Mbunge Geofrrey Mwambe Azindua Zahanati Matawale

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,900
944

MBUNGE GEOFFREY MWAMBE AZINDUA ZAHANATI MATAWALE

• Imegharimu Milioni 200
• Wananchi wampongeza

Mbunge wa Jimbo la Masasi Mjini Mheshimiwa Geoffrey Mwambe, leo amezindua zahanati mpya katika kijiji cha Matawale kata ya Matawale.

Ujenzi wa zahanati hiyo umegharimu TZS. 200,000,000/= (Milioni Mia Mbili) kutoka Serikali Kuu.

Kata ya Matawale yenye vijiji saba haikuwa na zahanati na hivyo kuwalazimu wananchi kutembea zaidi ya kilomita thelathini kufuata huduma za matibabu katika kituo cha afya Mbonde au hospital ya Mkomaindo.

Akizungumza katika hafla hiyo Mbunge Geoffrey Mwambe alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassani kwa namna anavyomuunga mkono na kumpatia fedha za kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Jimbo la Masasi Mjini ikiwemo ujenzi wa zahanati hiyo ya Matawale.

Mheshimiwa Mbunge Geoffrey Mwambe aliwaomba Wana Matawale kuendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassani, Diwani Mnela pamoja na yeye ili nia yao ya kuwaletea maendeleo iweze kufikiwa kwa uharaka zaidi.

Mheshimiwa Geoffrey Mwambe(MB) aliwaeleza wananchi waliohudhuria hafla hiyo kuwa serikali imedhamiria kuhakikisha suala la elimu linapewa kipaumbele ndani ya Mji wa Masasi na yeye kwa nafasi yake atahakikisha kata ya Matawale inapata shule ya sekondari ya kata ili kupunguza adha ya watoto kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya shule kwenye kata za Napupa na Mwenge Mtapika.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Mbunge Geoffrey Mwambe aliongozana na viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Masasi wakiongozwa na
Katibu wa Siasa na Uenezi Ndg Twahili Mayola, Kaimu Katibu wa CCM wilaya Ndg Pius Amoli, pamoja na Mwenyekiti wa umoja wa vijana wilaya Ndg Seif Abdul
Namtusi.

Akizungumza katika hafla hyo ya uzinduzi wa zahanati kwa nyakati tofauti tofauti viongozi hao wa CCM wilaya walimpongeza Mheshimiwa Mbunge Geoffrey Mwambe kwa namna anavyotekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025 ndani ya Jimbo la Masasi Mjini na kuwaomba waendelee kumuunga mkono Mheshimiwa Mbunge kwani anaonesha dhamira ya dhati ya kuijenga Masasi Mjini na Chama Cha Mapinduzi kwa ujumla.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri Mheshimiwa Hashimu Namtumba (Sugu) alimpongeza Mheshimiwa Geoffrey Mwambe (MB) kwa namna anavyoshirikiana naye vizuri kuhakikisha kero na changamoto za Wana Masasi Mjini zinapatiwa ufumbuzi.

Wakizungumza kwenye hafla hiyo Kaimu Mkurugenzi Andrew Kalinga na Mganga Mkuu wa Halmashauri Salumu Gembe, wamempongeza Mheshimiwa Geoffrey Mwambe(MB) kwa juhudi anazozifabya kuhakikisha wananchi wanafikiwa na huduma za kijamii zikiwamo huduma za afya. Wamemuahidi kusimamia utendaji wenye tija kwa watumishi wa zahanati hiyo na maeneo mengine ya halmashauri.

#MASASI MPYA

Imetolewa na OFISI YA MBUNGE JIMBO LA MASASI MJINI
Facebook: Ofisi ya mbunge jimbo la masasi mjini
Instagram: Ofisi ya mbunge jimbo la masasi mjini
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-11-26 at 01.37.34.jpeg
    WhatsApp Image 2023-11-26 at 01.37.34.jpeg
    121.9 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2023-11-26 at 01.37.34(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-11-26 at 01.37.34(1).jpeg
    116.8 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2023-11-26 at 01.37.35.jpeg
    WhatsApp Image 2023-11-26 at 01.37.35.jpeg
    200.6 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2023-11-26 at 01.37.35(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-11-26 at 01.37.35(1).jpeg
    190.4 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2023-11-26 at 01.37.35(2).jpeg
    WhatsApp Image 2023-11-26 at 01.37.35(2).jpeg
    101.7 KB · Views: 3
Wananchi wasio na akili wanampongeza na kumshukuru mbunge ambae anajambia tu vitu vya bunge hovyo kwa kuzindua zahanati.

Badala ya kujipongeza wao wenyewe kwakuwa zahanati imejengwa kwa majasho yao (kodi au mikopo ambayo watailipa wao na vizazi vyao) wanampongeza mchumia tumbo mbwa mwitu alivika ngozi ya mwanakondoo.

Siku hii nchi watu wakapata uelewa hata kidogo mambo kama haya hayawezi kusikika.
 
Wananchi wasio na akili wanampongeza na kumshukuru mbunge ambae anajambia tu vitu vya bunge hovyo kwa kuzindua zahanati.

Badala ya kujipongeza wao wenyewe kwakuwa zahanati imejengwa kwa majasho yao (kodi au mikopo ambayo watailipa wao na vizazi vyao) wanampongeza mchumia tumbo mbwa mwitu alivika ngozi ya mwanakondoo.

Siku hii nchi watu wakapata uelewa hata kidogo mambo kama haya hayawezi kusikika.
Mzazi akikulipia hela ya Ada unamshukuru, licha ya kuwa ni wajibu wake,
Ni utamaduni wetu watanzania
 
Mzazi akikulipia hela ya Ada unamshukuru, licha ya kuwa ni wajibu wake,
Ni utamaduni wetu watanzania
Nikijilipia ada mwenyewe halafu siku ya graduation mzazi aje nianze kumshukuru kwa kunisomesha huo ni wendawazimu.

Huwezi kumshukuru mbunge eti kwa kuja kuzindua zahanati iliyojengwa kwa pesa ya kodi yako wewe mwananchi na mikopo ambayo utailipa wewe na vizazi vyako.

Huo ni uhayawani.

GET THE DIFFERENCE.
 
Nikijilipia ada mwenyewe halafu siku ya graduation mzazi aje nianze kumshukuru kwa kunisomesha huo ni wendawazimu.

Huwezi kumshukuru mbunge eti kwa kuja kuzindua zahanati iliyojengwa kwa pesa ya kodi yako wewe mwananchi na mikopo ambayo utailipa wewe na vizazi vyako.

Huo ni uhayawani.

GET THE DIFFERENCE.
Nikiri, tuna malezi tofauti,
Endelea kuamin msimamo wako
 
Malezi tofauti yapo bro. Inawezekana kweli wewe shule ulienda kucheza tu ndio maana mambo mepesi kama haya yanakupa ugumu kuelewa.

Until then.
Shida yenu wapinzani mnajionaga mna akiili 😂😂😂 nyumbani tulishinda shambani na bustanin, kisha tukala ugali/ maboga tuliyolima wenyewe, tukavuna wenyewe na kupika wenyewe, ila hatukuacha kusema Ahsante kwa mama na Baba kwa chakula,

Ni malezi ya Kiafrica na malezi bora, ni malezi ya kumtia moyo kiongozi azidi kuwapambania,

Kama hamtamsifia akifanya vizuri, bas msimseme akifanya vibaya, that is rule of thumb
 
Back
Top Bottom