake kwani hauna tija kwa wananchi wa jimbo hilo na hauna maana yoyote.

Na kahamasisha wananchi wake kuendelea na shughuri zao za kila siku.

Hii inahashiria nini kwa nchi?

Hapa najiuliza nashindwa kupaja majibu yenye tija na umuhimu wa shughuri husika.

Mh. Kayanza Peter Pinda yupo katika ziara ya nchi bila shaka nchi nzima katika kukagua, kuhimiza na kufungua miradi mbalimbali ya kimaendeleo ona imefika wakati hadi mama Tunu Pinda anauliza swali kwa mmewe anayetembea nae kote ii hari kwamba kama hawaonani.

Nauliza mwenge unauzunguka na Pinda anavyozunguka kuna tofauti gani????

Mwenge wa Uhuru hutumia zaidi ya 800million kwa Mwaka kuizunguka nchi (Kutoka kwenye hazina kuacha nyingine wanazochangishwa wadau na wafanyabiashara wa sehemu husika)
 
Huyu mbunge ana matatizo ya ubongo. Unahamasishaje watu wagomee mwenge wa uhuru ambao ndiyo ishara ya umoja na amani ya nchi yetu? Kwahiyo anapingana hata na Baba wa Taifa ambaye alisema tunauwasha mwenge na kuuweka kileleni ili umulike mpaka kusikomulikika?
 
Huyu mbunge ana matatizo ya ubongo. Unahamasishaje watu wagomee mwenge wa uhuru ambao ndiyo ishara ya umoja na amani ya nchi yetu? Kwahiyo anapingana hata na Baba wa Taifa ambaye alisema tunauwasha mwenge na kuuweka kileleni ili umulike mpaka kusikomulikika?

kwani huyo unayemuita Baba wa Taifa ndio dictionary au msaafu kwamba hakukosea.
mantiki ni kuwa mwenge haujawahi kuwa na tija wala hautawahi kuwa na tija. Ni moja ya ibada za kishetani na waliofungwa akili ni ngumu kung'amua. Hatuhitaji kukimbiza kijinga cha moto ili kuhamasisha maendeleo.
 
Hivi wanao jiita waombaji muko wapi? Majinamizi yamewakaba watawala akili zao ni kama ziko kuzimu, hii isue ya mwenge ingekuwa haipo kwa kuwa haina mshiko. Tatizo letu Tanzania watawala mawazo na fikra zao zimetekwa hakuna kiongozi anaye weza ona kuwa mwenge ni upuuzi. Sana sana mi nashauri waombaji au wapendwa kuombea taifa viongozi wetu wako kama vile msikule!
 
Huyu mbunge ana matatizo ya ubongo. Unahamasishaje watu wagomee mwenge wa uhuru ambao ndiyo ishara ya umoja na amani ya nchi yetu? Kwahiyo anapingana hata na Baba wa Taifa ambaye alisema tunauwasha mwenge na kuuweka kileleni ili umulike mpaka kusikomulikika?

ubongo wa mwenzio unamatatizo!!! ubongo wako umesalimikaje ulipouona wa mwenzio una matatizo.
 
Kwa kila jambo kuna majira yake na wakati kila kusudi chini ya mbingu. Kuna enzi ya Mwenge na wakati ambapo mwenge hauhitajiki. Kwa majira kama haya ambapo wananchi wameelimika mwenge hauna tija tena kwa sababu hizo zilikuwa fikra za mwenyekiti wa ccm ambazo hazidumu tena. So what is the need of Uhuru Torch???? It is wasted of our resources and energy.
 
Mwenge umulike wapi tena wakati wanaomulikwa ndio wenye chama cha Mapinduzi ambacho hata wenyewe wanapinga mambo mengi ambayo mwasisi wake aliyaanzisha?? Liko wapi azimio zuri la Arusha, liko wapi azimio la Musoma, liko wapi azimio la Moshi?? wewe uko my friend?? Iko wapi siasa ya ujamaa na kujitegemea??? Umesahau tulivyoimba kwamba "Ujamaa na kujitemea ndio njia pekee ya kujenga jamii ya haki na usawa"" Viko wapiiiiii??? Hon. Nasari afadhali watu wakalime kuliko kukaa barabarani kungojea kibatari. Niko na wewe kabisa!!!
 
Ivi kama nchi iko gizani,si Tanesco wafunge mitaa yote Tanzania badala ya kuendelea na ufreemason wa kukimbiza mwenge?au si taifa liagize mishumaa iwashwe kila tar9 ya uhuru kama kuna adui tumuone siku iyo?ivi ni nani anamlipa msimamizi wa mshumaa uyo mwaka mzima bila hata kufanya kazi ila kwa kuzurura na mwenge?kijijini kwetu apa tangu mwaka wa uhuru mpaka leo,mwenge unakuja ila hakuna umeme,hakuna maji,hakuna dispensar wala kitu cha usalama. Watu tunatoza gharama za kuzurura kwa mwenge wao. Tumechoka na ujuha huu wa taifa letu!
 
Back
Top Bottom