Mbunge Asumpta Mshana na Mary Mwanjelwa hawajui msimamo wa serikali ya Israel

Kikulacho

Member
Mar 29, 2012
33
12
Leo katika kipinsi cha maswali na majibu Mbunge wa Nkenge Asumpta Mshama na Mery Mwanjelwa (CCM), wameitaka Serikali itoe Maelezo kwa nini haijafungua Ubalozi nchini Israel kwani kutofanya hivyo ni kuikosea biblia na Tanzania itapata laana.

Kutokana na hali hiyo Wabunge hawa hawajajua msimamo wa Serikali ya Tanzania kwani inatambua kuwa Palestina ni Taifa huru na ndiyo maana nchi yetu katu haitafungua ubalozi katika nchi ya Israel na Lebanon kutokana na uonevu unaofanywa kwa chuki za kidini, hivyo hawa wabunge kuna kila chembe ya dalili ya kutumwa na makuadi wa Israel kwa kuwasemea kupitia Bunge.

Ni vema wawe wanasoma kwanza wabunge wetu kabla ya kukupuka na hoja butu.
 
Usiseme uongo kuhusu Lebanon, tuna Consulate pale na Mzee Zakhem ni Desk Officer.

Taarifa: Lebanon isiingizwe kwenye maelezo yako kama pro-Israel. Jua pia PLO iliundwa na kuwa na makao yake makuu ya kwanza kijijini Chebaa, kusini mwa Lebanon. Lebanon ina kundi la Hizbullah ambalo linakinzana na Israel na inavitunza vikundi vya kipalestina vinvokinzana na Israel nchini mwao. Mgogoro wa Israel na Palestina ni wa kijiographia (mipaka) na sio wa kidini. Nchi zote mbili zina wakristu na waislamu!!

Msingi wa wabunge hawa kudai ubalozi unatoka na Biblia kuwa "Nchi ya Kanaan" ambayo sehemu yake ni Israel ya leo, ni taifa teule. Si kwa sababu wanataka kuonesha kuwa wanaipinga Palestina. Kwa taarifa tu, mataifa mengi ya magharibi yana balozi za Palestina hali kadhalika za Israel. Kwa sababu mamlaka ya Palestina kwa Ghaza na West Bank yanajulikana kimataifa!!
 
leo katika kipinsi cha maswali na majibu mbunge wa nkenge asumpta mshama na mery mwanjelwa (ccm), wameitaka serikali itoe maelezo kwa nini haijafungua ubalozi nchini israel kwani kutofanya hivyo ni kuikosea biblia na tanzania itapata laana.

Kutokana na hali hiyo wabunge hawa hawajajua msimamo wa serikali ya tanzania kwani inatambua kuwa palestina ni taifa huru na ndiyo maana nchi yetu katu haitafungua ubalozi katika nchi ya israel na lebanon kutokana na uonevu unaofanywa kwa chuki za kidini, hivyo hawa wabunge kuna kila chembe ya dalili ya kutumwa na makuadi wa israel kwa kuwasemea kupitia bunge.

Ni vema wawe wanasoma kwanza wabunge wetu kabla ya kukupuka na hoja butu.
enzi za juchagua marafiki kwa maslahi ya kisiasa ulishapita, kwa nini tunatangaza diplomasia ya kiuchumi kwa maneno tuu? Yapo mengi tunaweza faidika kiuchumi kutoka israel hasa kupitia kilimo na utalii..
 
Hao ndio wabunge wa CCM! Kwa umri naamini walisoma kabla shule za kata hazijaanza, sasa tatizo ni nini? Wamepoteza kumbukumbu? Membe una kazi, aanzisha evening class Dodoma ili tuondokane na hii aibu.
 
Nyerere alifunga UBALOZI wa Israel hapa Tanzania kuwafurahisha Waislamu ambao leo hii wanamuona eti alikuwa adui wao mkubwa.

Matokeo ya kuwafukuza wa Israel Bugando Hospital Haikumalizika, Nkurumah Hall haikulimazika maana ilitakiwe iwe flyer ove bridge, mradi wa kupeleka maji kutoka Ziwa Victoria to Dodoma hakufanyika, majuzi tu ndiyo EL ali struggle na kupeleka maji Kahama. Just Kahama hata Singida hayajafika.

Ila hilo la kupata laana kutokana na kutofungua ubalozi wa Israel is a RELIGIOUS FANATISIM.

BTW, nimesikia Wa israel wameanzisha mradi mkubwa wa kilimo cha umwagiliaji maji Zanzibar. Labda ndiyo wanaanza kurudi taratibu.
 
Hao ndio wabunge wa CCM! Kwa umri naamini walisoma kabla shule za kata hazijaanza, sasa tatizo ni nini? Wamepoteza kumbukumbu? Membe una kazi, aanzisha evening class Dodoma ili tuondokane na hii aibu.
Wote wawili nasikia wanajiita walokole! Kama sikosei tumeisha rudisha mahusiano ya kibalozi. Balozi wa Israel Kenya ndiye anawakilisha nchi yake hapa Tanzania.
 
