Mbunge mwenye uchungu wa kweli

Swali zuri mno, kwamba imedhihirika wote bilankujali chama ni watu wasioweka mbele maslahi ya Taifa? Na hapa si wale wa CCM tu hapana, na vyama vyote! Tufanyeje tulio wanyonge? wapi kimbilio letu? Ni swali gumu mno.

Wewe mawazo yako yepi, tufute bunge? Katiba mpya iseme wabunge walipwe kima cha walimu? Dhana kubwa hapa ni watu kuwajibika ili taifa hili liendelee. Uadilifu na uwajibikaji wa mtu ni muhimu sana kuliko chochote. Kama bunge likiwa la waadilifu, litasimamia maslahi ya nchi na kuwawajibisha wafujaji.
My take, uadilifu wa wabunge hautapimwa kwa udogo wa mishahara, bali kuisimamia serikali na kuona inawajibika ipasavyo kwa wananchi.
 
Mkulu hii thrd yako haijakaa vizuri!! Kama wewe ni mtumishi ungeandika-: Mtumishi Bomba ni. 1. Anayegawa mshahara wake wote kwa maskini kwa huruma yake. 2. Anafanya overtime bure. E.t.c Kama wewe ni mfanya biashara, unagawa hela bure eeeeH! Angalia!!! you try to be introspective, Objective!!!!
 
Naomba nimjue Mbunge mwenye uchungu wa kweli wa nchi yetu:


  • Ambaye amekataa ule mkopo wa mamilioni (up to 200 mil) payable in 5 years?
  • Ambaye amekaa kuchukua mkopo wa gari wa milioni 90? Lema? Anybody knows?
  • Ambaye amekataa mshahara mkubwa wanaopata, au kutoa japo robo ya mshahara huo kuelekeza sehemu fulani jimboni mwake japo kwa mwaka mmoja?

Kama hakuna, basi mujue kwamba wote hawa ni sawa tu, tunawapepea tu wao wanakula kiulaini mnoo. Hakuna cha CDM,CCM,CUF,NCCR etc wote hawa ni walaji tu. Sisi huku tunabaki na ushabiki na kutoleana matusi na chuki, kashfa nk. Wenzetu wala. Tumeliwa kekundu.
Fikiri kwa makini utaona.
Kwani kukataa ndio kuwa na uchungu? Kwa taarifa yako hizo hela zinawasaidia wapiga kura wa wabunge husika kwa namna tofauti. Nimesoma mahali fulani kuwa Lema hutoa kiasi fulani cha hela (sijajua ni Tsh ngapi) kuwasaidia watu wa jimboni kwake. Asingechukua hao wapiga kura wake wangezipata hata hizo kiduchu? Na hizo mil 200 kwani anaenda kuziatamia? Si ajabu mmojawapo wa ndugu zako kapata ajira kupitia mkopo huo kwa mbunge. Kajipange tena
 
Wako wabunge waliotoa sehemu ya fedha zao kwa ajili ya majimbo mfano mnyika. Lakini hilo siyo kazi ya msingi ya Mbunge - Kugawa hela. Anatakiwa aibue mfumo endelevu wa kuendeleza wananchi wake.
 
Niliwasikia Mnyika kasema robo ya mshahara wake utachangia katika moja ya miradi ya maendeleo ya ubungo.
Lakini sio issue kulipwa kingi as long you are doing what people are expecting awe CCM,CDM,CUF,NCCR NA WENGINEO.
Na nidhana potufu kusema eti kukubali mshahara huo ni uadilifu au uzalendo mbona mimi nalipwa kikubwa kwa post yangu na nina wajua jamaa wenye post na qualification kama zangu makampuni mengine wanaminywa je unataka mimi nikatae haya masalalilo.
Kuna jamaa kibao weanalipwa bags of money mjini kwa kazi yao, so chapa kazi ulipwe ujira wako.

Hii hoja kimsingi imepinda au imeulizwa vibaya. Hapa hoja kuu ni jukumu la wabunge ni nini? Ili tujue nani anafanya vizuri na nani ana lala. Na si suala la nani anasusa mshahara wake. Hilo halisaidii sana, japokuwa ni vizuri ufahamu kwamba Chadema wanapinga mishahara ya wabunge kuwa mikubwa sana tofauti na wafanya kazi wengine.
Hapa kwetu Ubungo sehemu kubwa ya Mshahara wa Mnyika inatumika katika maeneo mbali kuazia vituo vya yatima, shule na uimarishaji wa Chama kwa ujumla.

Lakini hii si jambo kubwa sana ambalo sisi tutalisimamia huko mbeleni kuwa ndo mafanikio yetu hapa UBUGNGO kama Chama. Mbunge amefanya mengi sana. Ameshaitisha Kongamano la kutafuta utatuzi wa kero ya Maji. Ameshakaa vikao vingi ya kuboresha ulinzi Kimara, mbezi nk, ameshakuwa msemaji wa kero za wananchi Dsm na Bungeni ikiwepo kudai utaratibu wa sheria kufuatwa katika kuvunja nyumba za watu- si kukurupuka tu nk.
 
