nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Na Godfrey Ismaely, Dodoma
MBUNGE wa Ole Rajab Mbarouk Mohammed (CUF), amemjia juu mbunge wa Geita, Bw. Donald Max (CCM) kwa kuifananisha Zanzibar na wilaya.Wakati akichangia
hotuba ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Bw. Max alisema kuwa wilaya ya Geita ina ofisa kilimo mmoja, wakati wilaya hiyo ni kubwa kuliko Kilwa na Zanzibar.
Baada ya mbunge kumaliza kuchangia hotuba hiyo, Bw. Mohammed, aliomba kutoa taarifa kwa Mwenyekiti wa bunge, Jenista Mhagama akisema kuwa mbunge aliyemaliza kuchangia ameitaja Zanzibar kama wilaya.
"Mheshimiwa Mwenyekiti naomba kutoa taarifa, mchangiaji aliyemaliza ameitaja Zanzibar kama wilaya.
"Naommba kumpa taarifa kuwa Zanzibar ni nchi, ina rais wake, katiba yake na bendera yake…tunataka hili suala likome," alisema Mohammed.
Akijibu hoja hiyo, Mhangama alisema kuwa taarifa hiyo imezingatiwa na itaingia kwenye hansard kwani inafahamika kuwa Zanzibar ni nchi.
MBUNGE wa Ole Rajab Mbarouk Mohammed (CUF), amemjia juu mbunge wa Geita, Bw. Donald Max (CCM) kwa kuifananisha Zanzibar na wilaya.Wakati akichangia
hotuba ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Bw. Max alisema kuwa wilaya ya Geita ina ofisa kilimo mmoja, wakati wilaya hiyo ni kubwa kuliko Kilwa na Zanzibar.
Baada ya mbunge kumaliza kuchangia hotuba hiyo, Bw. Mohammed, aliomba kutoa taarifa kwa Mwenyekiti wa bunge, Jenista Mhagama akisema kuwa mbunge aliyemaliza kuchangia ameitaja Zanzibar kama wilaya.
"Mheshimiwa Mwenyekiti naomba kutoa taarifa, mchangiaji aliyemaliza ameitaja Zanzibar kama wilaya.
"Naommba kumpa taarifa kuwa Zanzibar ni nchi, ina rais wake, katiba yake na bendera yake…tunataka hili suala likome," alisema Mohammed.
Akijibu hoja hiyo, Mhangama alisema kuwa taarifa hiyo imezingatiwa na itaingia kwenye hansard kwani inafahamika kuwa Zanzibar ni nchi.