Nyerere alifunga UBALOZI wa Israel hapa Tanzania kuwafurahisha Waislamu ambao leo hii wanamuona eti alikuwa adui wao mkubwa.

Matokeo ya kuwafukuza wa Israel Bugando Hospital Haikumalizika, Nkurumah Hall haikulimazika maana ilitakiwe iwe flyer ove bridge, mradi wa kupeleka maji kutoka Ziwa Victoria to Dodoma hakufanyika, majuzi tu ndiyo EL ali struggle na kupeleka maji Kahama. Just Kahama hata Singida hayajafika.

Ila hilo la kupata laana kutokana na kutofungua ubalozi wa Israel is a RELIGIOUS FANATISIM.

BTW, nimesikia Wa israel wameanzisha mradi mkubwa wa kilimo cha umwagiliaji maji Zanzibar. Labda ndiyo wanaanza kurudi taratibu.

Pia wapo Dodoma, wana kama eka laki moja hivi chini ya Kilimo kwanza na Bwana Dustan Mrutu. Kama utakumbuka rais alitembelea hilo shamba mwezi uliopita, wanalima mboga mboga na wanasema in 3-4 years time Tanzania (maybe kupita kwao) itakuwa ina export kwa E/Africa & bayond.

Ila swali la msingi hapa nadhani na umbumbumbu wa legislatures wetu. Inakuwaje mbunge asijue issue/sera ya Tanzania Middle East?
 
tuna uhusiano na Israel ila hatuna ubalozi huko wala wao hawana ubalozi hapa. Balozi wa Israel Kenya ndio anasimamia maslahi ya Israel hapa. Mambo kuwa nchi itapata laana si sahihi na mimi binafsi sipendi siasa za vitisho. Kumbuka anayetoa laana humrudia yeye, sasa hawa kwa kutishia watu sidhani kama wapo sahihi.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Wote wawili nasikia wanajiita walokole! Kama sikosei tumeisha rudisha mahusiano ya kibalozi. Balozi wa Israel Kenya ndiye anawakilisha nchi yake hapa Tanzania.

Kwa muda Diplomatic issues za Israel zimekuwa zikifanyika Nairobi. Balozi wa Israel Kenya anawahudumia nchi za E/Africa pamoja na Malawi.

Hawa walokole wameshindwa kutofauita bunge na imani zao? Na huyu Mary Mwanjelwa sio ndio tuliambiwa aliiba taulo hotelini huko Arusha? Ulokole wake unaanzia wapi na unaashia wapi?
 
Usiseme uongo kuhusu Lebanon, tuna Consulate pale na Mzee Zakhem ni Desk Officer.

Taarifa: Lebanon isiingizwe kwenye maelezo yako kama pro-Israel. Jua pia PLO iliundwa na kuwa na makao yake makuu ya kwanza kijijini Chebaa, kusini mwa Lebanon. Lebanon ina kundi la Hizbullah ambalo linakinzana na Israel na inavitunza vikundi vya kipalestina vinvokinzana na Israel nchini mwao. Mgogoro wa Israel na Palestina ni wa kijiographia (mipaka) na sio wa kidini. Nchi zote mbili zina wakristu na waislamu!!

Msingi wa wabunge hawa kudai ubalozi unatoka na Biblia kuwa "Nchi ya Kanaan" ambayo sehemu yake ni Israel ya leo, ni taifa teule. Si kwa sababu wanataka kuonesha kuwa wanaipinga Palestina. Kwa taarifa tu, mataifa mengi ya magharibi yana balozi za Palestina hali kadhalika za Israel. Kwa sababu mamlaka ya Palestina kwa Ghaza na West Bank yanajulikana kimataifa!!

Inaelekea NewOrder na Kikulacho ni wajuzi wa siasa za kimataifa embu mnijuze sababu hasa za kina za sie kutokuwa na mahusiano na Israel maana wengine JF tunaichukulia kama vyuo vingine tu vinavyotoa elimu mbalimbali japokuwa hakuna cheti kinachotolewa zaidi ya kupanua uelewa wetu na ukichanganya na vyeti vyetu vya kuungaunga vya QT mpaka juu tunakuwa tupo fit.
 
Last edited by a moderator:
Kwa muda Diplomatic issues za Israel zimekuwa zikifanyika Nairobi. Balozi wa Israel Kenya anawahudumia nchi za E/Africa pamoja na Malawi.

Hawa walokole wameshindwa kutofauita bunge na imani zao? Na huyu Mary Mwanjelwa sio ndio tuliambiwa aliiba taulo hotelini huko Arusha? Ulokole wake unaanzia wapi na unaashia wapi?
Hata Mushama ni mtata sana!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Usiseme uongo kuhusu Lebanon, tuna Consulate pale na Mzee Zakhem ni Desk Officer.