Naomba nimjue Mbunge mwenye uchungu wa kweli wa nchi yetu:

  • Ambaye amekataa ule mkopo wa mamilioni (up to 200 mil) payable in 5 years?
  • Ambaye amekaa kuchukua mkopo wa gari wa milioni 90? Lema? Anybody knows?
  • Ambaye amekataa mshahara mkubwa wanaopata, au kutoa japo robo ya mshahara huo kuelekeza sehemu fulani jimboni mwake japo kwa mwaka mmoja?
Kama hakuna, basi mujue kwamba wote hawa ni sawa tu, tunawapepea tu wao wanakula kiulaini mnoo. Hakuna cha CDM,CCM,CUF,NCCR etc wote hawa ni walaji tu. Sisi huku tunabaki na ushabiki na kutoleana matusi na chuki, kashfa nk. Wenzetu wala. Tumeliwa kekundu.
Fikiri kwa makini utaona.

umeshasema mkopo kwa hiyo hiyo hela ni yake atarudisha wewe ukipewa mkopo urudishe ndani ya miaka mitano utakataa? ingekua ni bure hapo sawa, na swala la mshahara si wameukuta utakataa ili ufe njaa
 
Wakuu zangu msitake kulinganisha mishahara ya Wabunge na ajira zenu kwa sababu wewe ambaye ni mwajiri humpangii mbunge mshahara kama mashirika yanavyoajiri wafanyakazi wake..

Shangingi la millioni tisini sii solution ya barabara mbovu wala kipimo bora kuwekea sababu za kununua magari hayo...kisha sii wabunge wote wanaishi vijijini..

Specs za magari hayo zinaonyesha wazi kuwa ni ya kifahari na hayakutengenezwa kwa ajili ya baranara mbaya au milima na vitongoji vingi..Kwa kila umbali ndivyo gharama za matumizi yake zinazidi acha mbali maintanance...

Na jingine ni kwamba Wabunge hawatakiwi kutumia mishahara yao ktk maendeleo ya majimbo yao..
Hizi fedha utazi account vipi? ni income kutoka wapi na zinaingia vipi kimahesabu..

Jamani kuendelea na mifumo duni ndiko kuna.upeleka pabaya na ndio takrima yenyewe.Ili mbunge ajiweke ktk nafasi nzuri uchaguzi ujao kwa fedha yenu wenyewe...

Ikiwa mishahara yao wanasaza kiasi kikubwa cha fedha hadi waaiingize ktk maendeleo kwa nini wasikatwe kabisa kabla na fungu hilo likawa allocated ktk budget ya jimbo?

Je, hii yote sio ishara tosha kuonyesha kwamba tunawalipa wabunge mishahara mikubwa ambayo fedha hubakia na wanatafuta pa kuzitumia kujenga uaarufu wao..

Kama mbunge ana biashara zake na katoa donation ktk kuchangia kitu hilo sawa lakini sii kukubali ujiinga unaoendela kiasi kwamba Watanzania wote hawajui viongozi wao wanalipwa kiasi gani na ni asilimia ngapi..
...
 
Hilo kweli FUSO linazoazoa tuuu wala halichambui,, mtajuaje kwamba nalo limo barabarani ati?

You can give without love but you can not love without giving . Lema of arusha he just donated half of his car loan for women loan and youth so until this moment lema seems to love the country most
 
hakuna hata mmoja ila wapo wanataka umaarufu na ili kuupata lazima ujifananishe na wananchi,hivi yupo aliye wahi kusema wabunge ni mabwana ambao wanatafuna nchi yetu bila aibu,kwanini wabunge wasilipwe kwa mfumo wa kawaida wa serikali? kama yupo mbunge mzalwndo angesimamia hayo
 
hakuna hata mmoja ila wapo wanataka umaarufu na ili kuupata lazima ujifananishe na wananchi,hivi yupo aliye wahi kusema wabunge ni mabwana ambao wanatafuna nchi yetu bila aibu,kwanini wabunge wasilipwe kwa mfumo wa kawaida wa serikali? kama yupo mbunge mzalwndo angesimamia hayo
In colours, ndiyo point halisi. Hakuna mbunge mzalendo. PERIOD!
 
mbunge mshahara wake ni 3 mil a month. itapanda kutegemea vitu vifuatavyo mafuta, mshahara wa dereva na katibu wake, matengenezo ya gari, kids education if under 18, posho za vikao vya bunge, depending on these mbunge anapata btw 5 - 12 milion. kuna wabunge wengine wako kwenye kamati posho inaongezeka.
 
Kwa nchi kaa Tz, the system of check & balance is non-existent na hivo kimsingi sioni faida ya uwepo wa bunge na wabunge..tumeshazungumza hili mara nyingi sana..the bunge is a wastefukl white elephant. Gharama za bunge na wabunge zingepelekwa kuimarisha shughuli za maendeleo kwene wilayat mambo yangesogea kidogo.
 
Naomba nimjue Mbunge mwenye uchungu wa kweli wa nchi yetu:

  • Ambaye amekataa ule mkopo wa mamilioni (up to 200 mil) payable in 5 years?
  • Ambaye amekaa kuchukua mkopo wa gari wa milioni 90? Lema? Anybody knows?
  • Ambaye amekataa mshahara mkubwa wanaopata, au kutoa japo robo ya mshahara huo kuelekeza sehemu fulani jimboni mwake japo kwa mwaka mmoja?
Kama hakuna, basi mujue kwamba wote hawa ni sawa tu, tunawapepea tu wao wanakula kiulaini mnoo. Hakuna cha CDM,CCM,CUF,NCCR etc wote hawa ni walaji tu. Sisi huku tunabaki na ushabiki na kutoleana matusi na chuki, kashfa nk. Wenzetu wala. Tumeliwa kekundu.
Fikiri kwa makini utaona.

Mbona una njaa ivoo, we ulfkri kua kuingia kwa kiongoz madarakan ni ulaj kwako? Vp uligharimikia campen af umetupwa? Angalia ukomboz wa nchi na sio ukomboz wa mtu binafsi! We vip?
 
Mbona una njaa ivoo, we ulfkri kua kuingia kwa kiongoz madarakan ni ulaj kwako? Vp uligharimikia campen af umetupwa? Angalia ukomboz wa nchi na sio ukomboz wa mtu binafsi! We vip?
Kwa jazba unazoonesha, tayari umeliwa kekundu!!
 
Back
Top Bottom