Taarifa: Lebanon isiingizwe kwenye maelezo yako kama pro-Israel. Jua pia PLO iliundwa na kuwa na makao yake makuu ya kwanza kijijini Chebaa, kusini mwa Lebanon. Lebanon ina kundi la Hizbullah ambalo linakinzana na Israel na inavitunza vikundi vya kipalestina vinvokinzana na Israel nchini mwao. Mgogoro wa Israel na Palestina ni wa kijiographia (mipaka) na sio wa kidini. Nchi zote mbili zina wakristu na waislamu!!

Msingi wa wabunge hawa kudai ubalozi unatoka na Biblia kuwa "Nchi ya Kanaan" ambayo sehemu yake ni Israel ya leo, ni taifa teule. Si kwa sababu wanataka kuonesha kuwa wanaipinga Palestina. Kwa taarifa tu, mataifa mengi ya magharibi yana balozi za Palestina hali kadhalika za Israel. Kwa sababu mamlaka ya Palestina kwa Ghaza na West Bank yanajulikana kimataifa!!

Mkuu asante kwa elimu uliyonipa leo mimi nilikuwa sijui
 
Hawa wabunge wameuliza jambo la msingi sana ambalo serikali yoyote makini ilipaswa kuwa imelifanya juzi na zio jana. Maandiko matakatifu katika biblia yako wazi kuhusu kubarikiwa wale wanaibariki Israel kama taifa teule la Mungu. Na anayechaguaa ukilaani Israeli anachagua laana badala ya baraka. KWA HIYO< TANZANIA KUTOKUWA NA UHUSIANO WA KIBALOZI KAMA ILIVYOKUWA HUKO NYUMA AUTOMATICALLY IMECHAGUA LAANA. Jambo lolote laweza kutanguka lakini chochote kilichotajwa kwenye biblia lazima kitatimia tu.

Chukua mfano wa Marekani anabarikiwa kwa sababu ya kuwa na uhusiano mzuri na Israel na kuitetea Israel. Au tuangalia jirani zetu Kenya moja ya chanzo cha mambo yao kwenda vizuri ni kutokana na wao kuwa na uhusiano mzuri na Israel. Hebu angalia Tanzania pamoja na kuwa na rasilimali nyingi kuliko Kenya kwa mbali, Tanzania bado iko hoi sana. Wenzetu mpaka wamegundua mafuta sisi bado tupo tunapiga mark time. Kumbuka hili ni suala la kiroho zaidi ambalo taathira zake kwenye uchumi na maisha jumla ya kimwili ni kubwa kuliko unavyoweza kufikiri.

MIMI NASEMA UBALOZI WA ISRAEL NCHINI TANZANIA NA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI ISRAEL ULITAKIWA KUWA UMEFUNGULIWA JUZI NA SIO JANA. Tanzania una nafasi ya kuchagua laana au BARAKA.
 
Zanzibar lakini ina mahusiano mazuri sana tena sana na Israel, hivi nikiandika katika Hotel ya Aga Khan mjini Zanzibar wapo waandishi ya habari na Mwanadiplomasia mkubwa wa Israel
 
Lakini ni kweli,asiyeheshimu israel atalaaniwa na hii ni kutokana na biblia.Labda waislam watuambie quorani inasema nini kuhusu israel.
 
Lakini ni kweli,asiyeheshimu israel atalaaniwa na hii ni kutokana na biblia.Labda waislam watuambie quorani inasema nini kuhusu israel.

"Hakuna aliye adui mkubwa wa waaminio (waislamu) kama wayahudi....."
 
Lakini ni kweli,asiyeheshimu israel atalaaniwa na hii ni kutokana na biblia.Labda waislam watuambie quorani inasema nini kuhusu israel.
Huu ndio udini wenyewe tunaouongea sasa Waislam nao wakisema kuhusu Saudi Arabia, Mecca na Medina utawajibu nini? jamani ioneeni huruma Tanzania, tumeishi bila ya huo ubalozi na Israel sasa sioni kwanini tushindwe sasa hizi chokochoko za dini zitalipasua taifa hili! Tuwe na staha uisomavyo Biblia wewe usitake ieleweke hivyohivyo na kila mtu! Give us a brake nyie Walokole
 
Asumpta Mshama mbunge wangu ila ni aibu............TISS huyo.......maana huku kwetu ni wachache wanaojuan kazi yake . mara ruanbiwe alikuwa mpishi wa raisi...mara Air hostess.......mara nini yaani vurugu tupu.
 
Kuwa na mahusiano mazuri na Israel si lazima tufungue ubalozi wao kwetu na wetu kwao. Kimsingi tayari tuna mahusiano mazuri na Israel kielimu ambapo tuna wanafunzi wengi wapo huko vyuo vikuu vya Tel Aviv, Jerusalem, Haifa na kwingineko nchini humo.
 
Back
Top Bottom